leroy
JF-Expert Member
- Dec 8, 2010
- 1,589
- 2,140
- Nimekuwa mfuatiliaji mzuri sana wa siasa za Tanzania katika miaka ya hivi karibuni.
- Nakubali kabisa kuwa hali ya siasa ilivyo hivi sasa imechangiwa na mapungufu ya serikali ya chama tawala, ccm.
- Nimekuwa nikijiuliza mara kwa mara kwa nini mtu ukibainisha mapungufu ya chama cha CHADEMA unaonekana mbaya na kuishia kushambuliwa kwa matusi na lugha za kejeli. Hii ni matokeo ya ukereketwa ama nini...
- Je, ubaya upo ccm pekee? Chadema ni watakatifu? siasa hizi za kuangalia kibanzi kilichopo kwenye jicho la mwenzio na kusahau boriti lililopo jichoni mwako itatufikisha popote?
- Mi naamini kila taasisi ina mapungufu yake, kwa hiyo utamaduni wa kukosoa ulioibuka hivi sasa miongoni mwa watanzania nashauri ulenge pande zote la sivyo tutakuwa hatutendi haki.
- Kukosolewa ni sehemu muhimu ili uweze kusonga mbele......
nawasilisha.