GHIBUU
JF-Expert Member
- Jan 13, 2011
- 4,432
- 3,006
- Thread starter
- #1
Kwa Wazanzibar walio wengi leo hii ni kuona kwamba Zanzibar kama Nchi inajitawala wenyewe huku ikiongoza tawala zake kama vile historia ya kweli unavyotufahamisha, jinsi ya utawala halali wa kIzanzibar kabla ya kuja mapinduzi ambayo yamepelekea athari kubwa miongoni mwa Jamii ya Wazanzibar hadi leo hii.
Huu sio wakati wa malumbano kwa Wazanzibar kwani siku zote mwenye macho haambiwii tazama wala mwenye masikio yake hahitaji kuhimizwa kusikia.Hii ndio nafasi pekee kwa Wazanzibar kushikamana na kuondoa tofauti zao kwani kinyume chake ni kuipoteza Zanzibar na vizazi vyake ambavyo hadi hivi leo vinahangaika bila kujua hatma yao.
Wakati umefika kwa Wazanzibar kuchukua hatua zinazohitajika ili kuionesha dunia kwamba na sisi Wazanzibar sio wanyama ni binaadam ambao haki zetu za msingi lazima ziheshimiwe. Mifano mingi tumeiona leo hii imetokea Duniani na mpaka sasa Wanaukombozi bado hawajarudi nyuma, wapo na wanaendelea kudai haki zao, licha ya damu inayoendelea kumwagika, lakini leo lao ni ukombozi kwa kile wanachokiamini.
Hatuna budi kuvishukuru vyama vya upinzani Zanzibar kwa kutoa muamsho na taswiira inayoonesha kwamba Wazanzibar wameporwa kile ambacho kilikuwa chao, wametoa msaada mkubwa hili hatuwezi kulikataa.
Wakati umefika kwa Wazanzibar kuachana na mawazo mapotofu kwa kusema kwamba tunategemea chama fulani ili kituletee maendeleo na ukombozi, au fulani ndie pekee atatuokoa, tuelewe kwamba na huyu fulani ni binaadam na yeye pia anahitaji tumsaidie kufikia lengo lake, tusilaumu tu kwani ukombozi wa Nchi si wake peke yake bali ni jukumu la kila Mzanzibar awe ndani au nje ya nchi mchango wake unahitajika na taifa.
Huu sio wakati tena wa kufikiria hayo, kwani kila kitu kina wakati wake, la msingi hivi ni kukaa chini kama Wazanzibar bila kujali huyu ni chama gani na anatoka wapi, bali uzanzibar uwe ndio mwega wa kulalia ukombozi wa mhimili wa nchi yetu kijikomboa kwa Madhalim na maadui zetu.
Ikiwa Wazanzibar tutakaa kimya kwa kufikiria kusubiri rasimu ya katiba au vyenginevyo, hilo nikusema kwamba Zanzibar imeshapotea na haitorudi tena kwenye mikono ya Wazanzibar abadan.
Njama za kuihujumu Zanzibar haikuanza jana wala leo, kwa wale wenye kujua na kufuatilia historia wataungana na mimi , kwamba tokea enzi za Mababu na Mabibi zetu mbinu na hila zilitumika kuiangamiza visiwa hivi mashughuri vya Zanzibar. Kwa vile Wazanzibar waliongozwa na dini yao pamoja na ukarimu wao hayo ndio yakawa chachu kwa Wazanzibar kutawaliwa hadi leo hii. Sasa basi mwiba unapoingia ndio unapotolewa wakati umefika kwa Wazanzibar kutumia dini yao kuikomboa nchi yetu.
Mimi nahisi kwamba kwa sisi vijana wa Kizanzibar ingelikuwa ni vyema kama tungekuwa tunapigania Nchi yetu na kuuwawa kwa hilo kuliko kufa kwa madawa ya kulevya, kwani pindipo Zanzibar ikijikomboa basi ni kusema matunda yake yatakuwa kwa umma wote wa Kizanzibar.
Nataka niweke wazi kwamba na iwe iwavyo na tufanye kila linalowezekena, Zanzibar haiwezi kupatikana kwa njia ya kidemokrasia abadani. Sina haja ya kulizungumzia hili kwani kila Mzanzibar anajua ni kitu gani kinachoendelea Zanzibar tokea kuasisiwa kwa vyama vingi.
Watanganyika wako tayari kupigana vita ikibidi iwe hivyo ili kuhakikisha kwamba Zanzibar siku zote inakuwa katika miliki yake na hilo ndilo lengo la Watanganyika. Mbinu nyingi zinatumika ili kuwaziba macho Wazanzibar bila wao wenyewe kujitambua kwamba hizo ni mbinu za Watanganyika kuendelea kuwatawala Wazanzibar. Watanganyika huwachukua mamluki wachache pale Zanzibar na kuwapa vyeo ili Wazanzibar waone hawa ni wenzetu, kumbe hatujui kwamba kile ni chambo tu kwani viongozi wale hawazimi wala hawawashi kule Tanganyika, wapo pale kutumiliwa kuingamiza Dola ya Kizanzibar tu.
Watanganyika wanatumia mbinu za kitoto kabisa kuidhibiti Zanzibar, kiasi ambacho ni aibu kwa Wazanzibar kutozitambua mbinu hizi. Iweje kila maamuzi makubwa ya Wazanzibar yafanywe na Watanganyika ? Hivi sisi Wazanzibar vichwa vyetu ni maji au ? Nasema wakati umefika kwa Vijana Wakizanzibar kuacha kupiga kelele ovyo bali tukae pamoja tuandae mbinu na mikakati ya kuikomboa Zanzibar yetu, kinyume chake itakuwa tunajidanganya wenyewe Watanganyika hawawezi kuitoa Zanzibar kwa bei yeyote isipokuwa kwa vita na mikakati maalum.
