kaangwa
JF-Expert Member
- Jan 30, 2011
- 644
- 192
Ninawasalimu wanajamii forum wote mnaosoma na kujadili mambo muhimu sehemu hii
Nitangulie kuomba samahani huenda issue hii ilishajadiliwa humu lakini mimi kwa kiasi fulani bado ni mgeni,hivyo sijaiona lakini inanitatiza naomba kwa wenye ujuzi na ufahamu ktk nyanja hii wanielimishe.
Mimi ni mfanya kazi ninayekatwa kitu inaitwa(PAYE) na kwa mwaka nalipa si chini ya 3,600,000/= ,sijawahi kusikia mtu ananiulizia TIN,lakini ninapoenda kure-new,leseni ya gari ambapo fedha ninayolipa haifikii hata 50000/= baada ya miaka 3 au ninapolipia road licence ya gari kiasi cha 100000/= kwa mwaka nadaiwa TIN,hapo ndipo ninaposhindwa kuelewa kanuni inayotumika hapa.
Niliambiwa maana ya TIN ni ''tax payer identification number'' nilidhani ukishakuwa na hii number kila kodi unayolipa inaingizwa kwenye number hiyo,lakini nimekuta ninakokatwa fedha nyingi namba hii haitumiki,ninakolipa fedha kidogo inatumika,jambo hili linanichanganya.Mwenye utaalam na mambo haya naomba aniondolee ujinga huu.
Naomaba kuwakilisha
Nitangulie kuomba samahani huenda issue hii ilishajadiliwa humu lakini mimi kwa kiasi fulani bado ni mgeni,hivyo sijaiona lakini inanitatiza naomba kwa wenye ujuzi na ufahamu ktk nyanja hii wanielimishe.
Mimi ni mfanya kazi ninayekatwa kitu inaitwa(PAYE) na kwa mwaka nalipa si chini ya 3,600,000/= ,sijawahi kusikia mtu ananiulizia TIN,lakini ninapoenda kure-new,leseni ya gari ambapo fedha ninayolipa haifikii hata 50000/= baada ya miaka 3 au ninapolipia road licence ya gari kiasi cha 100000/= kwa mwaka nadaiwa TIN,hapo ndipo ninaposhindwa kuelewa kanuni inayotumika hapa.
Niliambiwa maana ya TIN ni ''tax payer identification number'' nilidhani ukishakuwa na hii number kila kodi unayolipa inaingizwa kwenye number hiyo,lakini nimekuta ninakokatwa fedha nyingi namba hii haitumiki,ninakolipa fedha kidogo inatumika,jambo hili linanichanganya.Mwenye utaalam na mambo haya naomba aniondolee ujinga huu.
Naomaba kuwakilisha