Hivi kutumia lugha ya Kiingereza kwenye matamasha ya nyumbani maana yake nini?

Analytical

Senior Member
Mar 7, 2011
149
73
Nilikuwa naangalia kwenye Michuzi blog, wakati wa kuzindua Flaviana Matata Foundation, ambayo pamoja na watu wengine ilihudhuliwa na wabunge kama January Makamba na Zitto Kabwe. Mgeni rasmi akiwa mkurugenzi wa Utamaduni katika wizara ya Habari Profesa Mwansoko. Naona ilikuwa Kiingereza tu tokea mwanzo mpaka mwisho. Hii inaashiria nini? Au mantiki ya uzinduzi huo ilikuwa ni kwa ajili ya nani? Je labda Falaviana ndo alikuwa hajui kiswahili? au wageni waalikwa walikuwa hawajui kiswahili? Au ni nini? Sina uhakika kama kulikuwa na yeyote kati ya waliohudhuria hakuwa anajua kiswahili kwa maana ya kutoelewa kinachoendelea. Lakini hata kama ni hivyo mbona nchi zingine wanatumia lugha zao kwenye makongamano yao. Au kiingereza kwetu ni nini? Kama waandaaji wamo humu wanaweza kunifafanulia hii mantiki.
 
Ni inferiority complex tu ndio inawasumbua watz ktk hiyo tasnia.

Nenda ujerumani leo uongee kiingereza kama utaonekana mtu wa maana na tena kama ni matumbi ndio itakuwa worse kwa maana ya kupewa ushirikiano.

The worst party kwa waandaji wa such events huwa hawazingatii kabisa hadhira.
 
Nilikuwa naangalia kwenye Michuzi blog, wakati wa kuzindua Flaviana Matata Foundation, ambayo pamoja na watu wengine ilihudhuliwa na wabunge kama January Makamba na Zitto Kabwe. Mgeni rasmi akiwa mkurugenzi wa Utamaduni katika wizara ya Habari Profesa Mwansoko. Naona ilikuwa Kiingereza tu tokea mwanzo mpaka mwisho. Hii inaashiria nini? Au mantiki ya uzinduzi huo ilikuwa ni kwa ajili ya nani? Je labda Falaviana ndo alikuwa hajui kiswahili? au wageni waalikwa walikuwa hawajui kiswahili? Au ni nini? Sina uhakika kama kulikuwa na yeyote kati ya waliohudhuria hakuwa anajua kiswahili kwa maana ya kutoelewa kinachoendelea. Lakini hata kama ni hivyo mbona nchi zingine wanatumia lugha zao kwenye makongamano yao. Au kiingereza kwetu ni nini? Kama waandaaji wamo humu wanaweza kunifafanulia hii mantiki.
Upuuzi mtupu!!!! Mkamba alikuwa akigoogle speech za rais sasa hicho kiingereza kimetoka wapi siku Hizi!!! Nashangaa!
 
Hata mimi jambo hili linanikera sana. Utakuta kiongozi mwenye cheo kikubwa kabisa, anahutubia wananchi huku anachanganya kiswahili na kiingereza! Hili jambo halikuwepo miaka ya nyuma hasa enzi za Mwalimu, ambapo kuongea Kiswahili fanisi ilikuwa jambo la sifa. Lugha ya taifa ni Kiswahili na viongozi wanatakiwa wawe ni mfano mzuri katika kuendeleze na kukuza lugha yetu.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom