Hivi ni kina nani wakiguswa nchi haitatawalika?

Gembe

JF-Expert Member
Sep 25, 2007
2,483
159
Ndugu wanajamii wenzangu,

Ni muda sasa kuna jambo ambalo limekuwa likinitatiza hasa pale ninaposikia maneno kama yule ni mkuu wa nchi anaweza kufanya lolote,usimcheze mtoto yule baba yake ni afisa wa usalama,ooh mzee wake ni Mwanajeshi.

Wanakijiji wenzangu wameendelea kutishwa na wamefikia hatu aya kuogopa sana hata kuikemea CCM eti kwamba ukisikiwa jina lako litapelekwa Usalama wa Taifa.Wabunge wetu wamekuwa wa kwanza kumponda Mkulu wa Nchi ila waklimuona hawamwambii ukweli khali halisi wanabaki kucheka cheka na kumsifia.


Maneno ya uoga na usiri ni maneno ambayo yamo miongoni mwa watanzania masikini ambao wamejaa wamehsakata tamaa sana na m,aisha yasiyo bora.

Baada ya kusema hayo naomba sasa nilerejee kwenye kichwa cha habri hapo juu.Kama mtakumbuka wakati tukikiomalia watu wa EPA wachukuliwe hatua Kuna kiongozi mmoja mwandamizi wa wa serikali alisema sula hili la kuwashitaki vigogo wa EPA (acha hawa dagaa) ni zito kama wakishtakiwa nchi itashindwa kutawalika.

Nilijiuliza sana na nimekuwa nikijiuliza ,Ni watu gani ambao wanaweza kuiibia nchi hii na baadaye kuja kujitokeza na kusema kama wakiguswa nchi haitatawalika?uwezo huo wanaupata wapi na nani anawapa?Kinachoniuma zaidi mimi ndiyo nachagua serikali ila kumbe kuna watu wanojipa uwezo wa kimungu sasa nimechoka.we need to change this.Yes We can

wanajambo forums,
Kuna watanzania Mafisadi ambao wanalipeka kubaya taifa hili na bado wapo hai wakitesa na kutudhihaki.Tumeamua kuwa wakimya sana toka kipindi cha RDC.Wameendelea kututusi,wamewaambia wake zao na watoto zao kuwa sisi watanzania ni wajinga waliwao.

47 year is Enough.Hii ni operesheni Ondoa Mafisadi na naombaianze leo hii hii.

wanajamiiforums,

Ningependa tuanze na hatua moja iliyo na nia njema kabisa kwa taifa letu,tuorodheshe majina ya watu wote ambo unadhani wanaweza wakafanya nchi hii isitawalike(wanavyofikiria wao).

Then mie nitayapaeleka majina haya kwa ajili ya kufanya dua maalum waadhibiwe na ikiwezekna unaweza kuchagua ni jambo gani liwapate sababu hawana huruma na tumechoka sana sababu serikali iemshindwa sababu inawogopa kw akuwa wan ubia na serikali yao.

Mie naomba tuanzea kuaandika jina moja hadi lingine na naomba kuweka kina la kwanza.Yes We can na tuanze mapambao haya leo hii hii bila kupoteza muda.

1.Mgonja
2.EL(added by waberoya)
 
2.Edward Lowassa

'' kumekuwa na tuhuma kuwa baadhi ya; jeshi la polisi, usalama wa taifa, wabunge wanamsikiliza yeye''
 
2.Edward Lowassa

'' kumekuwa na tuhuma kuwa baadhi ya; jeshi la polisi, usalama wa taifa, wabunge wanamsikiliza yeye''

Wanamsikiliza yeye kwasababu gani,unaweza kuniambia?
 
Bwana Gembe kuna orodha maarufu kwa jina la "List of shame", sina shaka unaifahamu, ni hapo tu pa luanzia, majina yapo fanya basi uwezalo.
 
Jitu Patel dagaa?
Masatu,

Jeetu Patel ni dagaa tu,Unadhania Kagoda ilichota Billioni 40.Una uhakika gani hizi zierudishwa wakti tuliambiwa zilienda kufanya kazi maalum??

Ukiangalia kwa undani huyu kaonewa tu,na hawa navyokiri waligoma kuruiusiha baada ya peza za kagoda kuacha kulipwa.Tusubiri waje watoe ushahidi.

We are about to know who own Kagoda and who took the money...Unreveal story of Kagoda will be publish here soon.

Wewe... hiyo miwani yako inafanya watu waogope!

nimeshavua miwani sana
 
Mkuu Gembe naongeza Bi Zakia Meghji...simwonei ila mama huyu nyendo zake zashinda wajuzi. List of shame ipo ila kuna hawa wanaoogopwa kwa mbwembwe zao... mtaani tunaita mate ya mbwa
Kuna mahali umesema wana JamboForums mkuu, naomba isomeke JamiiForums au ni nia ya dhati, I mean you mean it?
 
Bwana Gembe, mimi sitataja mtu ama watu, kwa uwazi na ukweli ambao ukiwagusa nchi haitawalika ni "WANANCI", ikifikia wakati wananchi wakazongwa na matatizo, wakati wengine wananeemeka. Wakakata tamaa hapo nchi haitatawalika.
 
Mimi nilifikiri una mkakati maalum wa kuwaadhibu mafisadi dua la kuku halimpati mwewe. What we can now is to use whatever means nescessary to economically liberate the country and not hockus pookus.
 
