Kwetu Iringa
JF-Expert Member
- Jul 4, 2011
- 355
- 88
Wana JF, nimekuwa katika mawazo mazito sana toka Dr. Mwakyembe aanze kushughulikia sakata la ATCL. Hili jambo limejadiliwa sana hapa jamvini. Wengine wakisema Mwakyembe kakosea wakati wengine waki-support. Hoja yangu iko tofauti na hili. Siko upande wowote wa mjadala huu.
Mara nyingi sana tumeshuhudia au kusikia Pinda akichelea kuchukua hatua juu viongozi waiopatikana na makosa kwa kisingizio kuwa anayepaswa kuwachukulia hatua za nidhamu ni Rais!!
Sasa Mbona Dr. ameweza kuwachukulia hatua hawa vigogo wa ATCL? Pinda, ambaye ni boss wa Dr, anashindwaje kuwachukulia hatua vigogo wa aina hii?
Je hii inathibitisha ile imani ya kuwa Pinda ni mwoga au dhaifu? Au hawa vigogo wa ATCL waliochukuliwa hatua za nidhamu na Dr ni tofauti na wale ambao Pinda anawaogopa?? Au Dr ni jasiri zaidi ya Pinda? Au ni nini?
Nawasilisha!
Mara nyingi sana tumeshuhudia au kusikia Pinda akichelea kuchukua hatua juu viongozi waiopatikana na makosa kwa kisingizio kuwa anayepaswa kuwachukulia hatua za nidhamu ni Rais!!
Sasa Mbona Dr. ameweza kuwachukulia hatua hawa vigogo wa ATCL? Pinda, ambaye ni boss wa Dr, anashindwaje kuwachukulia hatua vigogo wa aina hii?
Je hii inathibitisha ile imani ya kuwa Pinda ni mwoga au dhaifu? Au hawa vigogo wa ATCL waliochukuliwa hatua za nidhamu na Dr ni tofauti na wale ambao Pinda anawaogopa?? Au Dr ni jasiri zaidi ya Pinda? Au ni nini?
Nawasilisha!