..nikiwa primary miaka ya 80+ nilikuwa natumia mifuko ya rambo kubebea daftari nakumbuka darasa la kwanza hadi tatu ukichelewa dawati ni lazima ukae kwenye jiwe maana yalikuwa manne tu darasani, leo hii imepita miaka 30 bado mambo ni yale yale. Je Tutafika?
Kweli kusikia ni tofauti na kuona.Hiyo picha ya wanafunzi ni ya kusikitisha sana.Kibaya zaidi watu wanatanua na mashangingi.
Hata Misri,Tunisia,Yemen,Libya na sasa Siria mitandao kama hii ilisaidia watu kujua hali halisi.
Sisi sio kisiwa na wahusika wajifunze kwa wenzao.
DU hivi zile ahadi za watawala wa CCM kwa miaka 30 hazijamaliza hata katatizo kadogo ka madawati hii ni aibu ,na misaada tunapewa kila siku kwa kugawa dhahabu zetu ,bora tungetengeneza madawati ya dhahabu
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.