Djumbe
Member
- Apr 8, 2011
- 39
- 62
Jina sahihi la huyu mwigizaji ni lipi? Mwigulu Nchemba ni jina la kisukuma na yeye ni mnyiramba au hilo ndio jina la kisanii ndo maana usanii mtupu kila sehemu... mimi namsihi arudie jina lake halisi la Lameck Mkumbo kama anataka kutumikia jamii na sio usanii huu anaotufanyia...
Lameck Mkumbo Madelu ni jina halisi la mh Mwigulu Nchemba.
Akiwa anasoma shule ya msingi Makunda kata ya Kyengege tarafa ya Kinampanda wilaya ya Iramba mkoa wa Singida, Mh Lameck Mkumbo Madelu alifeli mtihani wa taifa darasa la saba, baada ya kufeli huko akawa anatafuta njia ya kurudia.
Kwa bahati nzuri kulikuwa na darasa la kata la kata ya Kyengege lililokuwa linajumuisha shule za Makunda, Mgundu na Kyengege yenyewe. Kutokana na kuwepo darasa hilo la kata ikawa kuna nafasi kwani mwanafunzi Mwigulu Nchemba (msukuma) alikuwa ameacha shule akiwa darasa la sita kwani mwinuko wa kielimu kwa wasukuma ulikuwa chini sana wakati huo. Ndipo Mwl Malumbi alipoweza kumuuzia jina la Mwigulu Nchemba bwana Lameck Mkumbo Madelu.
Baada ya kurudia masomo bwana Lameck alifaulu kwa kutumia jina la Mwigulu Nchemba lakini baadae akiwa Secondari aliliongeza likawa Mwigulu Lameck Nchemba
Source: Admission books
1. Makunda Primary School
2. Darasa la kata Kyengege
3. Ilboru secondary
4. Wakazi wa Makunda