Zion Daughter
JF-Expert Member
- Jul 9, 2009
- 8,921
- 4,236
Nimekuwa nikiwasikia wanaume wengi wakisema kuwa hawataki kuuziwa mbuzi kwenye gunia.Hapa ninaongelea waoaji na sio wababaishaji,Mtu anaweza kuwa amempenda mtu, ana nia ya kuoa na vigezo vingine vyote amekubali lakini bado atataka mpaka apewe unyumba.Nikichukulia mfano hapa Tanzania watu wengi wapo katika dini 2, wakristo na waislamu na zote zinakataza haya mambo ya kutest.Isitoshe zamani mababa zetu walikuwa wanasubiri mpaka siku ya ndoa ya kijadi itakapofanyika ndio wanaendelea.Na ndoa zao zilikuwa zinadumu na hakuna talaka za kumwaga kama siku hizi.
Mbaya zaidi kuna wengine wanatest mpaka wanapata HIV,Siku wanaenda kupima inakuwa to late.
Kwani wanaume hawawezi kusubiri mpaka siku ya ndoa? Na je haya mambo ya kutest ni sahihi au ndo wakati wake hasa ?
Mbaya zaidi kuna wengine wanatest mpaka wanapata HIV,Siku wanaenda kupima inakuwa to late.
Kwani wanaume hawawezi kusubiri mpaka siku ya ndoa? Na je haya mambo ya kutest ni sahihi au ndo wakati wake hasa ?