Hivi inakuwaje.....................

Kigeu geu....hukitaki ukiwa nacho ila ukiona kwamba mwingine anaweza kitaka/kitamani na kukichukua unataka urudishiwe.

Ubinafsi....wakati anakusema hufai anafanya vile kujifurahisha kwa kukufanya wewe ujione duni na sio kweli anavyokuona.Ndio maana anapoona mtu mwingine anafaidi anarudi mbio kulia "nimekosa...nimekosa."

Uroho....sikutaki pia nakutaka.Hawa ndo wale wanataka raha ya kuangalia chakula na kukila pia...kitu ambacho huwezi kuwa navyo viwili moja kwa moja....na kuchagua kimoja hawawezi.

Unyanyasaji....furaha yake inatokana na kuwafanya watu wengine waamini/wajione wao sio kitu.Anakuondolea/punguza kujiamini kwako ili uwe "Mwindwaji" mzuri.Unakua sehemu ya mchezo aupendao...akitaka kufurahi anakutapika...siku akiona vipi anakuweka mdomoni na sio anakumeza.Hapa kazi inabaki weka mdomoni...tema...weka..tema ikiwa utakubali kufanywa hivyo.


Kusema ukweli binadamu wengi kama sio wote tumeumbwa na roho ya wivu bila kuacha kigeu geu.Leo hii kuna mtu anaweza kutupa ndoo asioipenda sana kwasababu imepasuka ila kesho akimuona nayo jirani yake anavyoifurahia vaada ya kuichomea karoho kanamuuma na kutamani kwenda kudai ‘ndoo yake‘. Hivyo hivyo kwa wapenzi wakati mwingine mmoja anaweza kumuona mwenzake sio ‘hadhi yake‘...‘mchovu‘...‘mshamba‘...‘amefulia‘ n.k akamwacha kwa sababu hizo ila ikitokea yule mpenzi akakutana na mtu mwingine ambaye yeye ataenda mbali na kujaribu kumuinua na akabadilisha hayo/hicho kilichofanya aaachwe mwanzo lazima yule aliyeacha atamtamani huyu ex-mpenzi alikua upgraded na kuumwa roho kwamba "uzuri wote ule anafaidi/atafaidi mwenzangu?!SITAKI KABISA" Na ndio hapo usumbufu unapoanza maana all of the sudden unaonekana u-bora na sio choka mbaya anymore.

Lizzy umesema sawa kabisa yaani binadamu kweli tuna makuu
..................huwa tunajisahau kuwa tunapokiona cha nini huku twakunja uso na kuziba pua, kuna wengine wanajiuliza watakipata lini kishaufu kile chenye kunukia kama vikuba vya asmini!!
 
waswahili wasema, ukiwa nacho wakiona kibaya kumbe kuna wengine wanakitamani

Kweli kabisa Double A yaani hatuna utashi wa kutambua kweli kuwa hiki cha nifaa nikitunze! ndio kuna zile kero za kawaida na pia kuna extremes....... extremes zinawezapelekea ukaamua kutapika, hapo hulaumiwi na sidhani kama utawezatamani yarudia.......but kuna wale wanaamua tu kutapika kisa kwa jirani kaona sahani yenye chakula kipya ambacho hajakijua ladha na madhara yake...........
 
...........Hii inawezekana kabisa Elyer....yaani ukiwa nacho wakiona ca kawaida na kipo lakini kikitoweka unakitaka upya!

ni kama gari usiyoiendesha...unaiona barabarani..
hujjui inakula vipi mafuta,spare aghali na hazipatikani..
we unaitamani tu,kisa ni benz na wewe unaendesha vitz

kumbe vitz ina faida tele,mafuta kidogo,spare tele,inapenya kwa urahisi
but ukikaa barabarani ukiona ma vx na ma benz,
udenda unakutoka....lol
 
eehh, umenikumbusha msemo wa "kutema Big G kwa karanga za kuonjeshwa..."

a518e_funny-pictures-cat-watches-fish-in-toilet.jpg


"huwezi jua thamani ya mtu mpaka umpoteze...!"

Ah Mbu baby LOL
Aksante kwa huu ujumbe nimecheka yaani mtu kaki'tupa' wakati mwenzie akitafuta. !!

Hivi najaribu kujiuliza kwa watu wa aina hii wanaoamua kutapika ilhali wakingali wanatamani huwa wanatafakari faida na hasara za kutema Big G zao au wanatema tu japo kuwa bado zina utamu? Na zikiokotwa na mwingine ndo wanaamka na kutaka kumalizia ule utamu alobakisha??
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
[/FONT][/SIZE]
....ha ha ha, Bro BaK ulifikiri nishatemwa nini? LOL![/FONT][/SIZE]

Hebu funguka basi naweeeee! Ulishatemwa au ulitema? maana BaK alivyokushikia Bango yaani alikuwa na uhakika lazima uingie kwenye sred hii........imekugusa eh mpenzi?
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
we all want what we cant have.........

....................The Boss huu ni ujumbe mzito sana aksante sana Kaka.

Grass is Always Greener on the Other Side....., lakini ukifika huko unagundua kwamba Aint no Sunshine When She is Gone...

In short watu huwa tuna-concentrate on the negatives za mtu kwahiyo tunatafuta perfect partner tunajikuta tunaruka majivu tunakanyaga moto.. kwahiyo tukishamwacha mtu na kukutana na negatives za kule tunaanza kukumbuka positives tulizoziacha, na mara nyingi tukirudi the cycle inajirudia

Busara tupu za Babu aksante sana Babu. Angalau sasa naanza kuwaelewa wanaadam

Instead of learning to want what we have
Umeona eeee Babu!! We take for granted vile tulivyo navyo............
Speak for yourself...

HAhahahhahh Lizzy una visa!! Haya twambie mwenzetu unafanyafanyaje kuepuka vimbwanga vya kibinaadam?
 
HAhahahhahh Lizzy una visa!! Haya twambie mwenzetu unafanyafanyaje kuepuka vimbwanga vya kibinaadam?
Mamii nna principle yangu ambayo inaniepusha na “we all want what we can‘t have“......sikubali wala sijiruhusu kutaka kitu chochote ambacho najua fika siwezi kukipata/kuwa nacho.Iwe mpenzi...nguo..kiatu au gari...IF I CAN‘T AFFORD IT I DON‘T WANT IT.
 

...mwj1 :mimba:....

kuna 'kuvimbiwa' na kutapika,
kuna 'kuchefushwa' ukatapika.
Hizo ni involuntary actions.

Lakini, kuna wanaojitapisha makusudi,
kwa tamaa/ulafi wa kula kwingine,
Hao hawastahiki hata huruma.

Utamu wa ladha ya Chakula ni ulimi wako.
Usiposema na shibe yako, imekula kwako!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom