Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Asubuhi ya saa 12.30, STAR TV, kila siku walikuwa wanarusha hewani kipindi cha someni magazeti lakini katika kipindi hiki cha uchaguzi wameingia mitini na sasa hivi ni vigumu kukukubali hoja za sababu zisizoweza kuzuilika ili tuafiki hili pazia nene la vichwa vya habari vya magazeti.
Ninahisi kuna mkono wa CCM baada ya kuona mambo ya ushindi wa asilimia themanini wa mwaka 2005 sasa yameyeyuka .Na Ikulu iko mashakani
Kama kuna mwanajamvi mwenye taarifa zaidi anijulishe ili nami nielimike vinginevyo basi nitabaki na hisia zangu ambazo yawezekana kabisa siyo sahihi