Hivi kuna tofauti gani tukiwa na baraza la mawaziri na lisipokuwapo?

Makame

JF-Expert Member
Jan 3, 2008
512
60
Nauliza hili kwa sababu zifuatazo:-

1. Baada ya Uchaguzi wa 2010, Mheshimiwa Rais alichukua muda mrefu kabla hajatangaza Baraza la Mawaziri; katika kipindi ambacho tulikuwa hatuna mawaziri, Nchi ilizama? Ilididimia? Iliganda? Mawaziri wanakula tu.

2. Kwa Mawaziri wanaotuhumiwa, walishawahi kukutana na kamati za bunge husika; wakaambiwa na hawakuchukua hatua kurekebisha dosari husika. Sasa kama Mawaziri wanaelezewa dosari kinaga ubaga, na hawajachukua hatua; kuna haja kweli ya kuwa nao????

3. Taarifa ya CAG kabla haijawasilishwa Bungeni ina mikondo yake inayopitia; na kama CAG amekuwa akiripoti kila mwaka; na Mawaziri wanayawacha mulemule ndani ya mjengo kama vile CAG alikwenda kuwatumbuiza; Mawaziri hawawajibiki, mpaka kelele zipigwe na wabunge; kweli kuna haja ya kuwa nao?

Wana JF, hizo ni fikra ; leteni mawazo yenu
 
..nchi bila baraza la mawaziri???katiba inataka liwepo so for the tym being ni lazima liwepo, wakati wa kutoa maoni kwenye tume ya mabadiliko ya katiba katoe hiyo hoja lakini huku ukiwa na mkakati mbadala utaowezesha kazi zilizokuwa zinafanywa na mawaziri zifanywe bila wao kuwepo..sio mbaya uka share nasi hapa unadhani badala ya cabinet pawe na nini???
 
Tuache kupotosha na kujenga hoja nyepesi baraza la mawaziri ni la muhimu sana.

Mapungufu ya mawaziri mmoja mmoja hayaondoi umuhimu wa baraza hilo.
 
Mawaziri ni muhimu kuwepo kwa sababu ya kutekeleza sera za chama kinachotawala. Cha maana ni mawaziri hao kuwa wachapakazi na waaminifu.
 
Tofauti ipo ila kwa baraza lilopita ni kama 50 kwa 50 ,sababu Kuna bahadhi ya mawaziri kazi zao zinaonekana waziwazi kuwa zina manufaa kwa jamii na kuna mawaziri wako kimaslahi zaidi ambao wasingekuwepo nadhani taifa lingeokoa pesa ambazo zimefisadiwa na hao mawaziri.







Nauliza hili kwa sababu zifuatazo:-

1. Baada ya Uchaguzi wa 2010, Mheshimiwa Rais alichukua muda mrefu kabla hajatangaza Baraza la Mawaziri; katika kipindi ambacho tulikuwa hatuna mawaziri, Nchi ilizama? Ilididimia? Iliganda? Mawaziri wanakula tu.

2. Kwa Mawaziri wanaotuhumiwa, walishawahi kukutana na kamati za bunge husika; wakaambiwa na hawakuchukua hatua kurekebisha dosari husika. Sasa kama Mawaziri wanaelezewa dosari kinaga ubaga, na hawajachukua hatua; kuna haja kweli ya kuwa nao????

3. Taarifa ya CAG kabla haijawasilishwa Bungeni ina mikondo yake inayopitia; na kama CAG amekuwa akiripoti kila mwaka; na Mawaziri wanayawacha mulemule ndani ya mjengo kama vile CAG alikwenda kuwatumbuiza; Mawaziri hawawajibiki, mpaka kelele zipigwe na wabunge; kweli kuna haja ya kuwa nao?

Wana JF, hizo ni fikra ; leteni mawazo yenu
 
Back
Top Bottom