Amavubi
JF-Expert Member
- Dec 9, 2010
- 30,142
- 13,216
Najiuliza sana changamoto nyingi zinalolikumba Taifa kwa sasa, kuchelewa kwa mishahara ya watumishi, Halmashauri nyingi kukwama shughuli za Maendeleo, kupanda na kupandishwa kwa bei za vitu, bidhaa na huduma kwa njia ya LIFTI huku mishahara ikipanda kwa NGAZI, migomo ya watumishi wa kada mbalimbali, kutosikilizwa kwa kesi hususan za uchaguzi kutokana ukosefu wa fedha huku ikijulikana wazi kwamba kuchelewesha haki ni sawa na kuinyima na list goes on and on................mbaya zaidi najiuliza mantiki yake huku kwa sikio lingine nasikia majigambo ya onegezeko la makusanyo ya kodi kwa mwezi KWA ASILIMIA KAMA NYINGI HIVI.................naona pia Rais kasikia kilio cha wananchi na kupunguza safari za nje japo za misibani zimeongezeka zaidi.........sasaswali ninalojiuliza KODI ZINAKWENDA WAPI?????