serio
JF-Expert Member
- Apr 15, 2011
- 7,306
- 4,681
kuna ndugu yangu mmoja alipata kazi security group na huu ni mwezi wake wa pili kazini. anadai kwamba wanafanya kazi masaa (8) na overtime ya masaa manne(4) kwa siku. cha kushangaza, wameambiwa hawatapewa hela ya overtime kwa miezi minne ya kwanza kazini. hela ya overtime inasiniwa kwamba wamelipwa lakini hawapewi sababu kuu ikiwa, "wako kwenye miezi ya mtazamio"
Istoshe, ukipata tatizo kazini, kampuni haikupi msaada wowote ule, uwe polisi, jela au wapi, they dont want to know. na bila kuonekana kazini ndani ya siku tatu, huna kazi.
kwa mfano.. kuna laki tano zilipotea katika benki moja hapa mjini.(pesa zilipotelea ndani kwa teller), cha kushangaza walinzi (waliokua nje) ndio walikamatwa na kupelekwa polisi. walikaa ndani wiki mbili mpaka walinzi wenzao wa security group wakachanga changa 120,000/= kuwatolea dhamana.. kampuni haikushughulika nao, na sasa hawana kazi.
ndugu zangu, maisha bora kwa kila mtanzania yatawezekana kwa hali hii????
Istoshe, ukipata tatizo kazini, kampuni haikupi msaada wowote ule, uwe polisi, jela au wapi, they dont want to know. na bila kuonekana kazini ndani ya siku tatu, huna kazi.
kwa mfano.. kuna laki tano zilipotea katika benki moja hapa mjini.(pesa zilipotelea ndani kwa teller), cha kushangaza walinzi (waliokua nje) ndio walikamatwa na kupelekwa polisi. walikaa ndani wiki mbili mpaka walinzi wenzao wa security group wakachanga changa 120,000/= kuwatolea dhamana.. kampuni haikushughulika nao, na sasa hawana kazi.
ndugu zangu, maisha bora kwa kila mtanzania yatawezekana kwa hali hii????