Hivi CUF Bado niIko Kambi Ya Upinzani?

Fredrick Sanga

JF-Expert Member
Jan 27, 2011
3,153
697
Ni kitu ambocho inabidi kifanyiwe kazi, kuanzia kwa msajili wa vyama vya siasa, baraza la wawakilishi hadi bunge la Jamhuri. Muafaka kati ya CUF na CCM uko katika misingi ya kugawa nchi katika sehemu mbili, yaani Tanzania Tanganyika na Tanzania Zanzibar, muafaka huu uko upande mmoja wa muungano, sasa iweje CUF isishirikishwe katika serikali ya Muungano. Mwenyeki Mhe Sharif ni makamu wa kwanza wa Raisi wa Tanzania Zanzibar, naona kama ana ugumu wa kukaa bungeni kama mpinzani. Muafaka huu unafanya divide and rule ndani ya CUF, nao sasa sidhani kama wametafakari na kupitia tafakuri hiyo na kouna kama wana sera kuusu muundo wa serikali, muundo wa baraza la wawakilishi na muundo wa Bunge.

Swala la Chama kimoja kuwa na muafaka upande mmoja wa muungano, inakuwaje? muheshimiwa Msajili wa vyama, sio kwamba chama kinatakiwa kiwe na msimamo unaoeleweka pande zote za muungano. Labda tuseme muafaka uvunjwe au uwe extended upande wa Tanzania Tanganyika.

Kwa hali hii, kabla ya vyama vingine kuukubali upinzani wa CUF, Muafaka uangaliwe.
 
Back
Top Bottom