Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Kulingana na sheria za uchaguzi aliyefungwa kwa zaidi ya mwaka mmoja hana sifa za kuwa mgombea.
Bw. Aden rage ambaye hivi sasa anagombea jimbo la Tabora Mjini na ambaye hivi karibuni amekuwa akijifananisha na mmiliki wa klabu ya A.C mIlan ambaye ni Waziri Mkuu wa Italia kutokana na Bw. Rage kuwa Mwenyekiti wa Klabu ya Simba alikwishafungwa miaka mitatu. Kosa la jinai alilotiwa nalo hatiani ni kwa kumwibia mwajiri wake FAT/TFF alipokuwa ni katibu mtendaji wa chama hicho. Alienda mahakama kuu kupinga adhabu hiyo lakini rufani yake ilitupwa. Alinufaika na msamaha wa raisi Mkapa lakini hilo halimaanishi adhabu ilikuwa imefutwa. Kwa kuelewa hilo alikataa rufani mahakama ya rufaa. Sijawahi kusikia mahakama ya rufaa kama ilikwisha kuisikiliza rufani yake na kumsafisha vinginevyo hana sifa ya kuwa mgombea na sijui NEC walimpitishaje. Au kisingizio chao ni kuwa hakuwekewa pingamizi na mtu yoyote?
Kama aliwahi kusafishwa nijulisheni. Vinginevyo hata akishinda watakaoshindwa naye wana sababu nzito ya kwenda mahakamani na sheria ikafuata mkondo wake.
Bw. Aden rage ambaye hivi sasa anagombea jimbo la Tabora Mjini na ambaye hivi karibuni amekuwa akijifananisha na mmiliki wa klabu ya A.C mIlan ambaye ni Waziri Mkuu wa Italia kutokana na Bw. Rage kuwa Mwenyekiti wa Klabu ya Simba alikwishafungwa miaka mitatu. Kosa la jinai alilotiwa nalo hatiani ni kwa kumwibia mwajiri wake FAT/TFF alipokuwa ni katibu mtendaji wa chama hicho. Alienda mahakama kuu kupinga adhabu hiyo lakini rufani yake ilitupwa. Alinufaika na msamaha wa raisi Mkapa lakini hilo halimaanishi adhabu ilikuwa imefutwa. Kwa kuelewa hilo alikataa rufani mahakama ya rufaa. Sijawahi kusikia mahakama ya rufaa kama ilikwisha kuisikiliza rufani yake na kumsafisha vinginevyo hana sifa ya kuwa mgombea na sijui NEC walimpitishaje. Au kisingizio chao ni kuwa hakuwekewa pingamizi na mtu yoyote?
Kama aliwahi kusafishwa nijulisheni. Vinginevyo hata akishinda watakaoshindwa naye wana sababu nzito ya kwenda mahakamani na sheria ikafuata mkondo wake.