Hivi Hii Ya Marando Imekaaje?

[QUOTE=Ntemi Kazwile;1586048]Mkuu,

Hapa kuna shida kubwa, kama mimi sipendi ushoga siwezi kuwa wakili wa kutetea mtu anamshitake mwenzake kwa kumwita shoga! Hata kama ni kazi yangu kutetea watu watendewe haki, nikifanya hivyo nitakuwa napingana na dhamira yangu ya kupinga ushoga na wala sitaweza kumtetea ipasavyo kwa sababu nafsi yangu inataka nimzomee huyo shoga ili aache ushoga sasa nitawezaje kumtetea asizomewe??

Marando anatuzuga huyu wala siyo jemedari wa kupinga ufisadi. Mbona sijawahi kumsikia Lisu akiwa wakili wa hao mafisadi?[/QUOTE]



Ndugu Mtemi,

Tufanye kwamba ungekuwa "criminal lawyer", je ungekuwa unatetea watu wa namna gani? wezi, wauaji, wabakaji? maana hao wote ungewachukia, ina maana basi ungeacha kazi ya uwakili.

Kumbuka kuwa hawa akina manji, na wengine wengi wanaotajwa kwenye media, kisheria ni watuhumiwa tu, na mahakama haijathibitisha kama wametenda makosa hayo. Kwa hiyo ukiwa kama wakili unawatetea watuhumiwa ukiwa na assumption kuwa "they are innocent". Ni jukumu la waendesha mashitaka (serikali) kuthibitisha mahakamani kuwa hawa watuhumiwa kweli wametenda hilo kosa. Kusipokuwepo mawakili wa utetezi,kila mtu anaweza kubambikizwa kesi.

Pia ufahamu kuwa mawakili wote ni sehemu ya mahakama, wao ni "officers of the court" wanatakiwa kuhakikisha kuwa mahakama inatenda haki. Na kila mtu awe fisadi, mwizi, muaji, shoga, wote wana haki zao kikatiba na kibinadamu. Wakili yuko pale kuhakikisha haki ya mtuhumiwa haivunjwi.
 
Sasa inamaana hata kanisani/msikitini anakosali/swali RA wasimkubali coz fisadi? Kutetewa ni haki ya kila mtu hata aliyeua bado anapewa/ anatakiwa kupata wakili upo hapo?

Hatupingi haki ya mtu kutetewa,the concern ni double face ya MALANDO....Akiwa on court asema tofauti na akiwa kwenye podiums...kwani proffesion haina limits? haina ethics? tusijaribu kuwahadaa watu....unaweza fanya proffesionalism still uka maintain political status quo kwa kuchagua where to stand...angekua dr.angefanya hata abortion ili tu kupata pesa huku akitumia kivuli cha proffesionalism
 
Kweli Tanzania is full of sick and short minded people,,,, sasa ina maana manji mahitaji yake yote ya kila siku anapata kwa wale wenye kadi ya ccm?
 
Kila mtanzania anaepinga na asiyepinga ufisadi ni FISADI.
Kwa Marando kumtetea Manji...nadhani ni sawa tu kwa sababu yupo kazini kama mwanasheria....Ndio maana kuna watu wanaua tena kwa makusudi na ushahidi wa kuwatia hatiani unakuwepo wazi lakini wanatafutiwa wanasheria wa kuwatetea? Je wajuaje labda kawekwa ili kumzamisha fisadi?
 
Jamani wana CDM angalieni msije mkashindwa kuendesha mambo yenu. Isije ikawa huyo jamaa amewekwa kimtego ili kuvuruga chama. ikiwezekana mtimueni aishie zake. Huyu anaweza kuwa ndio "intellijensia wa CCM"
 
Au ndio kukamilisha usemi unaosema "MCHAWI MPE MWANAO AKULELEE?"
 
Huyu ndie Mabere Marandu alietaka kuwa Spika wa Bunge!!!!!! badala ya kuwatetea watuhumiwa wa maandamano ya Arusha, anamtetea yule aliemtuhumu ktk majukuu ya kisiasa!!!!
 
Kweli Tanzania is full of sick and short minded people,,,, sasa ina maana manji mahitaji yake yote ya kila siku anapata kwa wale wenye kadi ya ccm?
Tatizo sio proffesion tatizo ni ethics na moral kumtetea manji, swali langu ni kuwa marando akiambiwa na rostam nenda kanitetee dowans au issue yoyote hapo wadau mtasemaje.....watu wanajibu kwa ushabiki wa vyama but bottom line practise what you preach kwa hiyo wanaomtetea marando kwa kivuli cha ni wakili watasema nini akimtetea rostam koz inaonekana jamaa ukifika dau anakutetea...ndio wanasiasa wetu hao
 
[QUOTE=Ntemi Kazwile;1586048]Mkuu,

Hapa kuna shida kubwa, kama mimi sipendi ushoga siwezi kuwa wakili wa kutetea mtu anamshitake mwenzake kwa kumwita shoga! Hata kama ni kazi yangu kutetea watu watendewe haki, nikifanya hivyo nitakuwa napingana na dhamira yangu ya kupinga ushoga na wala sitaweza kumtetea ipasavyo kwa sababu nafsi yangu inataka nimzomee huyo shoga ili aache ushoga sasa nitawezaje kumtetea asizomewe??

Marando anatuzuga huyu wala siyo jemedari wa kupinga ufisadi. Mbona sijawahi kumsikia Lisu akiwa wakili wa hao mafisadi?



Ndugu Mtemi,

Tufanye kwamba ungekuwa "criminal lawyer", je ungekuwa unatetea watu wa namna gani? wezi, wauaji, wabakaji? maana hao wote ungewachukia, ina maana basi ungeacha kazi ya uwakili.

Kumbuka kuwa hawa akina manji, na wengine wengi wanaotajwa kwenye media, kisheria ni watuhumiwa tu, na mahakama haijathibitisha kama wametenda makosa hayo. Kwa hiyo ukiwa kama wakili unawatetea watuhumiwa ukiwa na assumption kuwa "they are innocent". Ni jukumu la waendesha mashitaka (serikali) kuthibitisha mahakamani kuwa hawa watuhumiwa kweli wametenda hilo kosa. Kusipokuwepo mawakili wa utetezi,kila mtu anaweza kubambikizwa kesi.

Pia ufahamu kuwa mawakili wote ni sehemu ya mahakama, wao ni "officers of the court" wanatakiwa kuhakikisha kuwa mahakama inatenda haki. Na kila mtu awe fisadi, mwizi, muaji, shoga, wote wana haki zao kikatiba na kibinadamu. Wakili yuko pale kuhakikisha haki ya mtuhumiwa haivunjwi.[/QUOTE]
Huyo ni mwanasiasa pia tena close aide wa presidential candidate ambaye ametengeneza heshima yake kwa kupinga ufisadi (slaa), sasa leo yupo na manji akisingizia profession then next atamtetea mramba....huyo ndiye former MP of eala aliyeingia kwa kura za ccm but now ni chadema may after that atakuwa cuf
 
Mimilabda mngeniambia inakuwaje Kada wa CDM anamtetea Kada wa CCM madarakani?

CDM tunawatumia watu kama hao ili watuletee nyaraka muhimu ili tukianza kuwalipua tunawamaliza mmoja mmoja.

Hii ni jambo zuri maana ukitaka kufahamu adui yako ana nini mfanye kwanza rafiki yako.
 
[/I]

Huyo ni mwanasiasa pia tena close aide wa presidential candidate ambaye ametengeneza heshima yake kwa kupinga ufisadi (slaa), sasa leo yupo na manji akisingizia profession then next atamtetea mramba....huyo ndiye former MP of eala aliyeingia kwa kura za ccm but now ni chadema may after that atakuwa cuf



Fahamu kuwa mahakama ndio chombo pekee na cha mwisho cha kusimamia haki za watu wote.

Utendaji wa mahakama unafuata “facts” za kisheria, na sio story za kwenye magazeti ua radio au tv. Lazima ushahidi uwakilishwe mahakamani ndipo mahakama itoe uamuzi.
Bila hivyo, utakubalina nami kuwa kuna watu huwa wanazushiwa habari na habari hizo huwa zinaenea miongoni mwa jamii, sasa je ungependa mtu ahukumiwe jela kwa sababu za kizushi? Nikikuita mwizi au jambazi kwa vile tu sijui umepataje utajiri wako wa magari na maduka, halafu habari ikaenea, itakuwa sawa kweli kwamba wewe ufungwe bila kutetewa? Kama ni mpenda haki, jibu lako litakuwa hapana. Na mahakama ndivyo ziko hivyo, lete kesi, lete ushahidi unaoridhisha, then mtuhumiwa anapewa adhabu yake.

Wakili anakuwepo pale mahakamani kama afisa wa mahakama kuhakikisha haki inatendeka. Kama ushahidi upo wa kutosha, hata wakili angekuwa mzuri kiasi gain, mtuhumiwa atapatikana na hatia. Kwa hiyo huyo Manji kama ushadi upo, atapatikana tu.
Sasa kiutaratibu katika utawala wa sheria, kila mtu ni presumed innocent until proven guilty. Na Marando kama wakili anawajibika kuhakikisha mahakama inatenda haki kwa Manji (hata kama hampendi).

Hata mimi nina hisia kuwa manji ni fisadi, mramba ni fisadi, EL, RA, na wengineo, lakini, hizi ni hisia zangu mimi kama raia. Mbele ya sheria, hawa watu wanahitaji kutetewa. Ushahidi ukiwa mzito, wanatiwa hatiani na watapewa adhabu wanayostahili.

Kwa upande mwingine, jiulizeni, kwanini Manji ahatarishe uhuru wake kwa kutetewa na wakili ambaye ni mwanachama wa upinzani? Hii ni kwa sababu hata Manji mwenyewe anajua kuwa kazi za uwakili ziko separated na ufuasi wa kisiasa.
 
