Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,709
Tangu tukiwa na umri wa siku moja,tunataka kukubaliwa,kupokelewa na kulindwa.Haya ni kama mambo ya kimaumbile kwa mwanadamu.Unapogundua kuwa watu wote hawakupendi utababaika na kuchanganyikiwa na maisha kwako yanaweza kupoteza maana.Wengi tunafanya tunayofanya au kuacha kufanya katika kutafuta kupendwa.Kwahiyo kila mmoja wetu ana kiu kubwa ya kupendwa.(hapa nazungumzia kupenda kuliko zaidi ya ule wa ngono)Hapa ndipo linapochipuka tatizo kubwa linalofanya wengi kushindwa kujua kupenda ni nini.Hushindwa kwa sababu hakuna anaejali kupenda,karibu wote tunajali kupendwa,siyo kupenda.Kama nguvu zetu zote tumeziweka kwenye kupendwa,kupenda kunakuwa na nafasi gani kwetu?Ndiyo maana wengi hatujui kupenda,tunangoja kupendwa.Mume anasubiri mkewe ampende,mke nae anasubiri mume ampende!Ni kitu gani kinatokea?Kulalamika kusikoisha.Tumewekeza kwenye kupendwa ambako hakutuhusu.Jambo linalokuhusu ni kupenda,kwani wewe ndo unaamua upende ama la.Kupendwa ni jambo unalofanyiwa,halikuhusu.Yanini uhangaike na jambo lisilokuhusu?Unaposubiri na mbaya zaidi kudai kupendwa,unapoteza muda wako bure kwani unaemtaka akupende nae anataka jambo hilo kwako.Ni jambo ambalo huwezi kulipanga wala kulidhibiti kwa sababu linamhusu mtu mwingine.Inawezekana vp umlazimishe mtu mwingine akupende?Haiwezekani.Lakini tunafanya jambo lisilowezekana.Lakini unaweza kupend kwani ni jambo linalotoka kwako,fanya hivyo maisha yako yote.Mtu akikuambia hakupendi huna haja ya kupandwa presha,au kumnunia na kuwmuwekea bifu,halikuhusu hilo wewe toa upendo tu,hili ndo linalokuhusu!