Vin Diesel
JF-Expert Member
- Mar 1, 2011
- 9,088
- 6,368
mbona kazi unayo kaka.
Sioni kwa nini anune kwa wewe kumzuia kuchukua mkopo ofisini. Jaribu kuchunguza taratibu, I am trying to think outside the box. Inawezekana kuna libosi linamtaka na lina mapesa. Sasa anaogopa akionekana ana mapesa utamuuliza kayatoa wapi.
Kwa nini anang'ang'ania kuchukua mkopo kwa vitu ambavyo mnaweza kuvinunua bila hata kuchukua mkopo? Au huko ofisini kwao kuchukua mkopo ni fasheni?
Habarini wandugu,
Wife kaniambia anataka achukue mkopo kazini kwao kama 1.5mil nikamuuliza kwa ajili ya nini akaniambia nataka kuongeza baadhi ya vitu hapa ndani nikamwambia sawa lakini hiyo 1.5m mbona tunaweza kupata kwa mwezi 1 bila we kuchukua huo mkopo kazin?Nikamwabia tuweke bajeti ya pesa kwa ajili ya hivyo vitu unavyotaka then tutavinunua tu.Nikamwambia ipo siku tutajakwama na hapo ndo utachukua mkopo ila kwa sasa sababu hatuna shida ya haraka hivyo haina haja ya kuchukua huo mkopo japo huo mkopo hauna riba ila nikamwambia unaweza chukua leo hiyo 1.5m then baada ya mwezi ikatokea issue ambayo ni urgent inataka pesa tutafanyaje na kama kwa upande wangu mi nikiwa nimekwama kpesa?Kwa sababu mi sikuona umuhimu wa kuchukua hiyo pesa sana nikamwambia aache.Ghafla akabadilika akanza kununa huwa tunakula pamoja nikaona anatenga chakula kila mtu na sahani yake,usiku hataki hata nimsogelee.
Basi asubuhi nikamwambia isiwe tabu sababu mshahara ni wako fanya vile unataka sintokuuliza wala kukuambia chchote kuhusu mshahara wako.Ila toka juzi hatuko vizuri nikitoka kazin nikimsalimia anaitika kama hataki ki ukweli inanikera sana.
Na shida ni kwamba hii ndio tabia yake yaani mkitofautiana maneno kidigo atanuna hapo hadi mi nijifanye mjinga kumwambia mama acha kununa na ile na ile basi ndo uhusiano unarudi tena.Ila nataka nijaribu kuona trip hii nione mwisho utakuwaje coz najua anasubiria nimwambie mama acha kununa.
Naomba munishauri sasa nifayeje wanandoa wenzangu?
Inawezekana pia kaongwa (kachuna buzi) sasa anashindwa jinsi ya kuzileta homeMh,huyo kuna jamaa anamlisha huko na kahitaji hela ndo mbinu ya kuzipata hiyo!
Ukimruhusu tu utasikia anakwambia kaibiwa
Uwe makini kdg,huenda kuna 'jamaa' kamwahidi kumpa,so anatafuta baraka zako kiaina 'while hiding her head in the sand' usije shangaa mabadiliko ya ghafla.Mkubalie/mtege auchukue muuweke bank mtapata hiyo interest.Check hiyo salary slip km ina deductions,km vp umeliwa.
Bado unachuna baba eeh?weeh endelea tu kuchuna kwa ushauri wetu,afu ujue mwenzio ataanza kutafuta wa kucheka nao.Utakapoanza kulazwa njaa urudi hapa tukupe ushauri mpya!weeh mbona mkeo anajua unapenda makande na anakupikia,ukimbembeleza utapata hasara gani?karaha jipe mwenyewe,for whatever reason.Nimejaribu kumchunia hadi sasa nahisi kama vile naanza kumchukia
Ahahahaaah!! Hii ni rahisi kugundua si huwa kuna fomu za kujaza?Inawezekana pia kaongwa (kachuna buzi) sasa anashindwa jinsi ya kuzileta home
Kha mie mtu anayenuna simpendi sana kwa sababu anakuwa na kinyongo mno na huwezi kujua anawaza nini.
Jaribu kumchunia na wewe kutoombwa acha kununa uone kama ataweza kununa mwezi mzima anakutega tu huyo na anajua utambembeleza.
Pole mwaya
Bado unachuna baba eeh?weeh endelea tu kuchuna kwa ushauri wetu,afu ujue mwenzio ataanza kutafuta wa kucheka nao.Utakapoanza kulazwa njaa urudi hapa tukupe ushauri mpya!weeh mbona mkeo anajua unapenda makande na anakupikia,ukimbembeleza utapata hasara gani?karaha jipe mwenyewe,for whatever reason.
AD afanye nini? ampikie,yaani mke wangu akinuna nimpikie na kufuli nimfulie? gggrrrrrrrrrrrr natamani nikumeze AD!Oohh jamani
nimeipenda story
yako kweli..
THIS IS REALY LOVE
mmbeleze mama bwana
Rahaa kweli kama mwanaume wako
akiwa anakudekeza
Borea hata huyu
Anataka kubembelez wa
tu..mmmhhh ungempata
Yule mpaka BM ndo mtapatana..
Kesho rudi home
Mapema mpikie,weka
wine juu yA meza
A bunch of Rosess ,
Mishumaa mmmhhh..
Yes u do have teenager love..
Look after her..
Ps. .sijaolewa natarajia..
Samahani maana ulisema kwa walio olewa tu..