Nsiande
JF-Expert Member
- Jul 27, 2009
- 1,649
- 872
Hahaha nimecheka sana na vituko vya utotoni, nakumbuka zamani sisi baba yetu alikuwa ni mtumishi wa serikali hivyo tulikuwa tunahamahama mikoa na hivyo tunahamishwa sana mashule
Mara nyingi mimi na ndugu zangu tukiitwa wageni maana shule moja humalizi hata mwaka, sasa bwana mimi mpenda vitabu nikiwa darasa la 3 Gangilonga Iringa, nikaazima kitabu kinaitwa 'dogodogo wanitesaaaa'
Kurudi home ilinichukua kama siku 3 kukisoma nikiwa nakificha na mto, salale baba akachungulia chumbani na kufunua mto na kunikuta ndio ninakimaliziamalizia...jamani nilichapwa! Mtoto wa miaka 8 unasoma dogodogo wanitesa....!! Mdingi akakichana kile kitabu
Kwenda shule nikawa nadaiwa mpaka ikabidi niache kwenda shule (nadaiwa na mtoto wa drs la 7 ), mama kugundua siendi shule ndio akanipeleka kwa mkuu wa shule na kulipia gharama za kitabu shs 40...
Kilichofuatia mkuu wa shule kwa ufisadi mzito hiyo hela hakumpa mdada anayenidai, akala kichapo na kuchimbwa biti juu kuwa asinidai tena!
Kwakweli mpaka leo kwa wiki nanunua wastani wa 2 storybooks, tht habit isn't easy to shake off..(Currently reading all 8 books of Alfu lela ulela )
Mhandisi
Mara nyingi mimi na ndugu zangu tukiitwa wageni maana shule moja humalizi hata mwaka, sasa bwana mimi mpenda vitabu nikiwa darasa la 3 Gangilonga Iringa, nikaazima kitabu kinaitwa 'dogodogo wanitesaaaa'
Kurudi home ilinichukua kama siku 3 kukisoma nikiwa nakificha na mto, salale baba akachungulia chumbani na kufunua mto na kunikuta ndio ninakimaliziamalizia...jamani nilichapwa! Mtoto wa miaka 8 unasoma dogodogo wanitesa....!! Mdingi akakichana kile kitabu
Kwenda shule nikawa nadaiwa mpaka ikabidi niache kwenda shule (nadaiwa na mtoto wa drs la 7 ), mama kugundua siendi shule ndio akanipeleka kwa mkuu wa shule na kulipia gharama za kitabu shs 40...
Kilichofuatia mkuu wa shule kwa ufisadi mzito hiyo hela hakumpa mdada anayenidai, akala kichapo na kuchimbwa biti juu kuwa asinidai tena!
Kwakweli mpaka leo kwa wiki nanunua wastani wa 2 storybooks, tht habit isn't easy to shake off..(Currently reading all 8 books of Alfu lela ulela )
Mhandisi