hii ni rushwaa ya ngono...kwa kuwaa alishaa mkataliaa na ka mrecords,anawezaa akaendaa takukuru wakamchezeaa mchezo huyo boss mkware then waka mkamata na kumfungulia mastakaa.Kuna dada mmoja anaefanya kazi ofisi ya jirani ambaye huna tunakutana wakati wa kula na tumezoeana nae na hula pamoja na kupiga stori za hapa na pale.Juzi kaja akiwa mnyonge sana nikamuuliza vipi mbona umepooza sana leo akasema we acha tu sisi watoto wakike tuna mitihani mikubwa sana humu makazini.Anasema bosi wake amekuwa akimsumbua kwa muda mrefu eti anamtaka kimapenzi,huyo bosi kaoa na ana watoto wakubwa tu.Mara hii ya mwisho bosi kasema asipopata majibu mazuri hali yake pale kazini itaharibika na akikubali ataongezewa mshahara na marupurupu mengine kibao.Mara hii ya mwisho alipoitwa ofisini alihisi suala hilo litazungumzwa kwa hiyo akajifanya anachezea simu bosi alipokuwa anaongea pumba zake akarekodi yale mazungumzo anasema apeleka wapi ili hatua zichukuliwe?