Hivi Luhanjo,Jairo, Ngereja na Malima Wanasubiri nini kujiuzuru?

Rejao mawazo yako ni ya wengi maana zaidi ya 98% ya CCM hudhania hivi. Na tunashukuru Mungu kuwa haya mawazo yamefanya kazi kwa zaidi ya miongo miwili ili kulinda na kudumisha 'amani iliyopo' - amini usiamini!
Wanafuata ushauri waliopewa, nafikiri ulisikia kutoka kwa most of MPs kuwa wasijiuzulu, kujiuzulu siyo suluhu ya matatizo ambayo yalitokea. Tusubiri...soon something will happen!
 
Kuwajibika ni dhana pana sana. Tuwaachie wahisika wenyewe waamue, kama dhamira zao zitawatuma kufanya hivyo basi watafanya.
Tusubiri dhamira zao ziwatume! Nadhani uko sahihi. Taarifa za "kiintelijensia" zinadai Jairo alikuwa awe Katibu Mkuu Kiongozi baada ya Luhanjo kustaafu rasmi baadae mwaka huu. Wabaya wake wakainyaka hiyo. Wakajua kuna kale kamchezo ka siku nyingi pale Nishati. Wakampasia Mama Shelukindo. Naye akafanya kama Baloteli juzi. Yaliyobaki sasa yanaingia kwenye historia ijayo ya nchi yetu. Kujiuzulu hakupo kwa kuwa ulikuwa ni "utaratibu wa kawaida", uliozoeleka pale Nishati
 
Hapo ndipo ninapomkumbuka fisadi Mkapa, angekuwa ashamtangaza waziri mwingine, mnakutana ofisini ndio utajua kama umefukuzwa au umejiuzuru
 
Hapo ndipo ninapomkumbuka fisadi Mkapa, angekuwa ashamtangaza waziri mwingine, mnakutana ofisini ndio utajua kama umefukuzwa au umejiuzuru
Huyu alikuwa mgumu zaidi kuwabadili mawaziri wake. Sumaye kapiga miaka 10 kwenye Uwaziri Mkuu, JK alipiga miaka 10 mambo ya nje,...., Kitine aliachia ngazi mwenyewe, Mbilinyi alijiondoa mwenyewe....
 
Ni kweli Ngeleja anakula kuku na familia yake wakati hapa Mwanza familia moja yatima hawana raha ya maisha kutokana na misukosuko wanayopata kutoka kwa ngeleja na diwani wake wa ccm juu ya nyumba yao.Wao na pesa zao za ufisadi wanaona kuwa wana haki ya kuingilia uhuru wa watu.kama unataka laana na watoto wako endeleza unyama unaowafanyia hao yatima wa mungu kwani ss hv nyumba yao inaweza kuanguka wakati wowote kwani nusu imezungukwa na maji uliozuia yasiingie kwenye jengo lako kuharibu vifaa vya thamani vya hotel yako vilivyoshushwa juzi na semi trela 3 vikitoka china.Kijana unacheza na moto hao yatima ni waislam tangu enzi za mababu zao, kamwe hutaiweza hiyo vita wakiinuka

garbage!
 
Aliyewaweka amewaambia " msihofu vijana wacha wapige kelele hapa kazi moja hakuna kujiuzulu kwa pamoja mimi na nyie tuna weza.wapinzani hawawezi ndiyo maana wanapiga kelele" alisema
 
Rejao,Wabunge wengi walisema watuhumiwa wote wawajibike. Alafu usipotoshe kuhusu dhana ya uwajibikaji. Kiongozi wa kisiasa anavyowajibika si lazima kwamba ndio suluhu ya tatizo au yeye ndio chanzo cha matatizo yaliyotokea. Kujiuzuru ni njia mojawapo ya kuonyesha umma kwamba hufurahii na unachukua yaliyofanywa na watendaji walio chini yako.
we Tumbili, maoni yako fantastic lakini picha iyo uloweka wala haijakaa vizuri, inatudhalilisha wanaume, please think twice about it.
 
Kwangu binafsi nilijua ile siku ya jumamosi jioni wangekuwa wamemaliza mchakato wa kujiuzuru kwa jinsi walivyo ihujumu Tanzania. Lakini mpaka saa hivi kimya au ndio kanyaga twende Watanzania ni wepesi kulalama na kusahau
.......wajiuzulu nini! atakayewekwa ni afadhali ya wao, waendelee tu, watanzania si tutasahau tu, kwani tutakuwa tumeanza kusahau? subiri uone habari za gamba zitakavyovuma, uone nani atakumbuka ya Jairo! afu mjiulize pia side B hv ni kwa nini JK hakuwasaidia maswaiba wake hadi wanavuliwa nguo hadharani? kwa watu ambao amefanya nao kazi kwa muda mrefu kama Luhanjo na Jairo, wanaomfahamu ndani na nje, hili sio sahihi kwa upande wa pili, lakini hili linahitaji busara kuelewa.
 
we Tumbili, maoni yako fantastic lakini picha iyo uloweka wala haijakaa vizuri, inatudhalilisha wanaume, please think twice about it.

Hutaona akiachia ngazi kama alama ya uwajikaji. Wao wanafikiria kuwa mnawanyia wivu tu.
 
Hivi nanyi bado hamjazijua live na muvi za CCM?Na kwa kawaida Anne Kilango na Ole Sendeka ndo masterling wa muvi zao.Kikwete huzinunua na kuwagawia watz wazicheki na kuzifurahia na mmwisho wa siku hugundua ni maigizo.MAMBO YA WASANII HAYO.MTACHEKI PICHA
 
Kama system ingekuwa inafanya kazi sawasawa, polisi wangetakiwa kuwakamata na kuwafungulia mashtaka! Maana ushahidi wa kutosha upo, tena wakutolewa na taasisi ya kuaminika(bunge).
 
Ngeleja yuko Arusha kirandaranda..........................lengo lake ni kuhubiri wamasai waachane na mila potofu.....................akifikiri kwa kufanya hivyo tutasahau............kasheshe lake.....................
 
Mimi binafsi najiuliza kila kukicha what the hell this people are waiting for?kibaya zaidi mabosi wao wapo kimya hamna kitu nachukia kama dharau,hivi kwanini wanajeuri hivi na dharau,i wish i wish 2858,
 
Wanasubiri wapelekwe mahakamani, na ushahidi utolewe na mahakama iamue kama wana hatia au la.
Inaweza ikawa kwamba bi kiroboto amewambia, huo ulikuwa ni mchezo wa kuigiza wa bunge, walikuwa wanawatania tu, nyie ni wasafi sana tena wateule wa raisi.
Raisi amesema kaeni hakuna mtu wa kuwafanya chochote, kwanza hayo ni maneno ya uchochezi wa CDM, mkijiuzuru mtaondoa amani na utulivu wa nchi. endeleeni kuchapa kazi. Sisi tutafunika kesi yenu na kikao chetu cha chama. mi ndiyo dikteta.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom