Katavi
Platinum Member
- Aug 31, 2009
- 41,983
- 12,701
Siku hizi imekuwa ni kawaida kwa watu wanaoenda kuwapongeza akina mama waliojifungua kutoa SIFA ambazo mimi naona ni KASHFA. Kwa mfano kama ni mtoto wa kiume eti wanasema "umetuletea jambazi" na kama wa kike "umetuletea changudoa, house girl...nk" Hata kama ni utani huu umezidi, inaweza kutokea kweli mtoto akawa hivyo. Hii tabia mimi siipendi, mbona zamani ilikuwa safi maneno ya umetuletea "mchumba, mkwe, mama, bibi dada, nk" yalitawala na yalikuwa mazuri.