Mtumishi Wetu
JF-Expert Member
- Oct 12, 2010
- 5,712
- 1,906
Wadau nimeona tujadili hili la serikali yetu kutumia mahakama zetu kama chaka la kuficha maovu yake!!! Tuliona swala la madaktari walipoanza tuu mgomo serikali ikakimbilia mahakamani kusitisha mgomo ikidai kuwa ni batili, limekuja swala la walimu wanasema swala liko mahakamani!! Sasa tuseme mahakama zetu ni dhaifu hazina sheria kali za kuweza kudhibiti watu kukimbilia mahakamani kuweka stop order??? Je ikiwa wakipeleka kesi wakashindwa adhabu zinazotolewa ni dhaifu kiasi hawaziogopi kama vile kutolewa amri ya kutaifisha na kuuza mali za serikali hadi walipe madai ya watu??? Nawasilisha!!!