Hivi ni Kwanini Marekani Hawaulizi Vyeti ?

Huulizwi vyeti au chochote kwa sababu wao wanajali "uungwana wako" na ni "watekelezaji wa sheria".
Unaweza usiulizwe vyeti na kazi ukapewa. Unaweza kusafiri kwenye usafiri wa umma usiulizwe tiketi.
Unaweza kudanganya chochote ukajiona wewe mjanja lakini....Siku wakikukamata, hakuna msalie mtume.

Mfano, ikiwa imeandikwa "Kupanda basi bila tiketi faini ni dola 10,000 au kifungo cha miaka 3, siku wakikukamata hakuna wa kumpa rushwa wala mjomba atakayekutetea.

Kweli Marekani inatumia sana uungwana lakini wanakua very selective maana hawatumii ungwana huo huko kwenye criminal backround, Drug test etc kuna vitu vingi tuu vingine visipokaa sawa hupati kazi

Ingekuwa rahisi kama walavyotumiama makampuni kwenye drug test na Criminnal wangeweza kutumia makampuni ya verify vyeti , wangeweza hata kusema leta copy wakae nazo ili kama wakija kukugundua wana kesi nzuri ya kugushi , lakini unaandika tuu Education:Master's Degree in Computer Science

Kazi ukiomba kwenye academic institution ndio wanauliza , maana huo ndio msingi wa kazi yenyewe au zile kazi zenye board exams ambazo unarenew baada ya muda fulani huko wanauliza board kama uko uptodate
 
unakuta mhasibu ana GPA ya 4.0 bank reconcilliation haiwez!unajiuliza hv kweli vyeti ni vya kwake au kanunua?bongo bwana!

kama mambo yote anaweza isipokuwa bank reconciliation, haimaanishi hawezi kuwa mhasibu mzuri.
unadhani ufaulu wa darasani uta reflect ufanisi wa huyo mtu katika ufanisi wake na utendaji wake wa kazi?
 
kama mambo yote anaweza isipokuwa bank reconciliation, haimaanishi hawezi kuwa mhasibu mzuri.
unadhani ufaulu wa darasani uta reflect ufanisi wa huyo mtu katika ufanisi wake na utendaji wake wa kazi?

Ndio maana USA wametupilia mbali mambo ya GPA , walishaona siku nyingi sio tija hiyo
 
hizo kasi niza kubeba mabox huko marekani,lakini kazi za maana lazima uonyeshe vyeti vyakooooo
 
Wewe niambie ni kazi gani ulionyesha vyeti, hayo mambo ya box ni watu tu bongo wanasema sio europe huku, watu wachache tuu wanapiga boxi marekani, kwahiyo umeneja wa IT au Forenstic expert sio kazi za maana na hawakawmbii ulete cheti chochote
 
Ni kweli usa taasisi zake hata bongo hawana haja na vyeti.nilikwenda interview mbili zote kwa kutumia cv tu na hawakuwahi kuomba copy au vyeti original.
 
Wewe niambie ni kazi gani ulionyesha vyeti, hayo mambo ya box ni watu tu bongo wanasema sio europe huku, watu wachache tuu wanapiga boxi marekani, kwahiyo umeneja wa IT au Forenstic expert sio kazi za maana na hawakawmbii ulete cheti chochote
mnaosha vyombo na kulea wazee sasa vyeti vya nini?
 
mnaosha vyombo na kulea wazee sasa vyeti vya nini?

Duu marafiki zako wote marekani ndio wanachofanya ? Ungekuja Diaspora Meetings za huku ndio ungejua watu wanafanya nini ? Hakuna kuosha vyombo wala nini
 
Duu marafiki zako wote marekani ndio wanachofanya ? Ungekuja Diaspora Meetings za huku ndio ungejua watu wanafanya nini ? Hakuna kuosha vyombo wala nini
sio kwa nia mbaya,lakini bora hata huko kuosha vyombo maana huku ukata mtupu.whtever your doing bro,keep it up for the best and mungu akutangulie kwa hilo.
 
Sio hivyo dada yangu , watu wengi sana marekani hawafanyi hizo kazi ni uongo sana , watu wakiwa shule ndio wanazifanya kujipatia kipato , but mimi na watanzania wengi tuu hatujawahi kufanya hizo kazi huo ndio ukweli na watu hawaulizwi vyeti huku na mimi nilishangaa sana maana niliajiriwa mpaka nikawa meneja wa IT kwa kuamini tuu nilichoandikka kwenye resume
 
Haha Mkuu Njiwa mimi hiyo GPA nimekuja kujua maana yake huku marekani mimi na elimu yangu ya kuunga si wangenitimua zamani, bongo wanauliza na GPA ? Kazi kweli kweli



Nfanyie mchakato basi mkuu nije huko kupga kaz.
 
Nfanyie mchakato basi mkuu nije huko kupga kaz.

Ni PM tuu nitakuunga uwe na ujuzi tuu wa utalaamu fulani unaohitajika , usijali kama cheti kikiwa kina GPA ndogo maana sijui hata kubwa ni ngapi au huna cheti una professional experience yote sawa
 
Back
Top Bottom