Hivi haya ndio mapenzi au kitu gani hiki????.....!

Sajenti

JF-Expert Member
Apr 24, 2008
3,651
412
Kuna familia moja imehamia mtaani kwetu ni kama miezi 7 sasa tangu wahamie hapa. Huyu bwana amekuja yeye na mkewe na watoto watatu, mmoja ni wa kike anasoma sekondari na wawili ni wavulana wote wako shule ya msingi. Kitu kinachonishangaza kwa mtazamo wangu huyu bwana haipiti wiki bila kusikia zogo yeye na mkewe na wakati mwingine nahisi hata mkong'oto huwa unatembea humo ndani kwa mama. Siku za mwanzo nilidhani ni tofauti za kawaida baina ya Mr & Mrs lakini kadri siku zinavyokwenda hii hali inaendelea. Mzee ni mtumishi wa taasisi moja inayosimamia masuala ya nishati na mama ni nesi kwenye hospitali moja binafsi hapa mjini.

Sasa ninachojiuliza ni je hii mikong'oto ya angalau mara 2 kwa mwezi huyu mama inakuwaje maana hata kama ni mtu kufanya kosa basi angalau aonywe mara moja na mambo yawe sawa. Najaribu kutathimini mambo ya hawa majirani zangu sipati jibu........Msiniulize eti kwa nini nafatilia mambo ya nyumba ya mtu..kuna siku nililazimika kutoa hifadhi kwa watoto wa huyo bwana baada ya kosovo kuwa zito likawakumba na watoto...:frusty::frusty:
 
Laiti mabati na kuta yangekuwa yanaongea... tungeweza jua...!waachie wenyewe!:eyeroll2:
 
Huyo Baba atakuwa mkorofi bwana wanawake walivyo wanyenyekevu hawezi kila siku anarudia kosa na kupigwa..mwanamme ana gubu:confused2:
 
:mad2: :glasses-nerdy: :mad2:
Huko ni knitwear na wakati hayo mambo yalikuwa long tym ago. lets get up with time and leave those bad traditions. we our wives an children lets show them real lov an not hatred.
 
Sajenti nadhani bado unayo nafasi kubwa na nzuri ya kuisaidia familia hii. Vile watoto walikuja kupata hifadhi kwako basi nadhani ni wakati mzuri pia wa kujenga mahusiano na mzazi mwanaume ukapata nafasi ya kumshauri kwa upeo wako na zaidi utakuwa unawasaidia watoto.Ni kazi nzito na inahitaji moyo lakini kuwa mwangalifu maana binadamu sisi hatuna shukrani.. Huu ni ushauri tu.
 
Huyo Baba atakuwa mkorofi bwana wanawake walivyo wanyenyekevu hawezi kila siku anarudia kosa na kupigwa..mwanamme ana gubu:confused2:

Aisee!!!! nafikiri umesema hivyo kwa kuwa tu na wewe ni mwanamke. Unasema wanawake ni wanyenyekevu?? Wee acha tu, ukiona nyumba imetulia ujue mwanaume ameamua kujifanya mjinga ili maisha yaendelee. Sema kwenye hiyo nyumba atakuwa jamaa hana uvumilivu. Wanawake wanaweza wasiwe wepesi kuinua mkono kupiga, lakini ukimpata anayejua kuchonga, mbona utakonda?
 
Sajenti nadhani bado unayo nafasi kubwa na nzuri ya kuisaidia familia hii. Vile watoto walikuja kupata hifadhi kwako basi nadhani ni wakati mzuri pia wa kujenga mahusiano na mzazi mwanaume ukapata nafasi ya kumshauri kwa upeo wako na zaidi utakuwa unawasaidia watoto.Ni kazi nzito na inahitaji moyo lakini kuwa mwangalifu maana binadamu sisi hatuna shukrani.. Huu ni ushauri tu.

Sajenti Nawaza huu ushauri wa Pakawa ni mwafaka, ufanyie kazi na utakuwa umeisaidia hiyo familia, ingawa kweli inaitaji uangalifu wa aina fulani pindi utakapokuwa unabadilishana mawazo na huyo bwana, mwangalie tabia aliyonayo halafu tafuta mbinu ya kuanza kumshauri.
 
huyo mdingi atakuwa bado yuko premiteve sana, dunia ya sasa ni modernised sana
kila demokrasia hutembea hata makosa yangekuwa makubwa kiasi gani sasa ukimpiga
mwanamke unakuwa unamfundisha, unamuonya ama unamuumiza maana umri wa kupigwa
nao mmmmmh hapana
 
Sajenti nadhani bado unayo nafasi kubwa na nzuri ya kuisaidia familia hii. Vile watoto walikuja kupata hifadhi kwako basi nadhani ni wakati mzuri pia wa kujenga mahusiano na mzazi mwanaume ukapata nafasi ya kumshauri kwa upeo wako na zaidi utakuwa unawasaidia watoto.Ni kazi nzito na inahitaji moyo lakini kuwa mwangalifu maana binadamu sisi hatuna shukrani.. Huu ni ushauri tu.
...Pakawa, kifupi ni kuwa baba mwenye nyumba kwa nje ni mtu mwerevu tu kiasi kwamba hutegemei kama ni mtu wa kuvurumishana na mkewe kila wakati.mUshauri wako ni mzuri sana kinachonifanya nisite kujaribu kuwa msuruwishi wa hii familia ni kuwa kuna j2 moja kulikuwa na kama kikao cha wanafamilia maana walipata ugeni wa watu wengi tu..muda si mrefu kukaanza mabishano makali sana kati ya father house na mmoja wa jamaa waliokuja hapo (nahisi ana undugu na mwanamke) na kauli niliyosikia ni kuwa " kama unamuonea huruma dada yako mchukue uende naye na naweza kukuchapa na wewe pia". Hilo peke yake likanipa picha kuwa huyu bwana ni mgumu na huenda matatizo yao yanafahamika hata huko kwa ndugu zao. Nikatulia..
 
Huyo Baba atakuwa mkorofi bwana wanawake walivyo wanyenyekevu hawezi kila siku anarudia kosa na kupigwa..mwanamme ana gubu:confused2:
..Sorry FL1, kwa kizazi cha wanawake wa sasa sidhani kama wana unyenyekevu wowote. Sio kama na-support huyu bwana kumtwanga mkewe kila siku la hasha. isipokuwa majority of wanawake wa siku hizi ni wajeuri, kiburi na dharau na hasa kwa wale walioelimika na kupata kazi zenye kipato. Wao hudhani akishakuwa na uhakika wa kuvaa apendavyo, na pocket money basi haitaji mume utakuta kunakuwa na ukorofi wa hovyo hovyo tu....Nadhani mumeo FL1 anaraha ya ajabu hapa duniani kupata mke wewe laiti wanawake wengi (wote haiwezekani) kuwa kama wewe dunia ingekuwa sehemu bora ya kuishi...
 
Unaweza ukasikia mayowe kana kwamba ni mke anapewa kichapo... kumbe ndo wanapeana tamtam bana...!! Waachie wenyewe msaaada ukihitajia utatafutwa!!!
 
Unaweza ukasikia mayowe kana kwamba ni mke anapewa kichapo... kumbe ndo wanapeana tamtam bana...!! Waachie wenyewe msaaada ukihitajia utatafutwa!!!

Tamu tamu mpaka watoto kutumuliwa na kupewa hifadhi kwingineko mmmmh??????????
 
Unaweza ukasikia mayowe kana kwamba ni mke anapewa kichapo... kumbe ndo wanapeana tamtam bana...!! Waachie wenyewe msaaada ukihitajia utatafutwa!!!
...Na ndio maana nikataka kujua kama ndio mapenzi yao au inakuwaje???? Yote yanawezekana..................:mad2:
 
Ukiona mwanaume anampiga mkewe ujue anakabiliwa na tatizo la ushamba uliokisiri kwa kuwa kipigo sio dawa ya tatizo badala yake ndiyo kuchochea tatizo!!!! Mwanamke haonywi kwa kipigo bali kwa upendo usio elezeka. :confused2:
 
Back
Top Bottom