Ta Muganyizi
R I P
- Oct 19, 2010
- 5,361
- 2,734
Nimesoma muda mrefu na kusikiliza makundi mbalimbali humu nchini pamoja na wananchi kwa ujumla dalili zote zinaonesha watanzania wamechoka.
Kama kuna mtu aliangalia TBC jana muda wa saa 4:30 utaona wazee na vikongwe walivyokata tamaa ya kuishi. Wengine walidiriki kusema wanasubiri kufa tu maana wanaona hata aibu kusema wao ni watanzania ambao wanaishi katika nchi ambayo inaamini maisha bora kwa kila mtanzania. Serikali iliwatoza kodi walipokuwa vijana na kilichoko sasa ni matunda ya juhudi zao wakiwa na nguvu za kuzalisha, lakini sasa wao wanaoneka ni takataka.
Pili ndani ya ccm watu wanaona jinsi nchi ilivyoenda mrama kila anayetaka kuiba anaiba tu raslimali hakuna wakusema chochote. Madini yanazidi kuibiwa, miundo mbinu kama reli vimeharibika, umaskini unaongezeka, ufisadi ndo usiseme yaanin kila kitu tabu lakini mkuu wa kaya kimyaaaaaaaa.
Wananchi woote wanashangaa wanajua kabisa kuwa nchi iko pabaya. Sasa njia muafaka ni ipi?
Mapinduzi........mapinduzi.........mapinduzi inabidi yafanyike tena ya umma kama huko Tunisia lakini nani aanzishe? Watu waoga kama nini. Wamechoka na uonevu lakini maneno ya kulaumu ndo mengi. Sasa inabidi tutoe maneno ya kufikia muafaka tufanyeje? Nikitoa ushauri hapa si ajabu thread hii ikaondolewa kuwa nitasababisha matatizo nchini hivyo tubaki hivi hivi tu jamaa waendelee kuila nchi yetu. Siku moja nilishauri kuwa Jwtz waangalie mwenendo wa nchi lo!. Naomba tukubalianae katika jukwaa hili tufanyeje ili tubadilishe hali hii. Lile la kusubiri uchaguzi hadi 2015 naona limezoeleka na bado kura zitaibiwa tu. Waadhiri vyuo vikuu wamechoka, wanafunzi wamechoka, wafanyakazi wamechoka, polisi hoi wanaona ni bora walale kwenye lindo kule benki kuliko home kwao walikopanga, kila sekta wamechoka sasa tunasubiri nini?
Naomba wadau mtaje hapa chini nani aanzishe ili wengine tufuate.... nikieleza mie kama hapo awali thread inapotea. Jamani ni hivi "Bora kuwa maskini lakini huru, kuliko kuwa tajiri lakini mtumwa" Mapinduzi muhimu jama na muda ndo huuu, tuandamane nchi nzima auuuu????? na nani aanzishe kutoa tamkoooo????? aghhh. Jeshi la JWTZ si kweli kuwa la wananchi, linalinda wachache aaaahh. Nikiendelea nitaambiwa mie mhaini, jamani kulaumu kumeisha tutoe suluhishoooo. Tajeni basi hapa chini nani aanzishe??? Mie nampendekeza Mwakyembe wewe je?
Kama kuna mtu aliangalia TBC jana muda wa saa 4:30 utaona wazee na vikongwe walivyokata tamaa ya kuishi. Wengine walidiriki kusema wanasubiri kufa tu maana wanaona hata aibu kusema wao ni watanzania ambao wanaishi katika nchi ambayo inaamini maisha bora kwa kila mtanzania. Serikali iliwatoza kodi walipokuwa vijana na kilichoko sasa ni matunda ya juhudi zao wakiwa na nguvu za kuzalisha, lakini sasa wao wanaoneka ni takataka.
Pili ndani ya ccm watu wanaona jinsi nchi ilivyoenda mrama kila anayetaka kuiba anaiba tu raslimali hakuna wakusema chochote. Madini yanazidi kuibiwa, miundo mbinu kama reli vimeharibika, umaskini unaongezeka, ufisadi ndo usiseme yaanin kila kitu tabu lakini mkuu wa kaya kimyaaaaaaaa.
