Brooklyn
JF-Expert Member
- Mar 17, 2009
- 1,459
- 284
Wana JF habari za ujenzi wa Taifa?
Mimi ni mtumiaji mzuri sana wa asali ya kutoka mkoa wa Tabora. Jana nilienda kuchukua mzigo wangu (asali) katika ofisi moja inayojihusisha na kusafirisha mizigo. Nilipokuwa nikitoka kuelekea parking kwa bahati mbaya au nzuri nikawa nimeongozana na jamaa mmoja ambaye naye alitokea kwenye hiyo hiyo ofisi nilitokea mimi.
Akaniomba samahani kuna neno anataka kuniambia, nikamwambia bila shaka anaweza kunieleza. Akasema alinisikia nikitamka pale ofisini kuwa nimeenda kuchukukua asali na angependa kwa roho safi kunitahadhalisha juu ya matumizi ya asali kutoka mkoa wa Tabora. Akaniambia asali ya kutoka mkoa wa Tabora sio nzuri kiafya kwa sababu ina kiwango kikubwa sana cha nicotine kinachosababishwa na mazingira ya uzarishaji wa asali yenyewe. Nyuki wanapotengeneza asali huwa wanakuwa tayari wamefyonza chemicali za nicotine kwenye mimea ya tumbaku.
Mwishoni akamalizia kwa kusema kuwa ndio maana nyuki kutoka mkoa wa Tabora wamepigwa marufuku kuuzwa/kusafirishwa nje ya nchi.
Sasa nauliza kwa wadau werevu kwenye hili eneo je ni KWELI asali ya Tabora haifai kwa matumizi ya binadamu?
Kama hivyo ndivyo, serikali na mamlaka zinazohusika mbona zimekaa kimya bila kuwaelimisha wananchi jii ya hatari hii.
Angalau wangefanya kwenye pakiti za sigara, wawalazimishe wafanyabiashara waweke angalizo (disclaimer).
Mimi ni mtumiaji mzuri sana wa asali ya kutoka mkoa wa Tabora. Jana nilienda kuchukua mzigo wangu (asali) katika ofisi moja inayojihusisha na kusafirisha mizigo. Nilipokuwa nikitoka kuelekea parking kwa bahati mbaya au nzuri nikawa nimeongozana na jamaa mmoja ambaye naye alitokea kwenye hiyo hiyo ofisi nilitokea mimi.
Akaniomba samahani kuna neno anataka kuniambia, nikamwambia bila shaka anaweza kunieleza. Akasema alinisikia nikitamka pale ofisini kuwa nimeenda kuchukukua asali na angependa kwa roho safi kunitahadhalisha juu ya matumizi ya asali kutoka mkoa wa Tabora. Akaniambia asali ya kutoka mkoa wa Tabora sio nzuri kiafya kwa sababu ina kiwango kikubwa sana cha nicotine kinachosababishwa na mazingira ya uzarishaji wa asali yenyewe. Nyuki wanapotengeneza asali huwa wanakuwa tayari wamefyonza chemicali za nicotine kwenye mimea ya tumbaku.
Mwishoni akamalizia kwa kusema kuwa ndio maana nyuki kutoka mkoa wa Tabora wamepigwa marufuku kuuzwa/kusafirishwa nje ya nchi.
Sasa nauliza kwa wadau werevu kwenye hili eneo je ni KWELI asali ya Tabora haifai kwa matumizi ya binadamu?
Kama hivyo ndivyo, serikali na mamlaka zinazohusika mbona zimekaa kimya bila kuwaelimisha wananchi jii ya hatari hii.
Angalau wangefanya kwenye pakiti za sigara, wawalazimishe wafanyabiashara waweke angalizo (disclaimer).