NB: Ni maoni yangu tu.
Huu sio wakati wa malumbano kwa Wazanzibar kwani siku zote mwenye macho haambiwii tazama wala mwenye masikio yake hahitaji kuhimizwa kusikia.Hii ndio nafasi pekee kwa Wazanzibar kushikamana na kuondoa tofauti zao kwani kinyume chake ni kuipoteza Zanzibar na vizazi vyake ambavyo hadi hivi leo vinahangaika bila kujua hatma yao.
Wakati umefika kwa Wazanzibar kuchukua hatua zinazohitajika ili kuionesha dunia kwamba na sisi Wazanzibar sio wanyama ni binaadam ambao haki zetu za msingi lazima ziheshimiwe. Mifano mingi tumeiona leo hii imetokea Duniani na mpaka sasa Wanaukombozi bado hawajarudi nyuma, wapo na wanaendelea kudai haki zao, licha ya damu inayoendelea kumwagika, lakini leo lao ni ukombozi kwa kile wanachokiamini.
Hatuna budi kuvishukuru vyama vya upinzani Zanzibar kwa kutoa muamsho na taswiira inayoonesha kwamba Wazanzibar wameporwa kile ambacho kilikuwa chao, wametoa msaada mkubwa hili hatuwezi kulikataa.
Wakati umefika kwa Wazanzibar kuachana na mawazo mapotofu kwa kusema kwamba tunategemea chama fulani ili kituletee maendeleo na ukombozi, au fulani ndie pekee atatuokoa, tuelewe kwamba na huyu fulani ni binaadam na yeye pia anahitaji tumsaidie kufikia lengo lake, tusilaumu tu kwani ukombozi wa Nchi si wake peke yake bali ni jukumu la kila Mzanzibar awe ndani au nje ya nchi mchango wake unahitajika na taifa.
Huu sio wakati tena wa kufikiria hayo, kwani kila kitu kina wakati wake, la msingi hivi ni kukaa chini kama Wazanzibar bila kujali huyu ni chama gani na anatoka wapi, bali uzanzibar uwe ndio mwega wa kulalia ukombozi wa mhimili wa nchi yetu kijikomboa kwa Madhalim na maadui zetu.
Ikiwa Wazanzibar tutakaa kimya kwa kufikiria kusubiri rasimu ya katiba au vyenginevyo, hilo nikusema kwamba Zanzibar imeshapotea na haitorudi tena kwenye mikono ya Wazanzibar abadan.
Njama za kuihujumu Zanzibar haikuanza jana wala leo, kwa wale wenye kujua na kufuatilia historia wataungana na mimi , kwamba tokea enzi za Mababu na Mabibi zetu mbinu na hila zilitumika kuiangamiza visiwa hivi mashughuri vya Zanzibar. Kwa vile Wazanzibar waliongozwa na dini yao pamoja na ukarimu wao hayo ndio yakawa chachu kwa Wazanzibar kutawaliwa hadi leo hii. Sasa basi mwiba unapoingia ndio unapotolewa wakati umefika kwa Wazanzibar kutumia dini yao kuikomboa nchi yetu.
Mimi nahisi kwamba kwa sisi vijana wa Kizanzibar ingelikuwa ni vyema kama tungekuwa tunapigania Nchi yetu na kuuwawa kwa hilo kuliko kufa kwa madawa ya kulevya, kwani pindipo Zanzibar ikijikomboa basi ni kusema matunda yake yatakuwa kwa umma wote wa Kizanzibar.
Nataka niweke wazi kwamba na iwe iwavyo na tufanye kila linalowezekena, Zanzibar haiwezi kupatikana kwa njia ya kidemokrasia abadani. Sina haja ya kulizungumzia hili kwani kila Mzanzibar anajua ni kitu gani kinachoendelea Zanzibar tokea kuasisiwa kwa vyama vingi.
Watanganyika wako tayari kupigana vita ikibidi iwe hivyo ili kuhakikisha kwamba Zanzibar siku zote inakuwa katika miliki yake na hilo ndilo lengo la Watanganyika. Mbinu nyingi zinatumika ili kuwaziba macho Wazanzibar bila wao wenyewe kujitambua kwamba hizo ni mbinu za Watanganyika kuendelea kuwatawala Wazanzibar. Watanganyika huwachukua mamluki wachache pale Zanzibar na kuwapa vyeo ili Wazanzibar waone hawa ni wenzetu, kumbe hatujui kwamba kile ni chambo tu kwani viongozi wale hawazimi wala hawawashi kule Tanganyika, wapo pale kutumiliwa kuingamiza Dola ya Kizanzibar tu.
Watanganyika wanatumia mbinu za kitoto kabisa kuidhibiti Zanzibar, kiasi ambacho ni aibu kwa Wazanzibar kutozitambua mbinu hizi. Iweje kila maamuzi makubwa ya Wazanzibar yafanywe na Watanganyika ? Hivi sisi Wazanzibar vichwa vyetu ni maji au ? Nasema wakati umefika kwa Vijana Wakizanzibar kuacha kupiga kelele ovyo bali tukae pamoja tuandae mbinu na mikakati ya kuikomboa Zanzibar yetu, kinyume chake itakuwa tunajidanganya wenyewe Watanganyika hawawezi kuitoa Zanzibar kwa bei yeyote isipokuwa kwa vita na mikakati maalum.
NB: Ni maoni yangu tu.