Hivi ttcl wamelala au wanahujumiwa

Mtazamaji

JF-Expert Member
Feb 29, 2008
5,937
1,437
Wanajamvi wenzangu.
Kwa nini TTCL inashindwa uwa ISP No 1 nchini tena wa BROADBAND ya uhakika na bei nafuu?position yao kwenye Market share ya voice communication iko chini. Let assume kwa hilo hawana cha ufanya. But wht abaout other Data communication?

Naamini TTCL ina miundo mbinu ya cables na wiring amabayo kwanza iko underutilised sababu sasa hvi ni wateja wachache sana wana simu za landline.

Lakini Nina hakika VIongozi na wakurugenzi wa TTCL wanaweza kuwa Biggest Broadband Provider Tanzania. Sielewi kwa nini wakurugenzi wa hili shirika hawajafikiria kufanyia kazi hii . Au kuna watu wamo kwenye utawala wa hili shirika na ajenda yao kubwa ni kulihujumu kwa manufaa ya kampuni binafsi za mawasiliano.

Nahakika hata akija muwekezaji na kununua hili shirika mambo ya VOICE ataweka pembeni na effort zake kubwa itakuwa ni kwenye BROADBAND.

My advise kwa Viongozi wa TTCL. mmeshapigwa bao kwenye mambo ya VOICE amkeni mnaweza kuwapiga bao kwenye DATA.

Nawasilisha kwa mjadala
 
Mkuu Siasa zimejaa huko na si unajua ni shirika la umma so hakuna mwenye uchungu nalo. Watu wanaiba tuu wanavyotaka, wala usitegemee hao jamaa watafanya lolote lile la maana
 
Nilishasema weeeeeee lakini wapi.
Mie naomba waniazime shirika kwa mwaka mmoja on a rental basis waone nitakavyochanganya.
 
Nilishasema weeeeeee lakini wapi.
Mie naomba waniazime shirika kwa mwaka mmoja on a rental basis waone nitakavyochanganya.

Kwa kweli inasikitisha infastructrure zipo kama ni kuongeza kidogo sana. Sasa nadhani Shirika leye hisa za serikali Mteja wao mkubwa ni serikali. Hizo huduma za internat wanazota za dial up ni kituko.
 
TTCL inahujumiwa...kwenye kila eneo...hata ukiangalia kwenye pricing...wao bado wana gharama za juu...huo hule ushindani!
 
TTCL inahujumiwa...kwenye kila eneo...hata ukiangalia kwenye pricing...wao bado wana gharama za juu...huo hule ushindani!

Mkuu nadhani hii si kweli, nilikuwa bongo sometimes in January, nilitumia TTCL mobile for 2 weeks and was the cheapest and most reliable, lakini sikuwahi kuyiona wala kuisikia hata siku moja kwenye tv and or radio ads.
 
Mkuu nadhani hii si kweli, nilikuwa bongo sometimes in January, nilitumia TTCL mobile for 2 weeks and was the cheapest and most reliable, lakini sikuwahi kuyiona wala kuisikia hata siku moja kwenye tv and or radio ads.

Kwa kuwa bado huna uhakika...rudi kafanye utafiti ili kama unapinga nilichoandika huwe na uhakika zaidi!
 
TTCL inahujumiwa...kwenye kila eneo...hata ukiangalia kwenye pricing...wao bado wana gharama za juu...huo hule ushindani!

Ni kweli TTCL inahujumiwa, lakini hapo kwenye pricing angalia vizuri mkuu, au angalia bei hizi:http://www.ttcl.co.tz/internet_bandwidth2.asp#tariffs
Kama unamatumizi madogo ya 2gb/m unauziwa sh15 kwa mb1!! na kama unatumia 200gb/m wanakuuzia sh5/mb!!! (at 8mbps!). Hata kama haununui bando utatozwa 75/mb!
Hiyo ni kwa matumizi ya ofisini, kwa mobile users nadhani ni haki kutafuta otenetivu nyingine labda zantel.
Ni kweli ttcl bado huduma inasumbua wakati mwingine, lakini mostly wanatuunganisha kwa spidi na bei nzuri. (niliwahi kukaa bila mtandao miezi miwili wakati nalipa kila mwezi! nilikasirika nikawatukana sana, lakn waliporekebisha roho ikatulia nikaweka kando modem ya voda)
 
lakini sikuwahi kuyiona wala kuisikia hata siku moja kwenye tv and or radio ads.
Hili Nalo tatizo. labda ndio kuseam hawana cha Kutangaza. Ukisiakia sana sana bado wanajaribu kuprmote mambo ya Voice. Huko wameshapigwa bao.

Ni kweli TTCL inahujumiwa, lakini hapo kwenye pricing angalia vizuri mkuu, au angalia bei hizi:Products and Services
Kama unamatumizi madogo ya 2gb/m unauziwa sh15 kwa mb1!! na kama unatumia 200gb/m wanakuuzia sh5/mb!!! (at 8mbps!). Hata kama haununui bando utatozwa 75/mb!
Hiyo ni kwa matumizi ya ofisini, kwa mobile users nadhani ni haki kutafuta otenetivu nyingine labda zantel.
Ni kweli ttcl bado huduma inasumbua wakati mwingine, lakini mostly wanatuunganisha kwa spidi na bei nzuri. (niliwahi kukaa bila mtandao miezi miwili wakati nalipa kila mwezi! nilikasirika nikawatukana sana, lakn waliporekebisha roho ikatulia nikaweka kando modem ya voda)
Lakini kwa nini TTC wasijaribu kutumia promotion kuwa na flat rate charge kwa mwezi. Wanaweza wakaenga makundi matatu ya wateja.
wateja wanaotumia net kusurf tu mtandao. may be gharama ikawa 40,000 per month. Wateja wanatumia net kudurf kudowload kucheza michezo ya online labda gaharama ikawa 70,0000. Na mwish wakwa na wateja kwa wenye business na maofisi na kampuni labda 150,000.

Lakini naamini bado TTCL hawajutumia potential walizoanao kuwakata wateja wa majumbani. wateja wote waliowao kuwa na simu za landline wanaweza kuwa wateja wa TTCL true broaband sio ile Broadband ya wireless.
 
Binafsi naona hili shirika linaingizia serikali yetu khasara maana inaonekana wanatumia pesa bila kuzalisha...mimi ningeshauri wapige mahesabu mapato na matumizi waona kama vipi lijiendeshe lenyewe kwa khasara au waliue lifilie mbali.
 
Hivi wakuu, TTCL inatumia mfumo upi wa mtandao ule wa Cabling yaani au Satelite?

Mfumo wa cabling nafikiri ungewafaa sana TTCL.
 
I think, Kulink mikoa hadi mikoa wanatumia Land satelite......mimi sijui hawa jamaa wananini gharama zao ziko juu sana halafu net yao inakatakata speed sio nzuri kiivyo wanazidiwa na Zantel mbali tu.
 
Tatizo la hayo mashirika mnayoyaita ya umma yanakosa strategists ili kuona mbali na kuingia katika ushindani halisi!
 
Wazee shirika lahujumiwa ,kwa karibu wiki tatu nimelipia kuunganishiwa landlinendipo nikaletewa waya leo! huduma kesho isitoshe siku nilipopeleka maombi ilinichukua saa moja na nusu kukutana na mtu wa marketing ,hakukuwa na mtej yeyote siku hiyo yaani ilikuwa karibu niondoke-hapa nazungumziaTTCL _Zanzibar nadhani wanahujumu bila kujijua!
 
Sizani kama imetangazwa, but wako katika process ya kutafuta CEO mpya :tape:. Kwahiyo wenye qualification jiandaeni kuuza lugha. Ila tuu msiende na kikaratasi kujibu maswali ya interview
 
I think, Kulink mikoa hadi mikoa wanatumia Land satelite......mimi sijui hawa jamaa wananini gharama zao ziko juu sana halafu net yao inakatakata speed sio nzuri kiivyo wanazidiwa na Zantel mbali tu.

Kulink mkoa hadi mkoa kwa asilimia kubwa wanatumia microwave links, ila pia wanapitishia kwenye mkonge wa taifa kwenye maeneo ambayo mkonge umekamilika, pindi mkonge ukikamilika pande zote za nchi, connections zote za mikoa na wilaya zitapitia humo.

Currently suala la speed ndogo linachangiwa na vitu vipi, lakini zaidi ni capacity ndogo ziliyoweka kwenye hizi links hasa kwa kutegemea kuwa mkonge wa taifa ungekamilika mapema.
 
Hata mimi siwaelewi kabisa, rates zao haziendani kabisa..nimejaribu kuongea nao customer care siku moja,lakini kama hawaelewi...Zantel wataendelea kupeta
 
Hata mimi siwaelewi kabisa, rates zao haziendani kabisa..nimejaribu kuongea nao customer care siku moja,lakini kama hawaelewi...Zantel wataendelea kupeta

Siwezi kushangaa hata organisation structure ya shirika kama hili haiendani na zama hizi za Digital age. Unaweza kukuta Director wa finance ni mkubwa sana kicheo kuliko Director wa Internet Services( Sijui kama yupo) Sijui Mikoani kama kuna mameneja wa wameshafikiria kuwa na mameneja wa broadband

Kwa sasa nadhani mteja mkuwa wa hili shirika ni Serikali . na product au huduma kubwa inayoingiza pesa nyingi bado ni landline bado no voice communication
 
Hawa jamaa nilienda ofisi zao za TTCL Oysterbay nikajaza form kwa ajili ya fixed line mpya tarehe 28 June, hadi leo navyoandika hapa hawajanifungia hiyo line. Wanapita tu na gari lao la njano kila siku, wanachungulia then wanasepa. Nimeulizia wanasema wanafanya survey. Survey gani ya miezi miwili? Nimerudi ofisini kwao twice, wakasema wanafuatilia but nothing happens. So I gave up, naendelea na 3G modems zangu! Kuna yeyote mwingine limemtokea hili au mimi tu?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom