STK ONE
JF-Expert Member
- Dec 31, 2011
- 627
- 184
Siyo mara yangu ya kwanza kushangazwa na hii sirikali ya JK wa pili. Hivi kwa nini watu wanakosa utashi wa kufanya mambo kwa akili zao na badala yake wanafanya kazi kwa kutumia akili za watu wengine? Mtu kama JK hivi kweli anafanya adha ambayo watu wanaipata kwa kukosa huduma za madaktari pale muhimbili?
Au anafanya hivyo kwa sababu hakuna ndugu yake ambaye anatibiwa MNH? Watu wanafanya kazi kwa kujituma kutoa huduma kwa mioyo yao yote halafu hawapati malipo kisha wanaambiwa wawe wazalendo.
Najiuliza, Uzalendo ni kufanya kazi bila malipo? Au ni kufanya kazi kwa uvumilivu usio na kikomo?
Kwa nini hili suala la Uzalendo linaelekezwa kwanza kwa wanfayakazi wa sekta za umma, kama madaktari, waalimu, polisi na wengine wengi? Kwa nini viongozi wa kuu wa serikali kama rais, waziri mkuu wake na wabunge siyo wazalendo? Au wao siyo watanzania?
Au wabunge wakiongozwa na Bi Kiroboto kudai posho za 200000/- ndiyo uzalendo? Mbona sijasikia rais kutaka kupunguza mshahara wake kuonesha uzalendo? Mbona sijasikia mawaziri wakakataa kutumia mashangingi ili kuokoa gharama kubwa za uendeshaji wa magari hayo ili kuelekeza fedha hizo kwenye huduma mbalimbali za jamii, au wao siyo Watz?
Naamini, kuna siku haya yote yataisha na tutaipata Tanzania yetu iliyopotelea kwa mafisadi wa CCM. Haya yatatokea tu kama wote kwa pamoja tutachukua hatua kwenye sanduku la kura.
Au anafanya hivyo kwa sababu hakuna ndugu yake ambaye anatibiwa MNH? Watu wanafanya kazi kwa kujituma kutoa huduma kwa mioyo yao yote halafu hawapati malipo kisha wanaambiwa wawe wazalendo.
Najiuliza, Uzalendo ni kufanya kazi bila malipo? Au ni kufanya kazi kwa uvumilivu usio na kikomo?
Kwa nini hili suala la Uzalendo linaelekezwa kwanza kwa wanfayakazi wa sekta za umma, kama madaktari, waalimu, polisi na wengine wengi? Kwa nini viongozi wa kuu wa serikali kama rais, waziri mkuu wake na wabunge siyo wazalendo? Au wao siyo watanzania?
Au wabunge wakiongozwa na Bi Kiroboto kudai posho za 200000/- ndiyo uzalendo? Mbona sijasikia rais kutaka kupunguza mshahara wake kuonesha uzalendo? Mbona sijasikia mawaziri wakakataa kutumia mashangingi ili kuokoa gharama kubwa za uendeshaji wa magari hayo ili kuelekeza fedha hizo kwenye huduma mbalimbali za jamii, au wao siyo Watz?
Naamini, kuna siku haya yote yataisha na tutaipata Tanzania yetu iliyopotelea kwa mafisadi wa CCM. Haya yatatokea tu kama wote kwa pamoja tutachukua hatua kwenye sanduku la kura.