Hivi Siku Hizi Shule Hazifundishi Punctuation na Singular/Plural

Ruge Opinion

JF-Expert Member
Mar 22, 2006
1,838
701
Nimekuwa na kazi ya kusoma ripoti mbali mbali zilizoandikwa katika lugha ya Kiingereza. Kuna mambo mawili ambayo nimeyaona katika ripoti nyingi. La kwanza ni kutotumia alama za vituo kama coma, colons, semi-colons,nk. Mtu anaandika paragraph yenye mistari zaidi ya kumi lakini hakuna kituo hata kimoja. Baadhi hata full stop za mwisho wa sentensi hawaweki.

La pili ni kutojua kutumia umoja na wingi (singular and plural). Unakutana na vitu kama many house, 500 student, monies, we are implementing eight project, nk. Baadhi ya hizi ripoti zimeandikwa na watu wazito kwenye wizara za serikali na taasisi zingine.

Swali langu ni je, mambo ya punctuation na umoja na wingi siku hizi havifundishwi shuleni?
 
Nimewahi kukutana na lecturer check bob mmoja chuo kikuu kimoja hapa nchini akawa anatuambia kwamba kwenye mtihani andika as much as you can, point atatafuta mwenyewe humo! Sasa kwa mtindo huo unadhani kuna mtu atakaye angalia punctuation wakati vijana wanataka kufaulu tu!
 
watangazaji wetu clouds wanaita "hii nyimbo" ni kali instead of wimbo!!
 
Back
Top Bottom