Hivi jamani mambo haya tanapa hadi lini.......?

notorious big

Member
Jan 11, 2012
5
1
Hifadhi ya taifa ya mikumi ilitangaza nafasi kadhaa za askari wanyama pori kwa wenyeji wa mikumi na vijiji vinavyo izunguka hifadhi hiyo kama ujirani mwema kupitia kwa afisa mtendaji wa kijiji cha mikumi, na wanakijiji wengi walipeleka maombi yao kupitia kwa mtendaji wa kijiji na sifa walizo ainisha kuwa wanazitaka ni (a)-uwe na cheti cha form 4, (b)-uwe na cheti cha JKT au MGAMBO. na wapo wanakijiji amabao ni wazawa kabisa wa mikumi na wanasifa zote hizo walizo zihitaji na wamekwisha ita watu kwenye interview tarehe 31/01/2012 hakuna mzawa wa mikumi hata mmoja alie itwa kwenye usahili na ukimuuliza mtendaji wa kijiji anasema hajui kinacho endelea,sasa iwaje barua za maombi zipitie kwake na za majibu zipelekwe juu kwa juu hapo ni wazi kabisa kuwa waliochaguliwa kwenye usahili si wakazi halali wa mji wa mikumi wamewachagua watoto zao na nduguzao kwenye nafasi za wanamikumi wazawa, pia nasikia hata waziri wa maliasili yupo hifadhini mikumi tokea jana .
Sasa jamani haya manyanyaso ya wanyonge wa mikumi wanaostahiki kupewa nafasi hizi bila ya kuwa na mtetezi itakuwaje...? wenye uwezo wa kuwasaidia wana mikumi wasaidieni jamani huu ni uonezi wa wazi kabisa hasa serekali iliyoko madarakani mnawaona watu wenu hawa..? na ndio watakao wanyima kura 2015 kama hamto washuhulikia. "MAMBO HAYA TANAPA HADI LINI....?"
":hatari:
 
Inauma sana,nadhan wakati umefika watz tuache kuongelea pembeni,nchi hii ni yetu tunamwogopa nani jaman.
 
Vanmedy
Nafahamu nachokiandika na nimesoma.
Mleta thread athibitishe walioachwa hata usaili wenyewe bado
 
Back
Top Bottom