Hivi Kwanini Lowassa anautaka Urais?

Gembe

JF-Expert Member
Sep 25, 2007
2,483
159
Heshima Mbele

Ni muda sijaanzisha Mada hapa ila kuna jambao ambalo limekuwa likinitatiza kwa muda sasa ila naamini nyie mnaweza kuwa mnajua?

Hivi kwanini Lowassa anautaka Urais? akichaguliwa atalisaidiaje Taifa? Je, Pesa hizi anazotumia kuweka watu wake kwenye Chama tawala atazirudishaje?

Nimeanza kuogopa sana na kama watanzania wakikubali kuzugwa tena 2015 na kuchagua viongozi ambao wana mvuto wa sura, mvuto wa kutawala bila kuangalia rekodi yao ya nyuma taifa litaenda kubaya sana.

Taifa linaoelekea kupata Gesi na Mafuta linahitaji viongozi makini ambao wataweza kulivusha taifa, kutuondoa kwenye lindi la umasikini na kujenga utawala bora.
 
Anaweka mfumo wa kulinda ufisad wke kwa watanzania huyu ni wakuogopwa hafai hta kidogo kupewa urais wa taifa hili huwez kua na amir jeshi mkuu aina ya Lowassa na nchi ikabaki salama 2mkatae EL&CCM YAO KWA MASLAH YA WATANZANIA WALIO WENGI LASIVYO HISTORIA ITA2HUKUMU
 
its called power...he's rich, he's got all the money in the world bt what he doesnt have is POWER and that's what he's after..IKULU that's what he's after and he would do all it takes to get there...its called AMBITION, DREAM plus he knows no one can really make a difference in terms of improving the lives of wabongo like he can especially within CCM.
 
Kwa uadilifu simuon LOWASSA WALA YOYOTE KUTOKA CCM WAKUINGIA IKULU 2015
 
Kwa kua ana vigezo vya kuiongoza nchi katika haki na kweli.Vile vile ni chaguo la Mungu kama alivyotabiriwa na Mtumishi wa mungu TB JUSHUA wa emmanuel Tv.
 
Lowassa na JK waliunda mtandao tangu 1995, mmoja akiwa rais mmoja atakuwa PM, Nyerere aliona mbali akawachinjia baharini hawa Boys 2 Men! 2005 wakaungana tena, safari hii wakakubaliana kuwa JK atawale term moja (2005-2010) halafu Lowassa atawale (2010-2015).....Lowassa akampigania kwa hali na mali alitumia utajiri wake ili JK ashinde.

Cha ajabu JK akanogewa na madaraka akataka atawale 2 terms ikabidi amtoe sadaka lowassa kwenye kashfa ya richmond ili yeye atawale.
 
Inatisha inaonekana anataka kwanza kulipiza kisasi na rafiki yake waliyeunda mtandao wa kumuingiza madarakani.

Haileti maana kusema kuwa alibadilisha maamuzi ya baraza la mawaziri kwa kupendekeza kupewa tenda ya utata Richmond. Atafanyaje bila ya ruhusa ya mwenyekiti wa baraza la mawaziri?

Na mrichmond mwenyewe ni swahiba mkubwa wa mzee wa ikulu,angalia hadi leo mapendekezo ya Bunge hayajatelekezwa na hayatatelekezwa na hawa viongozi wa hili bunge na serikali hii.

Kuhusu gesi watu walioweka mabilioni Uswisi zinahisiwa ni mikataba na makampuni ya kutafuta gesi,labda anataka kuja kulinda, othrewise haileti maana kutumia hela zote kwa kuutaka urais.

Hii ni matusi kwawatanzania kuona kwamba tunaweza kuja nunuliwa kama njugu ili mtu mwenye sifa za ufisadi aingie tena madarakani ili kwanza aje arudishe pesa zake alizotumia. Inawezekana kwenye chama chao kwa sababu rushwa na fedha ni kigezo cha kwanza, inatia aibu wasomi maintellectual ambao wangeweza kuwasaidia wananchi wanakimbilia kuingia kwenye chama hiki ili wapate madaraka watuibie.

