Simba Mkali
JF-Expert Member
- Jan 31, 2012
- 620
- 239
Kuna mradi wa umeme pale Dodoma katika kitongoji cha Kikuyu Kinyambwa ambako wananchi wameahidiwa kupewa nguzo na Tanesco ili waanze kupata umeme wa mradi lakini mradi umekwama kwa kuwa wafanyakazi wa chini wa Tanesco Dodoma wanadai rushwa kwa wananchi wa kawaida. Hadi sasa wananchi wachache waliowekewa nguzo hizo ni wale waliotoa kidogodogo na wale ambao hawajatoa chochote nguzo zimeng'olewa.
Suala hili Mwenyekiti wa mtaa analijua, Diwani analijua, meneja wa Tanesco analijua na hata Injiani wa Tanecso Dodoma analijua, je Takukuru wapo hai? kwanini wanaacha wananchi wanyonge ambao hawana uwezo wa kutoa rushwa wanyanyaswe? au na wao wameshakatiwa chao?
Suala hili Mwenyekiti wa mtaa analijua, Diwani analijua, meneja wa Tanesco analijua na hata Injiani wa Tanecso Dodoma analijua, je Takukuru wapo hai? kwanini wanaacha wananchi wanyonge ambao hawana uwezo wa kutoa rushwa wanyanyaswe? au na wao wameshakatiwa chao?