Nimeshangazwa sana na kauli ya naibu spika bwana Job Ndugai wakati wa kufunga bunge mchana tarehe 15/7/2011kutangaza kuwa kwa kuwa mtoa hoja wa kambi ya upinzani alipomaliza kutoa hoja hakuuliza wanaounga mkono hoja hivyo hoja yake imepotelea hewani. Mimi najua kwa kuwa bunge linatetea maslahi ya taifa na kwa kuwa hoja yake ilikuwa ni muhimu basi angewaambia aulize wanaounga mkono hoja maana hoja yennyewe ni kwa ajili ya kutetea maslahi ya watanzania na sio chadema kama anavyofikiria ndugai. Kwake yeye ndugai alifurahi Mnyika alivyosahau kusema wanaounga mkono hoja, ni kama alikuwa anategea asahau hilo jambo. Umeme ni jambo la muhimu na limekuwa kero kubwa hapa Tz hivyo kufanya mambo ya kutegeana (unamtega mwenzako asahu ili upande mwingine ufaidi) kwa swala la kitaifa ni ujinga. KUna kukosea na kama kiongozi alipaswa kumkumbusha. Sina imani na Bunge la Tz kwani ni la CCM zaidi na sio kwa manufaa ya watanzania.