Utawala bora my god, hakuna takukuru, Hosea aliitakasa Richmond hajawajibishwa na bado yupo akishuhudia rushwa kwenye chaguzi zao,hakuna ikulu na usalama wa taifa muulize Mwamboka, hakuna polisi kumbuka Iringa kijiji cha nyololo mpaka leo RPC yuko madarakani.

Bunge wasikilize spika na wenyeviti, mahakama naogopa wazee wa jumuia hadi leo hawajalipwa wanazungushwa, Idd Amin aliwalipa lakini nchi ya amani yenye viongozi wanaotarajiwa kupewa utakatatifu maji ya kuwashwa.

Kumbuka mahakama ya rufaa kesi ya katiba utafikiri kikao cha kamati kuu ya NEC ya CCM
 
sifa zipi?za kuipa tenda Richmondya magumashi badala ya kuiwezesha tanesco kwa kuipa mitambo ili wananchi tupate umeme rahisi,au tujuze labda atatoa hela kama anavyotoa kwa uchaguzi wa ccm?
 
Kuna watu humu wanakesha kumpamba lowasa,inafika mahala naona kama tunachanganyikiwa vile,hivi nchi hii tumekosa mtu miongoni mwa watu 40 milioni kutuvusha hapa?
 
heshima mbele

ni muda sijaanzisha mada hapa ila kuna jambao ambalo limekuwa likinitatiza kwa muda sasa ila naamini nyie mnaweza kuwa mnajua?

Hivi kwanini lowassa anautaka urais? Akichaguliwa atalisaidiaje taifa? Je, pesa hizi anazotumia kuweka watu wake kwenye chama tawala atazirudishaje?

Nimeanza kuogopa sana na kama watanzania wakikubali kuzugwa tena 2015 na kuchagua viongozi ambao wana mvuto wa sura, mvuto wa kutawala bila kuangalia rekodi yao ya nyuma taifa litaenda kubaya sana.

Taifa linaoelekea kupata gesi na mafuta linahitaji viongozi makini ambao wataweza kulivusha taifa, kutuondoa kwenye lindi la umasikini na kujenga utawala bora.



yaah
lipo la kujiuliza hapo..
 
Kwa kua ana vigezo vya kuiongoza nchi katika haki na kweli.Vile vile ni chaguo la Mungu kama alivyotabiriwa na Mtumishi wa mungu TB JUSHUA wa emmanuel Tv.

kigezo cha kwanza ni kipi?kuhonga wanachama wa magamba ili aweke watu wake?
pili Richmond ambayo imetusababishia kupanda kwa umeme?
tatu malipo ya mabilioni yanayodaiwa tanesco na kampuni ya mshikaji wao ambayoinabidi tuwalipewatanzania?
nne kwa sifa hizi kama kuna mtu unayemdhania ni mtumishi wa Mungu anamtabiria kuwa ni chagua la Munguhuyo umuepuke jua ni mtumishi wa shetani,kwani Mungu hawezi kusababisha watu wake wapate dhiki
 
Tena mpaka baadhi ya waliokuwa wapiga kelele za ufisadi now wanajikomba kwake! sasa nazidi kumuelewa Pengo na kauli yake kwa wapiga kelele za ufisadi.
 
Mh. Waziri mkuu mstaafu aka Fisadi EL: IWE ISIWE, LAZIME NIWE RAIS AJAYE WA TANZANIA (HATA KAMA ITABIDI WATANZANIA WOTE WAFE)
 
Time will tell. Lakini nina uhakika 2015, Watanganyika HATUDANGANYIKI tena. Anayefikiri Watanganyika wa 2010 ndio watakuwa wale wale wa 2015, basi atakuwa amejidanganya sana.
 
Mh. Waziri mkuu mstaafu aka Fisadi EL: IWE ISIWE, LAZIME NIWE RAIS AJAYE WA TANZANIA (HATA KAMA ITABIDI WATANZANIA WOTE WAFE)
hakustaafu bali alijiuzulu ....huyu anaweza yeye ndio alikuwa moja ya injini za mtandao....lakini kwa sasa nona kama afya yake imechoka hata akihutubia siku hizi hautubii kwa ukakamavu kama zamani
 
Lowassa anautaka tu urais kwa sababu anataka kuwa rais.
Suala la kulisaidia taifa si kipaumbele cha Lowassa.
Lowassa anataka urais inatosha.................
 
Back
Top Bottom