Bwana Gembe, mimi sitataja mtu ama watu, kwa uwazi na ukweli ambao ukiwagusa nchi haitawalika ni "WANANCI", ikifikia wakati wananchi wakazongwa na matatizo, wakati wengine wananeemeka. Wakakata tamaa hapo nchi haitatawalika.

naamini Mkuu Mfumwa alimaanisha WANANCHI. Na mimi namuunga mkono kwa sababu wao ndio wenye mandate ya kuwachagua watu ambao wataongoza utawala.
Lakini si tuliambiwa nchi yetu inaongozwa na Katiba, Sheria na Kanuni? Hili wazo la kwamba watu ndio wanaweza kuharibu utawala linakujaje?
 
naamini Mkuu Mfumwa alimaanisha WANANCHI. Na mimi namuunga mkono kwa sababu wao ndio wenye mandate ya kuwachagua watu ambao wataongoza utawala.
Lakini si tuliambiwa nchi yetu inaongozwa na Katiba, Sheria na Kanuni? Hili wazo la kwamba watu ndio wanaweza kuharibu utawala linakujaje?

Ni kweli Mkuu nilikuwa namaanisha WANANCHI. Kucheza na wananchi ni kama kuwasha moto karibu na pipa la Petrol.
 
Bwana Gembe, mimi sitataja mtu ama watu, kwa uwazi na ukweli ambao ukiwagusa nchi haitawalika ni "WANANCI", ikifikia wakati wananchi wakazongwa na matatizo, wakati wengine wananeemeka. Wakakata tamaa hapo nchi haitatawalika.

You can't be serious! Wananchi hawa hawa wa Tanzania? Au ulimaanisha nchi jirani?

Wabongo wametopea kwenye usingizi mzito wa limbwata (danganya toto toka CCM). Kwa miongo kadhaa sasa wadanganyika wapo kwenye lindi la umasikini na matatizo ya kila aina. Lakini CCM inawaimbia amani kama tunu bora kabisa ya maisha.

Watanzania wamekata tamaa toka siku nyingi sana. Ukishaona imani ya dini(imported religions) inashamiri, hata kwa shari, ujue kuna kukata tamaa ya kujipatia maendeleo hapa hapa duniani. Kilichobaki ni maisha bora peponi. Wakristu kwa waislamu hupigana vikumbo katika hili. Sipingi imani ya dini, ila hii ya kwetu (kushamiri) imevuka mpaka.

Imani ya kupata utajiri kwa kutumia viungo vya albino ni kielelezo kingine cha jamii iliyochanganyikiwa na kukata tamaa.

Watanzania, sio tu wameguswa, bali wameshikwa sehemu nyeti. Kimbembe kipo kwenye kujinasua.
 
You can't be serious! Wananchi hawa hawa wa Tanzania? Au ulimaanisha nchi jirani?

Wabongo wametopea kwenye usingizi mzito wa limbwata (danganya toto toka CCM). Kwa miongo kadhaa sasa wadanganyika wapo kwenye lindi la umasikini na matatizo ya kila aina. Lakini CCM inawaimbia amani kama tunu bora kabisa ya maisha.

Watanzania wamekata tamaa toka siku nyingi sana. Ukishaona imani ya dini(imported religions) inashamiri, hata kwa shari, ujue kuna kukata tamaa ya kujipatia maendeleo hapa hapa duniani. Kilichobaki ni maisha bora peponi. Wakristu kwa waislamu hupigana vikumbo katika hili. Sipingi imani ya dini, ila hii ya kwetu (kushamiri) imevuka mpaka.

Imani ya kupata utajiri kwa kutumia viungo vya albino ni kielelezo kingine cha jamii iliyochanganyikiwa na kukata tamaa.

Watanzania, sio tu wameguswa, bali wameshikwa sehemu nyeti. Kimbembe kipo kwenye kujinasua.

Wananchi hawa ambao ni watanzania waliokata tamaa?wasiojiweza wapendao maisha bora?,Waoga wasiopenda kusema ukweli pindi ukweli unapotakiwa.Nadahni uanweza ukaona jinsi wananchi tulio nao.

Mkuu Mpita Njia na Mfumwa,
Wakati Mamvi anstaafishwa kwa manufaa ya umma na bunge tukufu watu walimpokea kwa shangwe na vifijo wakimuita shujaa,wakimsifu kwa mapambio.Hawa ndiyo wannahci ambao unasema wanaweza wakafanya nhci isitawalike?

Kunma watu ambao tunaogopa hata kuwataja,sijui wameturoga na mimi huwa nashindwa kuelewa kwanini kila siku tunawapigia kelele mafisaid waondoke ila wakienda huko vijijini kwao wanonekana Mashujaa,wanasifiwa

Mhe. zitto naomba unisaidie kwa hili,Baada ya zoezi la operesheni Mwibara tuanze na Operesheni Kuwaburubu shebingwa watanzania waliolala


 
naamini Mkuu Mfumwa alimaanisha WANANCHI. Na mimi namuunga mkono kwa sababu wao ndio wenye mandate ya kuwachagua watu ambao wataongoza utawala.
Lakini si tuliambiwa nchi yetu inaongozwa na Katiba, Sheria na Kanuni? Hili wazo la kwamba watu ndio wanaweza kuharibu utawala linakujaje?

Kwa kweli hata mimi naunga mkono hili wananchi wakigushwa vibaya, nchi kutawala ni ngumu...watakuwa wakirusha mawe kila sehemu tumeona Mbeya wananchi kule walishikwa pabaya na ahadi hewa....
 
Back
Top Bottom