Historia ya Noti na Sarafu za Tanzania

Noti ya Mia Tano ni ya Kitambo ilifutwa lakini imegoma kung'oka tena ilipotangazwa kuondolewa sokoni ndipo zilifumuka Mia tano za Noti Nyingi mpya mpya sana Sikuelewa nini maana yake nikahisi kuna issue hapo.... hadi sasa hivi nahisi kuna jipu kuu... ila No Sweat tu tunasonga nazipenda sana Noti zenye Rangi ya Kijani zinapendeza haswa nikikumbuka noti za Shillingi Kumi green color
 
10 Tz Shilling
tz_10shs_nyerere_2.jpg
Noti niliyopenda kuliko zote... Nakumbuka nilikuta Kibunda Chumbani kwa Mdingi wangu nikazihesabu zote zilikuwa mpya Hesabu yenyewe iliishia elfu tatu first time kushika pesa Nyingi nilishangazwa... nakumbuka ndio nilikuwa naongoza class kwa Hesabu so nilizihesabu twice nijue sijakosea...
 
Dah Mkuu Asante Sana, Wale Walimu wa Uchumi Hii Inawahusu Sana Mana Shuleni Tunafundishwa Histori za Sarafu na Noti za Nchi Zingine. Thanks Mkuu
 
Wiki chache zilizopita niliwaletea historia ya fedha ya sarafu hapa nchini kwetu nikaahidi kumalizia na historia ya noti. Kwa bahati mbaya majukumu yamenizidi nikashindwa kupata nafasi ya kuiandika ingawa nilikuwa nimeshaifanyia utafiti wa kutosha. Leo hii nimeamua kulivalia njuga ili niikamilishe, samahani sana kwa wanachama kwa vile historia hii ni ndefu kidogo kuliko ile ya sarafu kwa vile noti zilipitia mabadiliko mengi sana kuliko sarafu.

Kwa muda mrefu fedha zilizotumia katika nchi hii zilikuwa ni sarafu. Noti za karatsi zilianza kutumiaka mwaka 1905 wakati wa utawala wa mjerumani kwa upande wa bara. Noti hizo zilitolweka katika thamani ya Rupie 5, 10, 50, 100 na rupie 500 kama ionekanavyo hapa chini. Noti za rupie 500 zilikuwa chache sana na sikufanikiwa kupata picha yake

Rupie 5
doa_5rupien.jpg

Rupie 10
doa_10rupien.jpg

Rupie 50
doa_50rupien.jpg

Rupie 100
doa_100rupien.jpg

Kwa upande wa zanzibar, mwaka huo huo wa 1905, noti za Rupee za kizanzibari zilitolewa katika thamani za Rupee 5, 10, 20, 50, 100 na rupee 500 pia. Kwa bahati mbaya sikuweza kupata picha zake zote, naonyesha mfano wa noti za rupee 5 tano tu niliyofanikiwa kupata.

5 Zanzibari rupee


zz10.jpg


Wakati wa vita ya kwanza ya dunia, serikali ya kijerumani ilitoa noti za dharura ambazo zilikuwa ni za karatasi ya kawaida kabisa. Noti hizi zilikuwa katika thamani za Rupie 1, 5, 10, 20, 50 and Rupie 200 ingawa hizi za Rupie 200 zilikuwa adimu sana na sikufanikiwa kupata picha yake

1 Rupie
doa_1rupiene_1.jpg

5 Rupien
doa_5rupiene.jpg

10 Rupien
doa_10rupiene.jpg

20 Rupien

doa_20rupiene.jpg

50 Rupien

doa_50rupiene.jpg

Noti hizi za dharura zilikuwa hafifu sana na wakati mwingine zilikuwa zinafyatuliwa kwa muhuri tu kama hii hapa chini ya Rupie 1.

doa_1rupiene_3.jpg


Inaelekea kuwa mji wa Tabora ulikuwa na umuhimu wa pili kwa dar es salaama wakati wa serikali ya kijerumani kwa vile unaonyeshwa katika Noti zote. Kama mtakumbuka, ile sarafu ya dhahabu ya Rupie 15 ilikuwa inaitwa "Tabora Pound."


.....INAENDELEA
kweli hata mimi nimependa
uko vizuri Mkuu
 
Kichuguu nyuma ya noti ya shilingi 1000 haikuwa kiwanda cha nyama cha Kawe bali mgodi wa makaa ya mawe Kiwira
 
Kichuguu nyuma ya noti ya shilingi 1000 haikuwa kiwanda cha nyama cha Kawe bali mgodi wa makaa ya mawe Kiwira
Asante kwa kurekebisha rekodi, hata hivyo jambo hilo lilijibiwa zamani kidogo na mchangiaji mwingine, nadhani ilikuwa kipindi hicho hicho nilipopost thread hii, yaani mwaka 2007 (karibu miaka kumi iliyopita!)
 
Asante kwa kurekebisha rekodi, hata hivyo jambo hilo lilijibiwa zamani kidogo na mchangiaji mwingine, nadhani ilikuwa kipindi hicho hicho nilipopost thread hii, yaani mwaka 2007 (karibu miaka kumi iliyopita!)
Nimegundua mimi mwenyewe nililijibu jambo hili mwaka 2011 ndipo tukapigia debe uwepo wa jukwaa la Historia.
 
Lakini Alikuwa Rais Wa Kwanza Wa Zanzibar

Na Ni Muhimu Sana Kwa Wananchi Wa Zanzibar Nao Kuona Kuwa Viongozi Wao Wanathaminiwa

Pesa Zimejaa Mijinyati Na Mijingombe Tuuu Halafu Watu Wa Zanzibar Wanachorewa Kijimlango Au Kijitawi Cha Rafuuu

Where Is The Fairness?

Nyie Mambo Haya Mnaona Mambo Haya Ni Madogo Lakini Yanasemwa
Eti nyie Wanzibar wenzangu mbona mwajitoa ufahamu, mnadai haki kwa kichuguu, yeye alichofanya Ni kuleta historia hapa. Hizo fedha zingine hazitumiki sasa hivi alaah mbona mwatuabisha, si mfungue mada muelezee jinsi mlivyonyimwa haki Kama ipo.
 
nakukumbuka Enzi zile walikua wanasema Hela 7 au Hela 10 nk sio pesa au sh. 10 au sh 100 kama sasa ivi
 
hakika ni darasa huru kabisa lenye kudhihirisha historia nzuri a noti ya tanzania,ila mkuu naomba nikukumbushe na hizi noti za mwendo kasi za coin ya miatano
 
asante sana mwanzisha mada,,,,,
dah! kumbe mimi wa karibuni sana,,,,,shikamoo kwa walionitangulia haswa, note nyinginezo mimi sikuzifahamu jamani, history is Holly
 
Back
Top Bottom