Peter Kilanga
New Member
- Mar 5, 2008
- 3
- 0
Jamani watanzania mimi ni mwanafunzi lakini naomba swali hili nisaidiwe jamani kulijibu.Ni kwa kipindi kirefu nimesikia migogoro ndani ya chuo kikuu cha Dar Es Salaam.
Chuo kiku cha dare s salaam ni chuo maarufu sana duniani kifupi cha chuo hicho hujulikana hivi UDSM.Chuo hiki kimebujikwa na rundo la wanafunzi wapya waingiao kila mwaka na hivyo kusababisha hata kuwa na upungufu wa majengo.Hivi ni lazima kweli wanafunzi wote wamalizao kidato cha sita na kuwa na sifa za kujiunga na Vyuo kwa masomo ya elimu ya juu wajiunge UDSM?Hivi ni kitu gani kilichopo pale ambacho vyuo vingine vyenye sifa kama ya UDSM hamna?.Kwa binafsi yangu mimi naona migogoro mingi iliyowahi kwisha tokea ni kutokana na wingi wa wanafunzi hao na hivyo kupelekea uongozi wa chuo kushindwa kuwahudumia kikamilifu.Hivi kuna haja gani ya wanafunzi kurundikana pale.Mimi nawasihi wanafunzi wenzangu migogoro katika sekta ya elimu hususani ya juu hushusha kiwango cha elimu kitolewacho mahala husika nchi yetu imekuwa ikijitahidi sana katika sekta ya elimu na hivyo kuwa na vyuo mbalimbali vyenye sifa.Mimi naomba kuliko kurundikana chuo kimoja na kutopata kile tulichokusudia au kukipata katika wakati tusiokusudia ni bora kabla ya kujiunga na UDSM ni jukumu letu kutafuta vyuo vyenye sifa kama ya UDSM ili pia ikiwezekana basi twende huko kuliko kujazana sehemu moja.
Na vile vile uongozi wa chuo hivi ni kigezo gani chatumika kuwa na idadi inayotakiwa ya wanafunzi chuoni?Kwa upande wangu nahisi ni kutokana na uwezo wa vyumba vya madarasa katika kuchukua wanachuo.Sasa kama ndivyo hivyo kama nijuavyo mimi inakuwaje wanafunzi wakawa wengi kuliko Vyumba vya madarasa?Naomba uongozi wa UDSM pamoja na SERIKALI iliangalie swala hili kwa macho yote na kwa mikono yote katika kulipatia ufumbuzi.
Chuo kiku cha dare s salaam ni chuo maarufu sana duniani kifupi cha chuo hicho hujulikana hivi UDSM.Chuo hiki kimebujikwa na rundo la wanafunzi wapya waingiao kila mwaka na hivyo kusababisha hata kuwa na upungufu wa majengo.Hivi ni lazima kweli wanafunzi wote wamalizao kidato cha sita na kuwa na sifa za kujiunga na Vyuo kwa masomo ya elimu ya juu wajiunge UDSM?Hivi ni kitu gani kilichopo pale ambacho vyuo vingine vyenye sifa kama ya UDSM hamna?.Kwa binafsi yangu mimi naona migogoro mingi iliyowahi kwisha tokea ni kutokana na wingi wa wanafunzi hao na hivyo kupelekea uongozi wa chuo kushindwa kuwahudumia kikamilifu.Hivi kuna haja gani ya wanafunzi kurundikana pale.Mimi nawasihi wanafunzi wenzangu migogoro katika sekta ya elimu hususani ya juu hushusha kiwango cha elimu kitolewacho mahala husika nchi yetu imekuwa ikijitahidi sana katika sekta ya elimu na hivyo kuwa na vyuo mbalimbali vyenye sifa.Mimi naomba kuliko kurundikana chuo kimoja na kutopata kile tulichokusudia au kukipata katika wakati tusiokusudia ni bora kabla ya kujiunga na UDSM ni jukumu letu kutafuta vyuo vyenye sifa kama ya UDSM ili pia ikiwezekana basi twende huko kuliko kujazana sehemu moja.
Na vile vile uongozi wa chuo hivi ni kigezo gani chatumika kuwa na idadi inayotakiwa ya wanafunzi chuoni?Kwa upande wangu nahisi ni kutokana na uwezo wa vyumba vya madarasa katika kuchukua wanachuo.Sasa kama ndivyo hivyo kama nijuavyo mimi inakuwaje wanafunzi wakawa wengi kuliko Vyumba vya madarasa?Naomba uongozi wa UDSM pamoja na SERIKALI iliangalie swala hili kwa macho yote na kwa mikono yote katika kulipatia ufumbuzi.