Sajenti
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 3,651
- 412
Kuna familia moja imehamia mtaani kwetu ni kama miezi 7 sasa tangu wahamie hapa. Huyu bwana amekuja yeye na mkewe na watoto watatu, mmoja ni wa kike anasoma sekondari na wawili ni wavulana wote wako shule ya msingi. Kitu kinachonishangaza kwa mtazamo wangu huyu bwana haipiti wiki bila kusikia zogo yeye na mkewe na wakati mwingine nahisi hata mkong'oto huwa unatembea humo ndani kwa mama. Siku za mwanzo nilidhani ni tofauti za kawaida baina ya Mr & Mrs lakini kadri siku zinavyokwenda hii hali inaendelea. Mzee ni mtumishi wa taasisi moja inayosimamia masuala ya nishati na mama ni nesi kwenye hospitali moja binafsi hapa mjini.
Sasa ninachojiuliza ni je hii mikong'oto ya angalau mara 2 kwa mwezi huyu mama inakuwaje maana hata kama ni mtu kufanya kosa basi angalau aonywe mara moja na mambo yawe sawa. Najaribu kutathimini mambo ya hawa majirani zangu sipati jibu........Msiniulize eti kwa nini nafatilia mambo ya nyumba ya mtu..kuna siku nililazimika kutoa hifadhi kwa watoto wa huyo bwana baada ya kosovo kuwa zito likawakumba na watoto...:frusty::frusty:
Sasa ninachojiuliza ni je hii mikong'oto ya angalau mara 2 kwa mwezi huyu mama inakuwaje maana hata kama ni mtu kufanya kosa basi angalau aonywe mara moja na mambo yawe sawa. Najaribu kutathimini mambo ya hawa majirani zangu sipati jibu........Msiniulize eti kwa nini nafatilia mambo ya nyumba ya mtu..kuna siku nililazimika kutoa hifadhi kwa watoto wa huyo bwana baada ya kosovo kuwa zito likawakumba na watoto...:frusty::frusty: