Hivi TTCL wamefilisika?

Mchokozi

JF-Expert Member
Feb 9, 2012
215
29
Naomba mwenye taarifa za ndani zaidi anifahamishe kwani sielewi mwenendo wa Kampuni Komgwe ya mawasiliano nchini (TTCL), nimesitushwa na kuona kwamba maeneo mengi yanayopata huduma ya simu za mezani kama Magomeni, Wageni, Osterdbay nk kwa hivi sasa hayana huduma hii. Mimi naishi Magomeni nilipofuatilia niliambiwa kuwa TeS sijui kitu gani haifanyi kazi,na nilipouliza itapona lini niliambiwa haijulikani na wala hakiponi ila wanabadilisha kwenda kwenye TeS nyingine na kwa sisi wateja wadogo simu zetu hazitaweza kupona, je suala hili ina maana walikuwa hawalijui? au TTCL wamefilisika kiungozi na Ufundi? Na kibaya zaidi tetesi nilizozipata nimeambiwa wafanyakazi walikuwa wanategemea kulipwa mshahara wa mwezi february leo 27/02/2012 lakini hata Salary Slip bado hazijatolewa. Mweye taarifa atufahamishe la sivyo je Hivi TTCL wamefilisika ??????
 
TTCL ni miongoni mwa mashirika mengi ya umma yanayopumua kwa mshine. Mengine ATCL (ambalo limebaki jina tu!), UDA (ambalo kila mtu amechukua chake hata parking).....
 
Kufilisika? Hii haiwezekani. Shirika hili ni la wasauz. Huduma wamezidiwa. Mashirika ya simu za mikononi ndiyo yanawazidi. Lakini hawawezi kufilisika.

Ni wajanja sana. Wanakula ki simba mwenda kimya. TAFAKARI.
 
tatizo linaloikumba TTCL ni management mbovu usitaka kuangalia maslahi mapana ya nchi, wachache wanaihujumu shirika hili na kuonekana kuwa kama shamba la bibi.ukirudi nyuma utatambua kuwa TTCL ni miongoni mwa mashirika ya kwanza tena kwa industry ya mawasiliano ilikuwa ni ya kwanza Tanzania na ilifanya vizuri hapo nyuma,ila baada ya madeni makubwa ya liosababishwa na taasisi za serikali ambazo hazikuwa tayari kulipa gharama ya matumizi ya simu kulingana na matumuzi yao ndio iliyoifikisha TTCL hapo ilipo, pili kuingia kwa makampuni mengine ya simu Tz ni Miongoni mwa sababu ziliopelekea TTCL kufikia hapo ilipo sasa, japo walikuja kushtuka kuanzisha simu za kiganjani kwa kuchelewa, sasa wamekuwa mzigo kwa serikali na kwa walipakodi
 
Mi niliwachukia sana simu yangu ya mezani nimeripoti ubovu tangu Jauari 28 mwaka huu na baadae tarehe 2,7, na 9 Februari lakini mpaka leo hakuna kilichofanyika. Kama wanalipwa mishahara ni kwamba wanatuibia kodi zetu watanzania..
 
Back
Top Bottom