Hivi ni kweli Jecha hajui sheria/ Katiba inasema nini Juu ya uchaguzi!??

Kaudunde Kautwange

JF-Expert Member
Nov 15, 2011
1,600
1,567
Habari wana Jukwaa...

Kwanza kabisa naomba mods msiuhamishe huu uzi.. Maana najua hapa nitapata wakunielewesha wengi zaidi.

Jana wakati naangalia taarifa ya habari ya ITV, baada ya habari za kitaifa, kuna kile kipindi cha mahojiano ya mda mfupi na mwalikwa yeyote, kuzungumzia suala lolote kwa jinsi atakavyo halikwa.

Sasa jana alikuwa mwanasheria moja nadhani anaitwa Awadhi Ali kama sijakoaea.

Na suala la kujadili lilikuwa juu ya uchaguzi wa marudi wa Zanzibar. Jecha Juzi kama sio jana alisikika kwenye vyombo vya habari akisema ya kwamba hakuna hata mgombea mmoja amekidhi vigezo vya kujitoa.

Kilichonishangaza, ni huyu bwana Awadhi kupinga wazi wazi tena akitumia vifungy vya sheria kwamba hakuna mahali popote kwenye katiba kumetolewa muongozi juu ya uchaguzi wa marudio wa jinsi ya Zanzibar, tena akaenda mbali kwa kusema hakuna kifungu chochote cha sheria kinaruhusu kuhairishwa kwa uchaguzi kama ilivyo situation ya Zanzibar.

Maswali
1. Je, ni kweli Jecha hajui sheria ya uchaguzi, yaani hazijui situation za kupelekea uchaguzi uhairishwe!?

2. Jecha ametumia sheria gani au kifungu gani cha katiba juu ya uchaguzi wa marudio kuwa wale wagombea hwajatimiza vigezo vya kujitoa, na hivyo vigezo ni vipi!?

Mnaojua haya mambo naomba msaada jamani.

Ahsante
 
Back
Top Bottom