kaburunye
JF-Expert Member
- May 12, 2010
- 672
- 74
Wadau, ningependa nijue huyu bwana mdogo ("First brother") wa TZ huwa anaongea nini huko anakozunguka akipiga siasa. Maana najua huyu dogo hana point kabisa, nataka yeyote anayejua ambayo huwa yanajiri kwenye ziara zake atumwagie hapa jamvini. Maana anayofanya "First lady" tumeyasikia na utumbo wake na nadhani ni muhimu tujue pia huyu dogo huko anaongea utumbo upi. Nasikia huwa ana demand reports kutoka kwa viongozi wa serikali na cha ajabu nao huwa wanampa. Hivi hatuna viongozi wenye akili timamu ambayo wanaweza kuukataa upuuzi huu hata ikibidi kunyang'anywa cheo???