Hivi, jirani kwanini hununui gari?

Huyu jirani kauzu zaidi ya dagaa, na wewe una roho ngumu maana ningemwambia anishushe palepale wakati anatoa dhihaka hiyo.
 
Hivi una akili sawaswa ndugu? uheshimiwe kwa gari!! kweli!!?? Mmezaliwa kwenye familia gani nyinyi viumbe?

= Wote tukiwa matajiri nani atamuomba mwenzake?

Sometimes umiza kichwa usichukulie mambo kirahisi mkuu au shule ya kata?
 
hata kama ana gar na uwa ananipa lft ndo anidharirishe mshenz tu! Na siach kuomba lift akizidisha mambo tu naomba aniuzie hlo gar lake au anikope nkanunue.
 
Hongera kwa kuanza kujenga kwa sasa, hilo ndo muhimu mkuu..Gari utakuwa nalo tu isikutie presha..ila kiukweli huyo jirani hilo swali alilokuuliza ni tata sana ukizingatia yeye ndiye mtoa lifti..inabidi uanze kubanda basi kuanzia kesho, hata taxi mara kadhaa ukiwa na emergency au umechelewa job maana dodoma kamji kadogo ndyoko na siyo ghali vilee.
Haya karibu lunch tupo maeneo ya rose garden hapa dodoma..jioni mara nyingi lazima nipitie chako ni chako kwa kukuz!!

Nimekuelewa mada. Ila tabia gani tena hiyo ya kuteremshana udenda tena muda huu, madam! nomaaa! heri ungekaa kimya maana hiyo nyama ya hapo rg na hao kuku wa cnic, na jnaa ya mchana huu, umeniharibia mchana wangu, agrrrrrrrr!
 
Ndyoko...kama ni muda mrefu umekuwa ukipata lifti, kiiungwana zaidi ingebidi atleast unampa kahela everymonth, uone kama angekataa na hii ingeepusha na embarassment. Sasa wewe kila siku unapandishwa bure, huku wasave nauli ya daladala na unajua kama mafuta and other maintenance are damn expensive. Uso sometimes unaumbwa na haya, huyu jamaa aliamua kukutolea uvivu

Mimi naona jamaa hajakosa kukujulisha may be the tone was a bit rude, kawaida tunajisahau tukipata mteremko. Personally ningeiita lifti kama for few days only lakini kama ni kila siku somehow you deserve it.
 
mhh mhhh mhhh!! Wewe utakuwa ni vigiteriani, anyway kesho nitakualika masaki didi's pub kwa ajili ya lunch ya mishikaki ya samaki na chips. Sea food is good for u?
fish pia situmii nawashwa mwili pia sipendi harusi yake labda dagaa.mimi ni kuku tu
 
Ndyoko,
Kwanza nimeku-mrs sana!
Pili, kwani ukipewa lift huwa una tabia ya kupiga honi? Manake inawezekana unataka kupanga na route na kuweka kishoka kabisa. Pole, hiyo ni changamoto tu.
 
= Wote tukiwa matajiri nani atamuomba mwenzake?

Sometimes umiza kichwa usichukulie mambo kirahisi mkuu au shule ya kata?
Form 4 Graduate & am very proud of it! Hatukuwa na shule za kata wakati Nagraduate, ilikuwa ni enzi za Sheikh Ally Hassan Mwinyi
 
wapewa lift wanasahau kitu kimoja. siku moja moja mtoa lift anahitaji privacy yake. awe tu peke yake garini mwake awaze na kuwazua mambo yake au awe peke yake na spouse wake wazungumze ya kwao, waimbiane, wasemane nk. sasa ikiwa kila siku mtu wa lift yupo inageuka kutoka msaada kuwa kero kwa watoa lift
 
Mhh! hapa mwenye kukosa maarifa nadhani huyu mwomba lift!
kwanini iwe kila siku wakati daladala ziko kibao tu!

na si lazime upewe lift kama hakuna emergence bana!

kama gari si kipaumbele kwake, apande daladala!
namuunga sana mkono huyo jirani, kwanza ni kunyimana uhuru,
halafu, lijitu lingine utakuta limepanda halijaoga vizuri, hiyo mijasho yake sasa?
au ameoga vizuri lakini Mipafyumu utafikiri ndo kaogea mpaka kero!
au ni Mzito mpaka gari linaegemea upande (springs/shockabs zinaumia),
au kaingiza mchanga/tope! ukija kwenye garama za mafuta, services, spareparts,
kuosha ni mwenye gari, wakati watumiaje ni wengi!!
wabongo tuache kupenda "FREE LUNCH/RIDE"!

HIVI INGEKUAJE KAMA KILA SIKU JIONI JIRANI YAKO HUYO NAYE AANZE KATABIA
KA KUJA KUOMBA HIFADHI YA KULALA??????? AU hata kuomba tu mkaa wa
kuchochelea moto??
kama huwezi nunua yako, tumia wa umma au nenda kwa miguu bana!

Aisee kwa kweli ni dalili ya kushoshwa na kuomba kwako lift,
Lakini huyo nae anadhani gari ni kipaumbele kwa kila mmoja,
Naamini ni limbukeni wa magari maana hata kama angekupa lift mwaka mzima bado alitakiwa kujua kuwa kila kitu kinafanyika kwa mipango.

Kwa kifupi huyo bwana amekosa Busara na zaidi inawezekana hana maarifa.
Pole sana Mkuu.
 
wapewa lift wanasahau kitu kimoja. siku moja moja mtoa lift anahitaji privacy yake. awe tu peke yake garini mwake awaze na kuwazua mambo yake au awe peke yake na spouse wake wazungumze ya kwao, waimbiane, wasemane nk. sasa ikiwa kila siku mtu wa lift yupo inageuka kutoka msaada kuwa kero kwa watoa lift

Nami nilitaka kuandika hivi hivi umeniwahi, naona wote wanaona kuwa jamaa kamchoka tuu, wakati mnaopewa lift mkiwa mambo yenu ya binafsi mnachepuka tu je yeye akiwa na jambo la binafsi atafanyaje?. Lift iwe kama dharula si kama ndio utaratibu wa maisha, weka bajet yako ya usafiri ya mwezi na itumie. Imetokea dharula ndio unaomba lift, ukifanya hivyo wala hutapata taabu kabisa.
 
Basi mngekuwa mnamsaidia hata gharama za mafuta kidogo, sasa nyie kila siku mnapanda na anawaendesha tu. watz tusizoee sana vitu vya bure.
 
nonuaa hata bajaji?au acha kuomba ombaaa lift kama unaonaa aibu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom