Hivi huyu mwanachama wa CUF Jussa ni mzima kiakili?

Acha uongo! Chadema ni ya watanzania usitake kulazimisha mambo ya udini hapa! Hivi bado tu hamjachoka kupotosha?
Bibie, tazama team ya CDM halafu tazama team ya CUF. Hivyo vyama vyote viwili ni vina udini
 
taarifa toka zanzibar ni kwamba chama cha wananachi (cuf), kilishindwa kulinyakua jimbo la uzini kutokana na kuwa na wakristo wengi na watu wa bara. Haya ni madai ya naibu katibu mkuu wa chama cha wananchi (cuf) zanzibar, ismail jussa ladhu. Je hii ina maana kuwa huyu ********* mwenzake aliyechaguliwa ni mtu wa bara na mkristo?
Kwa habari zaidi bonyeza hapa.

hao ndo wanasiasa waliofirisika sera vichwani mwao na kuleta udini, hawatafuti cause roots za kushindwa kwao wanaropoka tu kwa sababu wao ni wasemaji wa chama,
si jussa tu wapo wengi viongozi wa namna hiyo, watanzania tuwachekeche, wenzetu wanamaliza ubaguzi sisi tunataka kuukaribisha
wataanza kwa udini, watakuja kwa rangi nk

hoja yangu ; jussa kama jimbo hilo lina wakristo wengi na wabara wengi, ndo sababu ya kushindwa ni wazi kuwa wakristo na wabara wa jimbo la uzini hawaungi mkono chama cha cuf,

swali ; je, ni kweli chama chako kina waislamu na wazanzibar tu, katika wanachama wako wa jimbo la uzini,, ?
Swali ; kama sivyo unawarejesheaje imani wakristo na wabara walio ndani ya chama chako?
 
Za madrasa changanya na zako, halafu chapa mwendo. Nawe ni juha kama jusa


Madrasa imehusikaje hapa!!! Unatukaribisha tuje na makombora yetu tena au? Mumepata bahati sana mods hua wanawalinda! Wakiona maji yanazidi unga thread hua wanaifichaaaaaaa!
 
Taarifa toka Zanzibar ni kwamba Chama cha Wananachi (CUF), kilishindwa kulinyakua jimbo la Uzini kutokana na kuwa na wakristo wengi na watu wa bara. Haya ni madai ya Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) Zanzibar, Ismail Jussa Ladhu. Je hii ina maana kuwa huyu ********* mwenzake aliyechaguliwa ni mtu wa bara na mkristo?
Kwa habari zaidi Bonyeza hapa.
Hebu angalieni jina la huyo mwandishi wa makala, mulitegemea kupata maelezo gani yasiyokua haya!
 
Jussa aipalia makaa CUF


na Edson Kamukara


amka2.gif
SIKU chache baada ya Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) Zanzibar, Ismail Jussa Ladhu, kudai kuwa chama hicho kilifanya vibaya katika uchaguzi mdogo wa jimbo la uwakilishi la Uzini kwa sababu jimbo hilo lina Wakristo wengi na watu wa bara wengi, wadau mbalimbali wamemponda wakidai ni mbaguzi.
Jussa ambaye pia ni mwakilishi wa jimbo la Mji Mkongwe visiwani Zanzibar, alitoa madai hayo juzi, wakati akihojiwa na kituo cha televisheni cha Mlimani.
Katika uchaguzi huo ambao mgombea wa CCM, Mohammed Raza, aliibuka mshindi kwa kupata kura 5377, CUF ilidondoshwa na CHADEMA katika nafasi ya pili iliyojikusanyia kura 281 dhidi ya kura 223 za chama hicho.
Kauli ya Jussa ililalamikiwa na wananchi wengi waliotoa mawazo yao kupitia mitandao ya kijamii, wakisema moja kwa moja anataka kuashiria kuwa chama chake kinaungwa mkono visiwani pekee na na penye Waislamu.
Wachangiaji hao wakiwemo wanachama wa CCM, walidai kuwa Jussa analenga kuonyesha ni jinsi gani chama hicho kilivyo cha kibaguzi kama alivyokituhumu aliyekuwa mwanachama wao, Hamad Rashid Mohamed, mbunge wa Wawi.
“Nimehudhuria mikutano ya ufunguzi ya vyama vyote vitatu vikubwa vilivyoshindana katika uchaguzi ule, kwa maana ya CHADEMA, CCM na CUF na kila jioni nilikuwa najua kila kilichozungumzwa kwenye mikutano ya vyama hivyo viwili, hata kama sikuhudhuria ila nilishangaa kumsikia Jussa kuwa walishindwa kwa sababu kule kuna Wakristo wengi na watu wengi wa kutoka bara,” alisema mchangiaji mmoja.
Alisema kauli ile imezidi kumwanika Jussa kuwa ni mwanasiasa wa namna gani na kwamba vibaya kumsikia kiongozi kama yeye, akizungumza maneno hayo.
“ Jussa anataka kuwaambia Watanzania kuwa CUF wanaweza kushindana na kushinda pale tu ambapo kuna Waislamu wengi na misikiti mingi, kwamba penye Wakristo wengi, makanisa mengi, CUF haiwezi kushindana kwa dhati na kushinda au popote ambapo kuna watu wengi wa bara, CUF haiwezi kushindana na kushinda uchaguzi,” alihoji mchangiaji huyo kwenye mtandao wa kijamii.
Alisema kuwa Jussa anataka kuwasukuma Watanzania waamini katika propaganda za CCM zinazopalilia ubaguzi ndani ya jamii, kuwa CUF ni chama cha Waislamu na kuwa CUF ni chama cha Zanzibar.
Mchangiaji mwingine toka Zanzibar alisema kuwa kauli ya Jussa inajidhihirisha wazi kuwa ni mdini kwani hata wakati wa kampeni kule Uzini CUF walikuwa wakitembea na makaratasi waliyoita ni waraka wa maaskofu, wakiwadanganya wananchi kuwa unasema CHADEMA ni chama cha Wakristo.
“Nakumbuka ambavyo Jussa alitumia takriban asilimia 80 ya muda wa hotuba yake siku ya uzinduzi wa kampeni ambayo alikuwa mzungumzaji mkuu, kuizungumzia CHADEMA. Akaonyesha kushtushwa sana na nguvu ambayo chama hicho kiliyoionyesha katika uchaguzi huo.
Akahoji kulikoni. Kisha akaingiza propaganda, akisema kuwa nguvu hiyo ilikuwa na ajenda ya siri ya kusababisha vurugu Zanzibar, eti kama ambavyo kimekuwa kikifanya bara,” alisema mchangiaji huyo.
Hata hivyo, wakati Jussa akitoa kauli hiyo, mbali na Raza pia mbunge wa Jamhuri ya Muungano kutoka jimbo hilo, Sief Khatib (CCM), ni Muislamu aliyechaguliwa na hao anaowaitwa Wakristo.
Kada mmoja wa CCM ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini, aliliambia gazeti hili jana kuwa anajipanga kumwanika Jussa na chama chake kutokana na uzushi wa kutaka kupandikiza chuki za udini nchini.

