Hivi Tanzania kuna MacDonalds?

Ndio, Junk Food ni jina(lisilo rasmi) kwa vyakula ambavyo havina virutubisho vya muhimu kwa afya ya binadam,au kama vipo basi vinachanganywa na vitu ambavyo vina madhara katika afya ya mlaji. Haya na wewe unajua maana gani zaidi?

...kwa maana hiyo zile Burgers, coleslaw na fries hazina virutubisho muhimu mwilini? Kama unakubali vipo, preservatives gani unazojua wewe zinamadhara kwa binaadamu? acheni propaganda nyie... "Junk food" ni neno tu lilokaliwa kidedea kusisitiza umuhimu wa balanced diet, period!

Burger yenye salad na fries unaweza kulinganisha lishe yake na ubwabwa na maharage ya mama ntilie? acheni hizo bana...BTW, kule vijijini wanakula Organic products, kuanzia mapapai, matembele, mihogo na kisamvu chake nk, wala tusijilinganishe nao kwenye masuala ya mlo bora!

Mkuu, watalii wengi wanakuja kwetu ili waonje vitu tofauti. Ndio mana utawaona wengi wanakwenda sehemu kama Chef's Pride pale mjini n.k. Wewe unafikiri wanalipia ticketi za ndege ili waje kula McDonald's/KFC huku? By the way, wengi wanaofurahia hizo fast food joints huku "ulaya" ni wahamiaji, si wazawa!!!

...ooh, ok...

Kwa ufafanuzi mzuri, watalii wa aina hiyo wamo kwenye kundi la Drifters/Backpackers. Watalii wa aina hiyo wengi wao ni wanafunzi walio kwenye Gap years, nk. Watalii wa namna hiyo kule unguja huitwa 'vishuka'.
Vile vile watalii wa namna hiyo hujichanganya na wenyeji katika usafiri wa mabasi, treni nk. Si ajabu kupigana nao vikumbo kwa mama lishe...

Watalii hao huwezi kuwalinganisha na Business travellers, au waliomo kwenye package holidays, au expatriates...

Binafsi ningehitaji uthibitisho wa kina kuhusu hilo la immigrants kuwa walaji kwa asilimia kubwa kwenye hizo fast food joints
 
kama hamtaki macd kwa nini sasa mnakunywa vinywaji kama cocacola?? kwa nini msinywe madude mengine unayoyatengeneza mwenyewe??
 
kama hamtaki macd kwa nini sasa mnakunywa vinywaji kama cocacola?? kwa nini msinywe madude mengine unayoyatengeneza mwenyewe??

...na kweli, ma additives kibao mle kwenye cocacola mpaka watengenezaji wanafanya siri hiyo recipe! ...Kinywaji gani hicho hata ukimwaga kwenye sink la choo linasafishika?

Kunyweni togwa nyie!
 
Baada ya kupitia baadhi ya posts hapa naweza kusema kuwa watanzania wengi bado tumejawa na imani za kijamaa na kuwa kila kitu kutoka magharibi ni kiovu.
Sasa mbona mmekubali Steers (sawa na Mickey D's?), Spurs (wana ribs nzuri kwa standard yao) zifunguliwe au kwa kuwa ni za South africa?

Kazi kweli kweli.
 
Hakuna chakula mbaya unhealthy kama McD,bora watu waanzishe franchise za vyakula vyetu wenyewe kama ugali,wali na mboga mboga,haya mambo ya mikate na burgers ni vyakula vyao...nafikiri mtalii atafurahi sana akija bongo na kula ugali,maharage na milenda yetu kuliko hizi burger za Mcd!

Koba niko pamoja nawe.

Huyo investor wa kula macdonald ndio yale yale ya 'mainvestor' wa kichina waliojaa kariakoo. Investor wa uhakika atakwenda kula sehemu zenye hadhi na sio kwenye junk food.

