Sajenti
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 3,651
- 412
Niko mbele ya runinga yangu naangalia hili shindano lililopewa jina la Dume challenge....washiriki wanapimwa kuanzia michezo hadi uelewa wa mambo ya kawaida kabisa ambayo kwa washiriki wale wanaonekana ni wakubwa kiumri kiasi fulani nilitegemea mtu hatoshindwa kujibu maswali. Paliponiacha hoi mtu ameulizwa swali ataje mikoa 5 ya Tanzania inayoanza na herufi "M" mtu anashindwa aliyefunga kazi ni yule jamaa anaitwa Mgune eti anataja mkoa wa Musoma wakati huo huo anataja mkoa wa Mara.....ndio yale yale ya Mheshimiwa, Pemba na Zimbabwe tunapata Tanzania?