Sajenti
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 3,651
- 412
Ni muda mrefu sasa kumekuwa na manung'uniko kutoka kwa watu mbali mbali hapa nchini na hata hivi karibuni wanasiasa waandamizi walidiriki kusema wazi kuwa uongozi wa raisi kikwete umekuwa goi goi. Mengi yamezungumzwa na yanaendelea kuzungumzwa. Kwa upande wangu naumia roho kuwa mwaka 2005 wakati wa uchaguzi mkuu nilitumia takribani saa 2 kukaa kwenye foleni kusubiri kupiga kura. Na nakiri nilimpa kura yangu JK kwa matumaini kuwa nachangua kiongozi anayejua shida zetu watanzania na hivyo anaweza kuyatafutia ufumbuzi matatizo yetu. Kwa mtazamo wangu mimi na watanzania wenzangu wengi tulikosea kumpa kura ya ndio JK!
Napata picha kuwa umefika wakati nchi inakosa kilanja wa kusimama na kukemea uvundo unaondelea. Ufisadi mwigi uliotokea na unaondelea kutokea huenda ukatufikisha mahali Tanzania ikawa shamba la bibi kila mtu anajichukulia awezavyo bila shaka yoyote.
Naelewa wazi humu ndani ya JF kuna watu watakaokuwa tayari kuanza malumbano yasiokuwa ya lazima ili mradi kutetea uozo wa serikali hii ya awamu ya 4. Nilifurahi sana niliposikia kuwa polisi walipiga marufuku maandamano yaliyopangwa kufanyika Dar eti kumpongeza JK na serikali yake na pia kuwashutumu wale waliomsema JK na serikali yake kwa utendaji mbovu. Huu unafiki wetu watanzania ndio hutuletea vilio na kusaga meno kila wakati. Naomba niseme wazi kuwa endapo nitakuwa hai mwezi Oktoba 2010 wakati wa uchaguzi JK hatopata kura yangu. Mtadai kuwa hata nisipompa kura mimi wengine watampa, lakini nina imani na mwenyezi mungu analiona hili kuwa wengi wataamka usingizini na kuwakomboa watu na hili jinamizi lililoikumba nchi yetu.Kuna watakaokwazika na hiki nilichoandika lakini ndio ukweli wenyewe.Ujinga wakati wa kwenda sio kurudi!!
Napata picha kuwa umefika wakati nchi inakosa kilanja wa kusimama na kukemea uvundo unaondelea. Ufisadi mwigi uliotokea na unaondelea kutokea huenda ukatufikisha mahali Tanzania ikawa shamba la bibi kila mtu anajichukulia awezavyo bila shaka yoyote.
Naelewa wazi humu ndani ya JF kuna watu watakaokuwa tayari kuanza malumbano yasiokuwa ya lazima ili mradi kutetea uozo wa serikali hii ya awamu ya 4. Nilifurahi sana niliposikia kuwa polisi walipiga marufuku maandamano yaliyopangwa kufanyika Dar eti kumpongeza JK na serikali yake na pia kuwashutumu wale waliomsema JK na serikali yake kwa utendaji mbovu. Huu unafiki wetu watanzania ndio hutuletea vilio na kusaga meno kila wakati. Naomba niseme wazi kuwa endapo nitakuwa hai mwezi Oktoba 2010 wakati wa uchaguzi JK hatopata kura yangu. Mtadai kuwa hata nisipompa kura mimi wengine watampa, lakini nina imani na mwenyezi mungu analiona hili kuwa wengi wataamka usingizini na kuwakomboa watu na hili jinamizi lililoikumba nchi yetu.Kuna watakaokwazika na hiki nilichoandika lakini ndio ukweli wenyewe.Ujinga wakati wa kwenda sio kurudi!!