Kabla ya kushabikia ajira tuangalie pale Subway karibu na office za KLM wana wafanyakazi wangapi? Kuhusu suala la kutumia malighafi zetu kwa wale wanaokula Steers zile juice za unga ni vipi kwani hakuna matunda Tanzania? Je mmewahi kuta kuna Sato au Sangala salad zaidi ya Tuna salad na hizo tuna ni za kopo na ni imported.

Ingekuwa vyema tukashabikia franchise za mtu kama Jamaa Fast Food ambae anatumia malighafi zetu, vyakula salama na bei zake ni more affordable.
 
kwa hiyo wewe kwa nini hutaki macdonald tanzania? kwani ni lazima uende kula??

Kwani Macdonald kuna nini cha ajabu ndugu zangu hadi inakuwa shida hapa ndani ya jamvi!
Kama itakuja Tanzania ni vema pia ili kwa yule ambae hajawahi kula Macdonald akale na aone tofauti na incase kama haitakuja basi wewe ambaye unaisikia tu usijione kama kuna kitu unakikosa sana mi naukubali sana ugali nyama choma wa bongo kuliko hii MacD.
Kikubwa hapa naona hawa watu waliopo nje ya bongo wanataka waonekani kama wao wanakula vitu vizuri sana kuliko wenzetu kitu ambacho si sahihi hata kidogo.
Misosi ya home ni natural bwana hadi nimeimiss!
 
Wakuu ningependa kufahamishwa kama Tanzania macdonald ipo na kama haipo kwa nini?
Haipo maana watakosa biashara. Hawa watanzania wamezoea kunywa uji wa mbege, ndizi nyama, chapati maharage iwe asubhuhi, mchana na jioni. Nashangaa kama watajua jinsi ya kushika hilo liburger la Mcdonald lilivyo likubwa. Basi wanadai ni chakula cha mzungu maana mzungu hali kizito kama mwafrika. Hebu nipe tano
 
Koba niko pamoja nawe.

Huyo investor wa kula macdonald ndio yale yale ya 'mainvestor' wa kichina waliojaa kariakoo. Investor wa uhakika atakwenda kula sehemu zenye hadhi na sio kwenye junk food.

Kabla ya kushabikia ajira tuangalie pale Subway karibu na office za KLM wana wafanyakazi wangapi? Kuhusu suala la kutumia malighafi zetu kwa wale wanaokula Steers zile juice za unga ni vipi kwani hakuna matunda Tanzania? Je mmewahi kuta kuna Sato au Sangala salad zaidi ya Tuna salad na hizo tuna ni za kopo na ni imported.

Ingekuwa vyema tukashabikia franchise za mtu kama Jamaa Fast Food ambae anatumia malighafi zetu, vyakula salama na bei zake ni more affordable.

...absolutely! kilichopo sasa ni Jamaa Fast Food ku maintain standards ili migahawa yao iwe kwenye ngazi za kitaifa mpaka kimataifa. Sio unakuta vitumbua na sambusa za jana na juzi tofauti na za kesho kwa ladha hadi ubora. Hivyo hivyo kwa waajiriwa, na aura ya migahawa yenyewe...

Kwani Macdonald kuna nini cha ajabu ndugu zangu hadi inakuwa shida hapa ndani ya jamvi!
Kama itakuja Tanzania ni vema pia ili kwa yule ambae hajawahi kula Macdonald akale na aone tofauti na incase kama haitakuja basi wewe ambaye unaisikia tu usijione kama kuna kitu unakikosa sana mi naukubali sana ugali nyama choma wa bongo kuliko hii MacD.
Kikubwa hapa naona hawa watu waliopo nje ya bongo wanataka waonekani kama wao wanakula vitu vizuri sana kuliko wenzetu kitu ambacho si sahihi hata kidogo.
Misosi ya home ni natural bwana hadi nimeimiss!

...Mvina, hakuna cha ajabu kwenye MacDonald, ni mjadala juu ya "Brand" ilokusudiwa wateja wa aina fulani. Kuitetea au kuikosoa haina maana waliopo nje wanafwaudu na waliopo nyumbani wanakosa, kila mtu na taste yake almuradi roho inapenda.