[/I]
Fahamu kuwa mahakama ndio chombo pekee na cha mwisho cha kusimamia haki za watu wote.

Utendaji wa mahakama unafuata “facts” za kisheria, na sio story za kwenye magazeti ua radio au tv. Lazima ushahidi uwakilishwe mahakamani ndipo mahakama itoe uamuzi.
Bila hivyo, utakubalina nami kuwa kuna watu huwa wanazushiwa habari na habari hizo huwa zinaenea miongoni mwa jamii, sasa je ungependa mtu ahukumiwe jela kwa sababu za kizushi? Nikikuita mwizi au jambazi kwa vile tu sijui umepataje utajiri wako wa magari na maduka, halafu habari ikaenea, itakuwa sawa kweli kwamba wewe ufungwe bila kutetewa? Kama ni mpenda haki, jibu lako litakuwa hapana. Na mahakama ndivyo ziko hivyo, lete kesi, lete ushahidi unaoridhisha, then mtuhumiwa anapewa adhabu yake.
Wakili anakuwepo pale mahakamani kama afisa wa mahakama kuhakikisha haki inatendeka. Kama ushahidi upo wa kutosha, hata wakili angekuwa mzuri kiasi gain, mtuhumiwa atapatikana na hatia. Kwa hiyo huyo Manji kama ushadi upo, atapatikana tu
Sasa kiutaratibu katika utawala wa sheria, kila mtu ni presumed innocent until proven guilty. Na Marando kama wakili anawajibika kuhakikisha mahakama inatenda haki kwa Manji (hata kama hampendi).
Hata mimi nina hisia kuwa manji ni fisadi, mramba ni fisadi, EL, RA, na wengineo, lakini, hizi ni hisia zangu mimi kama raia. Mbele ya sheria, hawa watu wanahitaji kutetewa. Ushahidi ukiwa mzito, wanatiwa hatiani na watapewa adhabu wanayostahili.
Kwa upande mwingine, jiulizeni, kwanini Manji ahatarishe uhuru wake kwa kutetewa na wakili ambaye ni mwanachama wa upinzani? Hii ni kwa sababu hata Manji mwenyewe anajua kuwa kazi za uwakili ziko separated na ufuasi wa kisiasa.
Mkuu hebu kuwa real kidogo, unadhani Marando akiuona ushahidi beyond reasonable doubt dhidi ya mteja wake Manji ataiambia mahakama imuadhibu mteja wake kwa maana nyingine Manji apoteze kesi?
 
Mkuu hebu kuwa real kidogo, unadhani Marando akiuona ushahidi beyond reasonable doubt dhidi ya mteja wake Manji ataiambia mahakama imuadhibu mteja wake kwa maana nyingine Manji apoteze kesi?


Attorney-client priviledges:
Wakili yeyote hatakiwi kutoa siri za mteja wake, bila kujali mteja ni kibaka, fisadi, mwizi n.k.
 
Mabere Nyaucho Marando ni wakili wa Mengi.Huyo Marando ambaye ni wakili wa Manji ni yupi?Au kesi hii ina mawakili waliofanana majina pande zote mbili?
 
Mabere Nyaucho Marando ni wakili wa Mengi.Huyo Marando ambaye ni wakili wa Manji ni yupi?Au kesi hii ina mawakili waliofanana majina pande zote mbili?


Mimi kwa kweli sijui kuhusu undani wa kesi yenyewe, nipo nje ya nchi. Nilichokuwa nachangia, ni kuwa mtuhumiwa yoyote ana haki ya kutetewa mahakamani, bila kujali tuhuma alizonazo. Kwa hiyo kama Marando ni wakili wa Mengi ni sawa tu, au ni wakili wa manji, nayo sawa tu.
 
Nakubaliana na wewe ila kuna suala moja hapa,daktari si mwanasiasa,marando ni mwanasiasa tena anayepiga ufisadi sasa akianza kutetea watu wenye tuhuma za ufisadi unaeleweka kwel?tuache ushabiki jmn na tuseme ukweli,yan ina maana hta rostam akija kwake kutaka amtetee kwenye kesi kma ya dowans angeenda maana ethics zinaruhusu?
hata kama daktari ni mwanasiasa ethics zinambana amuudumie mgonjwa ndo maana wanakula viapo! Marando anfanya kazi pale kwa misingi ya jinsi sheria inavyosema kama mwanasheria hata fisadi ana haki ya kutetewa!
 
Ndio siasa zetu hizo za kuganga njaa...hakuna 'tunalolisimamia' katika maisha!
 
Kwa upande wa Marando kama mwanachama wa Chadema na kuwa upande wa kupigani haki. This is a conflict of interest here....Kitu gani kinamfanya kuwa na shida ya kifedha kiasi hiki? I don't believe mafisadi can buy anyone in Tanzania. Kama uongozi wa Chadema unajali wananchi they have to watch out for these kind of things, other wise we as Tanzanians we are not going to be bias and criticize CCM na mafisadi while leave Chadema alone. This is not going to happen...If this is true, Marando has to give explanation here.
 
Back
Top Bottom