Hivi kwa nini serikali haina Legal Aid Centers?

Luali

Senior Member
Jan 1, 2013
101
11
Habari ya leo waungwana,

Tafadhali ningependa kujua hivi ni kwa nini serikali kama serikali isiwe na vituo maalum ambavyo vingesambazwa mpaka vijijini,vitongojini,mijini na hata baadhi ya mitaa ili wananchi wawe na nafasi kubwa ya kutoa malalamiko yao kisheria na hata hivyo italeta hamasa ya kuzuia vitendo vya unyanyasaji juu ya wananchi dhidi ya sheria na haki zao kwa maana tathmini zinaonyesha fika kwamba asilimia kubwa ya wananchi ni waoga kwa kuwa hawafahamu sheria ama haki zao kama wananchi hivyo kudhulumiwa ama kuburutwa kwa kutofahamu haki zao. Na pia, kwa kuwa wananchi wengi hawawezi kumlipa wakili ama kuwa na wakili maalum hasa katika familia za hali ya chini ama watu wenye kipato cha hali ya chini - vitendo vingi vya haki za binadamu vinafanyika ila wananchi hawajui waanzie wapi mfano wanajeshi,polisi wanapochukua sheria mkononi au kiongozi wa serikali kuishi kwenye mtaa ama eneo akitaka kuishi tofauti na misingi ya sheria ama katiba inavyomruhusu aishi kama raia mwengine wa kawaida, na asijipe madaraka pasina na katiba ama sheria zilizopangwa
 
Habari ya leo waungwana,

Tafadhali ningependa kujua hivi ni kwa nini serikali kama serikali isiwe na vituo maalum ambavyo vingesambazwa mpaka vijijini,vitongojini,mijini na hata baadhi ya mitaa ili wananchi wawe na nafasi kubwa ya kutoa malalamiko yao kisheria na hata hivyo italeta hamasa ya kuzuia vitendo vya unyanyasaji juu ya wananchi dhidi ya sheria na haki zao kwa maana tathmini zinaonyesha fika kwamba asilimia kubwa ya wananchi ni waoga kwa kuwa hawafahamu sheria ama haki zao kama wananchi hivyo kudhulumiwa ama kuburutwa kwa kutofahamu haki zao. Na pia, kwa kuwa wananchi wengi hawawezi kumlipa wakili ama kuwa na wakili maalum hasa katika familia za hali ya chini ama watu wenye kipato cha hali ya chini - vitendo vingi vya haki za binadamu vinafanyika ila wananchi hawajui waanzie wapi mfano wanajeshi,polisi wanapochukua sheria mkononi au kiongozi wa serikali kuishi kwenye mtaa ama eneo akitaka kuishi tofauti na misingi ya sheria ama katiba inavyomruhusu aishi kama raia mwengine wa kawaida, na asijipe madaraka pasina na katiba ama sheria zilizopangwa
hoja zako ni za msingi kaka lakini kwa kumbukumbu zangu zamani ilikuwepo hii Legal Aid Center UDSM faculty of law mpaka sasa hivi ipo..sema inatoa ushauri tu wa kisheria sijasikia kama kuna mashauri yamefunguliwa mahakamani..so anaefahamu zaidi atakuja kutujuza...kuhusu swala la kudhulumiwa yapaswa uelewe kimsingi kwamba ingawa sheria wanadai inatenda haki unapaswa ujue haki ya nani? ni matajiri coz in one way or the other wao ndo wanainfluence sheria zitungwe ili waprotect interests zao mf mali etc..so sheria inafanya kazi in favour of them..kuhusu vijijini ndo hivyo sasa utaratibu ndo huo huo wa unyonyaji..kiaina halafu...unapaswa kujua kwamba kufungua kesi mahakamani, sio bure so kuna gharama..filing costs, litigations etc...so nani anaewza kudumu? ni tajiri so tajiri yule yule ndo anaeweza pata haki zake na hakuna wakili anaeweza fanya kitu bure hata wewe mwenyewe kumfanyia mtu kitu bure hua ngumu...ova...
 
hoja zako ni za msingi kaka lakini kwa kumbukumbu zangu zamani ilikuwepo hii Legal Aid Center UDSM faculty of law mpaka sasa hivi ipo..sema inatoa ushauri tu wa kisheria sijasikia kama kuna mashauri yamefunguliwa mahakamani..so anaefahamu zaidi atakuja kutujuza...kuhusu swala la kudhulumiwa yapaswa uelewe kimsingi kwamba ingawa sheria wanadai inatenda haki unapaswa ujue haki ya nani? ni matajiri coz in one way or the other wao ndo wanainfluence sheria zitungwe ili waprotect interests zao mf mali etc..so sheria inafanya kazi in favour of them..kuhusu vijijini ndo hivyo sasa utaratibu ndo huo huo wa unyonyaji..kiaina halafu...unapaswa kujua kwamba kufungua kesi mahakamani, sio bure so kuna gharama..filing costs, litigations etc...so nani anaewza kudumu? ni tajiri so tajiri yule yule ndo anaeweza pata haki zake na hakuna wakili anaeweza fanya kitu bure hata wewe mwenyewe kumfanyia mtu kitu bure hua ngumu...ova...

Ok, ila kama itakuwepo chuo kikuu nadhani itakuwa sana inaelemea kwa wanafunzi hasa na wafanyakazi wa chuo ila sidhani kama watakuwa wanahudumia raia kutoka nje ya chuo. Na hata hivyo nilimaanisha Legal Aid Centers zingekuwepo mikoani, na hata kwenye wilaya mbali mbali mpaka vijijini ili iwezekane kuwasaidia wananchi kuelewa haki zao na majukumu yao kama wananchi na kadhalika kwa kuwa mpaka sasa swala la mwananchi wa kawaida kujua haki zake zinazomzunguka mara nyingi huwa ni kitendawili kizito na ndio maana wananchi wamekuwa waoga na wananyanyasika kila leo kwenye nyanja mbali mbali za haki na maendeleo katika taifa lao wenyewe
 
Back
Top Bottom