only83
JF-Expert Member
- Oct 15, 2010
- 5,343
- 2,525
...Kama ulishuhudia kauli ya VC wa University of Dar-es-salaam Profesa Mukandala wakati anaongea na vyombo vya habari kuhusu kuwafukuza wanafunzi takribani 40 na kitu unaweza kulia.Kauli zake ni za kinyama na ambazo haziwezi kutolewa na mtu mwenye watoto na anayeumia na shida za watu.Jamaa anaongea kwa hasira na kusema tutapeleka taarifa bodi ya mikopo na TCU ili watu hawa wasipate mikopo wala udahili chuo chochote cha umma...Hivi kwani wakipata udahili chuo kingine wewe unaumia nini? kama sio unyama na ukatili..ili siku moja uwakute watoto wamekuwa majambazi na wanateseka barabarani ufurahi au siyo,hivi hujui kuwa hawa ni vibaka unaowatengeneza mwenyewe na kuna siku watakukaba mtaani? Hvi kwanini unafanya unyama kwa watoto wa wakulima kwaajili ya kulinda maslahi ya mafisadi wachache? Ni mwanafunzi gani mjinga aanze vurugu bila sababu?
VC Mukandala,tambua hao ni watoto wa wazazi kama wewe,sio watoto wa mawe!!!
VC Mukandala,tambua hao ni watoto wa wazazi kama wewe,sio watoto wa mawe!!!