Mteja wa Burger King huenda asishawishike kabisa na MacDonald, sawa sawa na tofauti ya wateja wa Chef's pride mtaa wa Libya na Royal Chef pale Lumumba...
 
Kwa kudra ya mwenyezi Mungu McDonalds haipo Tanzania. Najua kwa wale ambao hawajawahi kuiona au wanaoisikia wanaweza kusema ni bahati mbaya. Lakini kwa kuwa vyakula vyenyewe ni junkie (unhealthy food), kama vikija hapa Tanzania igefaa wapatiwe zaidi wale walio malnuorished. Maana kulidigest big mac moja lile la supersize unaweza kulidigest kwa siku tatu, linafaa sana kwa watu hao. Lakini tatiz0 ni affordability.
 
MacDonald Hakuna ila unaweza kupata steer,Nandos,Subway na Merry brown
Hata hard Rock ilipata kuwepo Pale kwa mbowe lakini ilishafungwa kitambo Sana
Tatizo nadhani bado waendeshaji hawakidhi au kifikia Standard wanazotaka wenyewe
lakini mpaka mwaka jana bado nile perch sangara wa Tanzania ndio alikuwa akitumiwa rasmi na Macdonald kama Fish Burger kila ilipo MacD .....l Fikiria avuliwe mwanza apelekwe nairobi Kenya baada ya muda US mpaka aje kuliwa ni kweli ni hana tena ladha lakini inawezekana unataka kujuwa ili uje ufungue huku pia anagalia kama (KFC)kentucky,Burgeland,Pizza hut,Planet Cafe ukipenda nenda nairobi kachukuwe Mfumo wa WIMPY ili uje na mfumo wako Maana Azam kashindwa kiana karibu Bongo Nyani!
 
haipo maana watakosa biashara. Hawa watanzania wamezoea kunywa uji wa mbege, ndizi nyama, chapati maharage iwe asubhuhi, mchana na jioni. Nashangaa kama watajua jinsi ya kushika hilo liburger la mcdonald lilivyo likubwa. Basi wanadai ni chakula cha mzungu maana mzungu hali kizito kama mwafrika. Hebu nipe tano

Kula tano mkuu!!! Aahhahaha
lazima tuilete tuone kama hawatakuja??
 
kama hamtaki macd kwa nini sasa mnakunywa vinywaji kama cocacola?? kwa nini msinywe madude mengine unayoyatengeneza mwenyewe??

Prevention is better than cure. Kama cocacola ina hizo harmful additives basi isiwe sababu ya kutuongezea more harmful stuff(McDonalds). What we've consumed is enough,what don't need any more of that. Acheni ulimbukeni wa cheap western foods. A person of your age and calibre should feel shy going to fast food joints to eat burger. Eat healthy food,take care of your own body and health. Start now!
 
Prevention is better than cure. Kama cocacola ina hizo harmful additives basi isiwe sababu ya kutuongezea more harmful stuff(McDonalds). What we've consumed is enough,what don't need any more of that. Acheni ulimbukeni wa cheap western foods. A person of your age and calibre should feel shy going to fast food joints to eat burger. Eat healthy food,take care of your own body and health. Start now!
You really dont know what your talking about!!
 
...hivi tuna matatizo ya ukomo wa kufikiri?



...mawazo yale yale ya Ubepari ni adui wa haki!



...kwani unalazimishwa ule?



...yale yale,...! target ni kina nani kaka?



...angalau wewe umeangalia nje ya boksi!



..hebu waulize...



...hii ndio athari ya kila kizuri tunasema cha kizungu.

Bandugu mna bore!...

Hivi mnadhani kilio cha serikali watalii/expatriates waje kwa wingi Tanzania maana yake watakula kwa mama Ntilie? au mnataka wale huo ugali na nyama choma mnazozifagilia hapa?

Hamjaweza fikiri MacDonalds watawezesha ajira ngapi hapa nchini? kuanzia wafugaji, wafanyakazi, suppliers, nk? Leo hii hamuoni faida ya Mahoteli ya kitalii, Supermarkets chache tulizonazo, au Mlimani City kwa mfano mdogo?

Hatuwezi kuishi kwa kutarajia mama ntilie atakidhi mahitaji ya watu wote wanaoishi Mijini.

Kwa taarifa yenu, watalii wengi kwenye vigezo vya health & safety hupendelea kula kwenye known/tried and tested franchise kama hizo tajwa hapo awali, ikiwemo KFC, Burger King, Nandos etc, sio kwa mama Ntilie!

Msidhani kuwa kuiga mifumo ya kimagharibi ni dhambi ati tu kwakuwa Mwl Nyerere alisema wao ni makabaila na wanyonyaji! Tumejiingiza kwenye mfumo wa soko huria, lazima twende na matakwa yake.

Yaani MBU- niliposoma hoja zako imebidi nami nijibu thread hii.

Si kweli , uanzishwaji wa MCd, Wendy, KFC, na nyinginezo zitawavutia watalii kuja kwa wingi katika nchi zetu na kula vyakula hivyo. Watalii wengi wanapokwenda kutembelea ughaibuni wanataka kuonja vyakula vya wenyeji, changamoto iliyopo ni kutengeneza vyakula vya kienyeji, katika hali ambayo itavutia wageni, kwa kuzingatia usafi, viwango nk...

Mahali popote duniani , sekta ya utaliii, inavutia wengi kwa jinsi ambavyo wenyeji wameweza kutunza utamaduni wao,vivutio vyao vinavyotambulisha eneo na huo utamaduni ndiyo unawavutia watalii kujifunza,kujaribu ustaraabu au kuushangaa ustarabu huo, kwani hujasikia ukitaka kushangaa nenda feli!!!! Anyway somo la vivutio vya utalii na utalii wa aina gani ni somo pana, ambalo linahitaji muda zaidi.

Tatizo lilipo kwa watanzania wengi, ambao wameenda nje na wanataka kufanya biashara Tanzania, wao huangalia business concept za nje na kuleta hapa kwetu kama copy bila kuzingatia hali halisi ya nchi husika ( local situations) , sikatai kwamba unaweza kufanikiwa kwa njia hizo !!

Lakini ninategemea mtu ambaye ameenda nje na anataka kufanikiwa kikwelikweli na kuleta mguso katika uchumi wa nchi kama Tanzania, aje na wazo mbadala kwa kutumia mazuri aliyoyaona nje, na hapo ndiyo anakuwa amepata elimu ya kupambana na mazingira yake.

Kwa mfano, fast food za kitanzania unavyoweza kuanzisha, ni kupika vyakula vyetu kwa mapishi ya kitanzania,halafu ukatumia business concept za fast food za Ulaya / Marekani, ikiwa unaweza kuweka mfumo ambapo mtu anakuja na gari anaagiza na anapewa chakula,kulipa akiwa kwenye gari. Hapa Tanzania watu wengi sasa wana magari, lakini biashara nyingi, hawafikiri hata kujenga parking lot za kutosha, au kuhudumia watu wakiwa ndani ya magari na vile vile kuhudumia watu watu wasiokuja kwenye biashara yako kwa home delivery nk , nk.

Mtu aliye serious anaweza akafungua franchise yake kwa concept ya kitan zania na akafanikiwa, anahitaji kujua juu ya food quality, to establish a network of reliable food suppliers na kutengeneza mfumo wote mzima.

Jamani nawakilisha kwa sasa, ili na wengine wachangie, lakini WILL BE RIGHT BACK.
 
Yaani MBU- niliposoma hoja zako imebidi nami nijibu thread hii.

Si kweli , uanzishwaji wa MCd, Wendy, KFC, na nyinginezo zitawavutia watalii kuja kwa wingi katika nchi zetu na kula vyakula hivyo. Watalii wengi wanapokwenda kutembelea ughaibuni wanataka kuonja vyakula vya wenyeji, changamoto iliyopo ni kutengeneza vyakula vya kienyeji, katika hali ambayo itavutia wageni, kwa kuzingatia usafi, viwango nk...