Wananchi woote wanashangaa wanajua kabisa kuwa nchi iko pabaya. Sasa njia muafaka ni ipi?
Mapinduzi........mapinduzi.........mapinduzi inabidi yafanyike tena ya umma kama huko Tunisia lakini nani aanzishe? Watu waoga kama nini. Wamechoka na uonevu lakini maneno ya kulaumu ndo mengi. Sasa inabidi tutoe maneno ya kufikia muafaka tufanyeje? Nikitoa ushauri hapa si ajabu thread hii ikaondolewa kuwa nitasababisha matatizo nchini hivyo tubaki hivi hivi tu jamaa waendelee kuila nchi yetu. Siku moja nilishauri kuwa Jwtz waangalie mwenendo wa nchi lo!. Naomba tukubalianae katika jukwaa hili tufanyeje ili tubadilishe hali hii. Lile la kusubiri uchaguzi hadi 2015 naona limezoeleka na bado kura zitaibiwa tu. Waadhiri vyuo vikuu wamechoka, wanafunzi wamechoka, wafanyakazi wamechoka, polisi hoi wanaona ni bora walale kwenye lindo kule benki kuliko home kwao walikopanga, kila sekta wamechoka sasa tunasubiri nini?
Naomba wadau mtaje hapa chini nani aanzishe ili wengine tufuate.... nikieleza mie kama hapo awali thread inapotea. Jamani ni hivi "Bora kuwa maskini lakini huru, kuliko kuwa tajiri lakini mtumwa" Mapinduzi muhimu jama na muda ndo huuu, tuandamane nchi nzima auuuu????? na nani aanzishe kutoa tamkoooo????? aghhh. Jeshi la JWTZ si kweli kuwa la wananchi, linalinda wachache aaaahh. Nikiendelea nitaambiwa mie mhaini, jamani kulaumu kumeisha tutoe suluhishoooo. Tajeni basi hapa chini nani aanzishe??? Mie nampendekeza Mwakyembe wewe je?
Ndugu zangu watanzania naumia sna na mambo yanavyokwenda katika hii nchi yetu kipenzi iitwayo Tanzania Ambayo kwa wachache wananiita Shamba la bibi kwa kuwa mjanja masikini anaweza amka tajiri.
1. Tumeona na kiusikia mmiliki wa DOWANS ametua nchi tena na kafanya Press Conference lakini hakuna reaction zozote toka kwetu wakati huyu ndiye anayesababisha matatizo na umasikini wote unaokuwa kwa kasi kila kukicha.
2. TANESCO wamepandisha gharama za umeme hakuna reaction zozote toka kwetu na mbaya zaidi gharama zimepanda na umeme ndio hakuna kabisa upo wa machale tuu unatusaidia kunyoosha nguo na kuonekana smart mtaani.
3. Nauli za mabsi yaendayo mikoani nazo zinapanda, tutashindwa hata kwenda salimia wazee wetu mikoani. nao watashindwa kuja kutusalimu au hata kuja kwa ajili ya matibabu zaidi kwa magonjwa yaliyoshindikana huko. Fanya reference Tanzania Daima ya jana tarehe 23/02/2011.
4. Gharama za maisha nazo zinapanda kwa kasi hebu chukulia bei ya sukari ilivyopanda mara dufu mwezi januari ilikuwa 1600/=Tshs leo huku ni 2500/= kwa kilo.
5. Maji na bado historia kwa watanzania tuliowengi, maji tunayaona kwa masaa yasiozidi matau na ndg zetun kule vijijin maji yenye rangi nyeupe (Water is Colorless) hawajawahi kuyaona wengine mpaka wanakufa.
Haya yote hakunja kiongozi wa serikalini au hata vyama vya siasa wanashutuka kwa mambo yanavyokwenda, watanzania tumenyamaza kana kwamba hakuna linalo tutafuna na kutuumiza ndio maana najiuliza tumelogwa?waoga?wajinga?au .....................?