Hivi kuna sababu gani za kupost/kuweka picha za watoto wetu mitandaoni?

sirjohn

JF-Expert Member
Aug 6, 2014
767
677
Hivi kuna sababu gani za kupost/kuweka picha za watoto wetu mitandaoni? utakuta wa kike kawekwa na maneno ya kumpamba kama
beautiful/cute/queen/mrembo wangu.

Wakiume: HB/ Prince /kidume changu

Mtoto anatakiwa kufunzwa kuanzia mdogo kabisa kuhusu faragha yake, nini cha kusema au kutoa na nini asiseme au asitoe. Hii ni pamoja na kwenye mitandao ya kijamii, simu na huduma nyingine za mawasiliano.

Umeshawahi kuona wanasiasa wanaweka picha za watoto wao au ndugu zao wa karibu kwenye mitandao hasa ya kijamii?Unajua ni kwanini?

Kwasababu kila anachofanya yeye kinamwathiri mtoto wake au watu wake wa karibu kwa ubaya au uzuri. Ni rahisi kuweka rehani faragha za watoto na ndugu zake.Kama ni mtoto wa kike anaweza kuanza kufuatiliwa na ‘mabazazi’ kwa sababu ya picha tu. Watatafuta anapoishi, shule anayosoma na usishangae siku moja akabakwa.

Kwa hisani ya mwananchi tunapata elimu kwanini hii tabia imezuka sana wanandoa siku hiyo hiyo mama anaugulia maumivu badala ya baba kumhangaikia mama na mwanae yeye anafuta kamera iko wapi tena siku hizi mchina amerahisisha anamfotoa mtoto na kupost kwenye wall yake ili iweje? kwamba watu wajue na wewe ni kudume cha mbegu au una kizazi?

Matokeo yake ndo wazazi mnapotofautiana na marafiki zenu mnawatukana mpaka watoto, kuna wengne sijui mtandao gani yule dada anauza pichu anamtukana mtoto wa mwenzaje eti baboon hivi mnahisi watoto wanajisikiaje? unamharibia mtoto future yake bila kujua, ukifikiri ni fahari kuweka picha ya mwanao sijui facebook, twitter, instagarma na kwingne huko ni ushamba na ujinga, labda siku hizi kwa kuwa imekuwa issue sana kupata mtoto!

Badilikeni!
 
Mkuu, tatizo la watu wengi kuwa 'vichwa maji', yani watu hawana content za kutosha alafu wanajilazimisha kupost vitu kwenye mitandao so unakuta anapost kitu icho hicho kila mara na vingine vinavuka mipaka. Wanachotakiwa kufanya ni kusoma sana vitabu mbali mbali na magazeti na kusikiliza habari ili kupanua ufahamu. There after unakuwa na vitu mbali mbali vya kupost kwenye mitandao ya kijamii.
 
somo zuri sana!!!! utasikia kama kaenda kununua shoes za mtot mliman city ili watu wajue kuwa kanunulia pale utaskia hapohapo anamfotoa akiwa kajaribu anarusha fb, inst, whtp n.K utaskia ma angle agrysh!! si ulimbuken huO jaman mbona hawapigag Na kupost wakiwa wamefilicka???
 
Mleta thread eti ni mzee sana wa age la 1925 huko ndiyo kazaliwa mleta thread! Hajui mambo ya Globalization tayari yalisha take place! sasa hvi ni kuji selfisha na 360 na kulirusha hewani!
 
Mkuu Athari Hasi Ya Kuweka Picha Ni Ipi? Coz Umeilezea Kwa Wanasiasa Tu Lakn Wapo Public Figure Wengi Kama Wanamusik Na Wengine Kama Hao.

Kwasisi Tusio Maarufu Nini Shida

ni ngumu kuelewa lakini kimantiki mtoto wako siyo wakuexpose kwa kila mtu! na kumsifia kwa uzuri wake! umakini na tabia za mtoto hutokana na maisha aliyoyaishi akiwa na wazazi wake! mpe mtoto vitu mhimu ktk maisha yake na siyo sifa za mitandaoni! kaa na mwanao mwambie ana kwa ana nataka uwe hivi na hivi hiii inamtosha kudraw atyention yake kwa yale unayomwbia.
 
ni ngumu kuelewa lakini kimantiki mtoto wako siyo wakuexpose kwa kila mtu! na kumsifia kwa uzuri wake! umakini na tabia za mtoto hutokana na maisha aliyoyaishi akiwa na wazazi wake! mpe mtoto vitu mhimu ktk maisha yake na siyo sifa za mitandaoni! kaa na mwanao mwambie ana kwa ana nataka uwe hivi na hivi hiii inamtosha kudraw atyention yake kwa yale unayomwbia.
Swa Mkuu Umesomeka Japo Inaonekana Hii Ishu Unaiangalia Kiimani Zaid
 
Mleta thread eti ni mzee sana wa age la 1925 huko ndiyo kazaliwa mleta thread! Hajui mambo ya Globalization tayari yalisha take place! sasa hvi ni kuji selfisha na 360 na kulirusha hewani!


mkuu unaweza kutoa maana ya globolization huku ukiwianisha na kupost picha za mwanao mitandaoni!


huuvujinga hufanywa na watu ambao ukikaa nao utakuta kichwani ni ()
 
Sidhani kama ni tatizo, kila mtu na uhuru wake, labda kama wewe umeliona tatizo hapo.
kubwa tu rafiki,
watoto sio haki kuwekwa humu. Je walitoa idhini? Uhuru usitumiwe vibaya. uhuru usiingilie mtu mwingine so si sawa. hata kidogo. msemeni huyo mtu mzima kwa alichoikifanya mkosoeni lakini with boundaries hasa watoto.
 
Kila jambo lifanywe kwa kiasi, privacy ni character muhimu kwa binadamu mwenye utashi kamili, family events kv birthday etc timely/rarely zinaweza wekwa online,mtoto hajafikia umri wa maamuzi huenda angekuwa mkubwa hata asingetaka hicho unachomfanyia AFA kumweka mitandaoni is concerned
 
Back
Top Bottom