Mahali popote duniani , sekta ya utaliii, inavutia wengi kwa jinsi ambavyo wenyeji wameweza kutunza utamaduni wao,vivutio vyao vinavyotambulisha eneo na huo utamaduni ndiyo unawavutia watalii kujifunza,kujaribu ustaraabu au kuushangaa ustarabu huo, kwani hujasikia ukitaka kushangaa nenda feli!!!! Anyway somo la vivutio vya utalii na utalii wa aina gani ni somo pana, ambalo linahitaji muda zaidi.

Tatizo lilipo kwa watanzania wengi, ambao wameenda nje na wanataka kufanya biashara Tanzania, wao huangalia business concept za nje na kuleta hapa kwetu kama copy bila kuzingatia hali halisi ya nchi husika ( local situations) , sikatai kwamba unaweza kufanikiwa kwa njia hizo !!

Lakini ninategemea mtu ambaye ameenda nje na anataka kufanikiwa kikwelikweli na kuleta mguso katika uchumi wa nchi kama Tanzania, aje na wazo mbadala kwa kutumia mazuri aliyoyaona nje, na hapo ndiyo anakuwa amepata elimu ya kupambana na mazingira yake.

Kwa mfano, fast food za kitanzania unavyoweza kuanzisha, ni kupika vyakula vyetu kwa mapishi ya kitanzania,halafu ukatumia business concept za fast food za Ulaya / Marekani, ikiwa unaweza kuweka mfumo ambapo mtu anakuja na gari anaagiza na anapewa chakula,kulipa akiwa kwenye gari. Hapa Tanzania watu wengi sasa wana magari, lakini biashara nyingi, hawafikiri hata kujenga parking lot za kutosha, au kuhudumia watu wakiwa ndani ya magari na vile vile kuhudumia watu watu wasiokuja kwenye biashara yako kwa home delivery nk , nk.

Mtu aliye serious anaweza akafungua franchise yake kwa concept ya kitan zania na akafanikiwa, anahitaji kujua juu ya food quality, to establish a network of reliable food suppliers na kutengeneza mfumo wote mzima.

Jamani nawakilisha kwa sasa, ili na wengine wachangie, lakini WILL BE RIGHT BACK.

...ohooo,... sikusema McDonald ni kivutio cha utalii bana,...! Niliijengea hoja kwa watalii kwakuwa ni worldwide brand hivyo haitawawia tabu kuhangaika sehemu za quick snack!

Likewise kwa mahoteli kama Kempinsky, Movenpick, Serena nk yaliyopo Tanzania, yote hayo ni 'kivutio' sio kwasababu ya majengo, bali Brand -'tangible products'- ambazo ni matarajio mwa watalii/wageni kuhusiana na makampuni hayo.

second, pale village museum -kijitonyama kuna vyakula vya kiasili, niambie wazungu/watalii wa aina gani humiminika pale 'kuonja' mseto, mlenda na kivunde? Wachache sana. Sababu? Marketing mbovu? la hasha...

No wonder hata kwenye mahoteli tajwa hapo juu 99.5% ya menu's zao na vinywaji ni International based i.e middle eastern, far eastern, (Mediterranean) french, Italian, Greek na kidoogo Turkish. Hukuti Togwa wala makande mjomba, kwakuwa sio 'soko' lake hilo!
 
Mbu napenda unavyofikiri,

It's true watu wengi huamini jina la baadhi ya products ili waweze kununua. So there is nothing bad kwa macD kuja wenye kuipenda watenda wasioipenda wataacha.

Mbona hamlalamiki kuhusu sigara kiwanda kifungwe wakati sigara haina faida yoyote kwa mwili wetu?

Nadhani ni vizuri kuwa na variety ili watu waweze kuchagua na kwa wale waliopigania vyakula bora pia nanyi mliweke katika utekelezaji hao wenye junk food wanavyoyaweka mawazo yao. tusiishie kuwapinga wakati huwapi watu option ya kuchagua.

Nchi ni huru so kila mtu ana haki ya kufanya apendayo so tusiishie kupinga bali nasi tufanye yale tunayoona ni sahihi
 
Back
Top Bottom