 
Hebu angalieni jina la huyo mwandishi wa makala, mulitegemea kupata maelezo gani yasiyokua haya!

Jina la mwandishi sio hoja,hoja ni alichokiandika na zaidi kaweka na evidence,bora mwambieni tu huyo mwarabu koko wenu kama siasa zimemshinda akae kimya kama hawezi basi ajiandae kuhama hii nchi afuatane na rafiki yake rost tamu anayejipanga kuhama tz.
 
Sikutarajia kwa mwanasiasa kama Jussa kutoa kauli kama hii, hii inadhibitisha kuwa CUF ni chama cha kidini na kikabila, tuna takiwa tukiogope kama UKOMA, sikutegemea hili kabisa, KUMBE JUSSA ni MS***** Kiasi hiki?
wana JF tuipige vita CUF kama wote wana vision moja ambayo ni ya kidini

Ni lini na ni wapi Jussa aliwahi kuwa mwanasiasa?
 
Kwa staili hii jussa ametujuza kuwa CUF ni chama cha kidini,ni heri wakajikita katika kueneza dini kuliko siasa.
 
Mwenyekit wa CUF na uongozi wa juu wakishindwa kutolea maelezo kauli hii ya Juha sorry Jussa.Itakuwa ni kweli wanaunga mkomo matamshi yake!Hv huyu jamaa ni nani hasa CUF mpaka awe anatoa kauli za kipoyoyo namna hiyo?Na we Prof Lipumba ukikaa kimya kwa hili tunakuvua ukabila maana utasababisha wanyamwezi wote tuonekane wanafiki!!Mnyamwezi gani legelege namna hiyo bana aaagh!!!
 
CUF ni ya Waislamu na CHADEMA ni ya wakristo na hii ndio sababu itakayo ifanya CCM itawale milele.

cuf ni waislam chadema wakristo na CCM YA MAJAMBAZI NA MATAPELI sasa hapo nani ana nafuu?
 
Tulishuhudia mwaka 2005 kampeni za CUF na tumeshuhudia mwaka 2010 kampeni za CHADEMA, hivi vyama vipo religious oriented, huo ndio uwazi wanaokataa na wakatae. havitaongoza nchi hii milele, kwa sababu zifuatazo:
0: Nchi hii idadi ya wakristo na waislamu inafanana hii ni kwa mujibu wa wikipedia, hivyo chama chochote kitakachojihusisha na dini fulani ni dhahiri kitapoteza watu wa dini nyingine na pia kitapoteza watu wa dini ile kinachoipigania kwa kuwa wengine ni makada wa vyama vingine na wengine hawapendi siasa za udini.
1: CCM inajitahidi sana kutoweka wazi udini(kuuficha hata kama upo)
2: waanchi wengi hawakubaliani na siasa za udini (siasa za maji taka) ushahidi angalia uchaguzi wa 2005 na 2010.
 
Hapa hakuna mwanasiasa ila kuna mtu mmoja mbaya sana amejificha ndani ya siasa na a hana nia njema na watu wa nchi hii hasa weusi toka bara Mzee Karume aliwaona hawa na mwaka 1964 akafanya kweli, hapa dini ameifanya kama hatua ya kwanza ili apate kuungwa mkono na watu wote wa dini yake na akishafanikiwa atawabagua weusi. Mimi naona kina jusa na watu wa type yake wangefanya tu utaratibu warejee walikotkea wakatuachia kisiwa chetu kwani naona wameshalewa na ukarimu wetu wa kiafrika!
 
Acha uongo! Chadema ni ya watanzania usitake kulazimisha mambo ya udini hapa! Hivi bado tu hamjachoka kupotosha?

Sio uwongo huo ndo ukweli mtupu, hata mkiukataa utabaki hivo hivo, CHADEMA ni chama cha kikristo tena kikiwa na mrengo wa kikatoliki (makafiri wakubwa). Huhitaji elimu ya chuo kikuu kulijuwa hilo, sera zao zinatoka kwa kadinali Pengo, hata hapa JF wanaokisapoti ni wakristo, na katibu mkuu wa chadema ni PADRI MUASI
 
Back
Top Bottom