Hivi TanzaniteOne inanufaisha nchi yetu au ndio shamba la bibi?

fredmlay

JF-Expert Member
Apr 30, 2008
1,849
388
Wana jamvi habarini za leo.
Nilikuwa napitia financial report za kampuni ya TanzaniteOne (ambazo hazijakaguliwa bado) inayofanya shughuli za uchimbaji madini ya Tanzanite Mererani Simanjiro. Kuna mambo mengi hayajakaa vizuri ila nataka kuzungumzia moja tu.

Nimesahangazwa na kiasi kidogo cha mrahaba kilicholipwa serikalini huku kampuni ikionyesha kuzalisha kwa mwaka 2010 carats 2,200,000 sina hakika kama hii ni polished au rough maana hawajasema, lakini ndugu zangu kwa soko lilivyokuwa mwaka jana hapa Arusha, carat 1 ya polished Tanzanite ilikuwa ikiuzwa kati ya US $180 – US $200

Kwa carats walizopata kwa mwaka huo, mathalani tuchukulie ni rough zikiwa polished wangepata carats 1,100,000 ambazo kwa bei ilivyokuwa hapa Arusha thamani yake ingekuwa US $198 mil – US $220 mil

Kwa taratibu za serikali kupitia idara yao ya madini serikali ilipaswa kukusanya kiasi kisichopungua US $5.94mil badala ya US $0.4mil zilizokusanywa kulingana na hesabu zao (hii ni kama carat 2,200,000 zilikuwa rough na si polished) kwa mwaka kama kiasi walichokiri kuzalisha kitakuwa exported, hata hivyo kuna uhakika kwamba Tanzanite wanayozalisha huwa haibaki hapa nchini bali hupelekwa Africa Kusini kwa maandalizi ya kuiingiza katika soko la dunia, huko penye bei nzuri zaidi kuliko hizi hapa kwetu. Na pia ikumbukwe mrahaba kwa wafanyabiashara ya madini hulipwa hata kabla ya mauzo kufanyika ilimradi madini yametoka nchini.

Pia ieleweke kwamba mkataba wao wa kuwepo hapa nchini kiuwekezaji unakamilika mwaka 2012 na inaonekana wanajiandaa ku-lobby ili mkataba uongezwe ikiwa ni pamoja na kubadili jina la kampuni yao na kuwa Richland Resources Ltd

Kazi kwetu wadanganyika, tukomae na serikali ikiwezekana hao wanyonyaji waondoke watuachie madini yetu

Ukitaka kupitia hizo account waweza download
 

Attachments

  • TZOne-FS2010.pdf
    197.4 KB · Views: 27
Jinsi hawa jamaa wanavyo vuna haya madini utaona ni wizi mtupu, nionavyo mm ni Shamba la Bibi.
 
Fredy kwenye suala la uhuru sio kwenye madini tu bali kila kona ya uchumi wa nchi yetu tumeibiwa na tusipoamka leo miaka kumi ijayo tutakuwa siyo watumwa tena kwenye nchi yetu bali tutakuwa kama wakimbizi ndani ya nchi yetu wenyewe huku wao wakiwana mkate na kutupaa mabaki
 
Fredy kwenye suala la uhuru sio kwenye madini tu bali kila kona ya uchumi wa nchi yetu tumeibiwa na tusipoamka leo miaka kumi ijayo tutakuwa siyo watumwa tena kwenye nchi yetu bali tutakuwa kama wakimbizi ndani ya nchi yetu wenyewe huku wao wakiwana mkate na kutupaa mabaki
ndugu yangu mwisho tutabaki na maeneo ya kuektia movie (mashimo/mahandaki)
 
Kuna haja ya kuzinduka na kudai uhuru wa nchi yetu

Fred, siku zote tumekuwa tunasikia makosa ya Barrick. Hatusikii kuhusu makampuni mengine ya uchimbaji wa madini. Tanzanite One wana madudu kushinda Barrick. Binafsi nimefika Merereni na hakuna sehemu 'watu wanaishi kwa umaskini' kama Merereni. It is beyond words! wachimbaji wadogo na watoto (wanawaita nyoka) wanaishi kwenye vijihema vilivyotengezwa na mifuko ya 'salfeti' na rambo. Sijui analalaje binadamu mle maana urefu kwenda juu hauzidi mita 2! Ni afadhali banda la kuku.

Wazungu wamezungusha uzio eneo lote lenye mwamba wa Tanzanite, hawa wachimbaji wadogo wako pembeni . Ni hivi, assumekuna duara , jiwe liko katikati ya duara then wachimbaji wadogo wanazaaga nje wa mduara. Kwa hiyo wanachimba kutoka huku pembeni kutafuta mwamba, it will take years kufika huko.Nilikuta na mtu kakaa huko zaidi ya miaka 10 hajapata kitu!

Sio maji, sio barabara Merereni na unaweza kujuwa ni mchimbaji gani mdogo kaja siku za karibuni kwa kuangalia kachafuka kiasi gani! Kuna barabarani wamechonga hawa wazungu lakini waafrika au nisema wachimbaji wadogo hawaruhusiwi.

Kituko: chunguzeni shareholders wa Tz? Balozi Amy Mpungwe ndio Chairman wa hawa wakubwa. Ni nani anaweza kuniambia miradi ya kijamii ya Tanzanite One? iko wapi? na wametoa kiasi gani hawa wakubwa?

Sijui nani anaandaa hii mikataba lakini niseme wakati umefika kwa BUNGE kutunga sheria itakayotamka waziwazi kuwa mwanasheria mtanzania akishiriki kuandaa mkataba wa KINYONYAJI kwa nchi afungwe kwa miaka mingi sana (he/she a danger to socierty). Sio faini, kifungo jela na sio chini ya miaka 10. Mererenani kuna matatizo ndugu zangu. Kuna udhalilishaji wa ajabu.
 
Back
Top Bottom