Dr Lizzy
Platinum Member
- May 25, 2009
- 30,801
- 59,269
Tumeshazoea kusikia watu wakiambiwa "Usiusemee moyo wa mwenzio" pale hisia za kimapenzi (kupenda) zinapokua zinahusika. Na hiyo kauli kama wengi tunavyojua hua inamaanisha kwamba hakuna anaeweza kujua nini mwingine anahisi ndani ya moyo wake kwa uhakika hata kama matendo yake hayatii shaka kuhusu hilo. Binafsi hua napenda kumwamini mtu mpaka atakaponipa sababu ya kutofanya hivyo, kwahiyo mtu akiniambia anahisi hivi au vile, ziwe hisia nzuri au mbaya ndizo ntazichukulia kama zilivyo.
Nwy leo nataka kuongelea zile ambazo ni hasi kidogo. Kwanini watu hua wanaona wana haki ya kumuamulia/kuona wana uhakika na kile mwingine anachohisi? Kwa mfano unaweza ukasema kitu cha kawaida tu. . .alafu mtu akadakia "mbona unajibu/ongea kwa hasira?"/ "una hasira wewe!!" na kukomalia hayo maneno hata pale mhusika anaposema sio? Au utasikia "fulani hata hakuumia mpenzi/ndugu yake alipofariki" kisa hakutoa machozi. Ina maana mtu hawezi kua hacheki cheki na bado asiwe na hasira? Mtu hawezi akaumia moyoni na bado mnaomuangalia msijue kisa hajatoa chozi? Chozi hili hili ambalo hata kwa vitunguu linatoka? Mtu hawezi akawa kimya labda kwaajili ya mawazo binafsi bila ya kuhisiwa kakasirika ama kaboreka? Mtu hawezi akawa na matatizo binafsi bila ya wewe kulazimisha kwamba ndie mkasirikiwa/mhusika?
Naamini UELEWA ni silaha kubwa sana, yani inaweza ikakulinda na aibu/hasira na hasara wakati wowote ule. .na KUTOKUA muelewa ni hasara inayoweza ikakufanya hata uonekane mjinga wakati mwingine.
Binafsi hua naboreka sana pale mtu anaponilazimishia hisia ambayo sinayo kwa wakati ule. . .hata kama nilikua napanga kumwambia kitu ntaahirisha kama sio kuacha kabisa.
Unapoona mtu yupo tofauti na ambavyo ungependa/ulitarajia uliza kulikoni badala ya kuassume na kulazimisha jibu liwe lile ulilomwandalia. Epuka kulazimisha kua wewe ndio tatizo, maana usipoacha kulazimisha UTAKUA tatizo kwa kukosa uelewa. Penda kuuliza badala ya kuassume. . .
Nwy leo nataka kuongelea zile ambazo ni hasi kidogo. Kwanini watu hua wanaona wana haki ya kumuamulia/kuona wana uhakika na kile mwingine anachohisi? Kwa mfano unaweza ukasema kitu cha kawaida tu. . .alafu mtu akadakia "mbona unajibu/ongea kwa hasira?"/ "una hasira wewe!!" na kukomalia hayo maneno hata pale mhusika anaposema sio? Au utasikia "fulani hata hakuumia mpenzi/ndugu yake alipofariki" kisa hakutoa machozi. Ina maana mtu hawezi kua hacheki cheki na bado asiwe na hasira? Mtu hawezi akaumia moyoni na bado mnaomuangalia msijue kisa hajatoa chozi? Chozi hili hili ambalo hata kwa vitunguu linatoka? Mtu hawezi akawa kimya labda kwaajili ya mawazo binafsi bila ya kuhisiwa kakasirika ama kaboreka? Mtu hawezi akawa na matatizo binafsi bila ya wewe kulazimisha kwamba ndie mkasirikiwa/mhusika?
Naamini UELEWA ni silaha kubwa sana, yani inaweza ikakulinda na aibu/hasira na hasara wakati wowote ule. .na KUTOKUA muelewa ni hasara inayoweza ikakufanya hata uonekane mjinga wakati mwingine.
Binafsi hua naboreka sana pale mtu anaponilazimishia hisia ambayo sinayo kwa wakati ule. . .hata kama nilikua napanga kumwambia kitu ntaahirisha kama sio kuacha kabisa.
Unapoona mtu yupo tofauti na ambavyo ungependa/ulitarajia uliza kulikoni badala ya kuassume na kulazimisha jibu liwe lile ulilomwandalia. Epuka kulazimisha kua wewe ndio tatizo, maana usipoacha kulazimisha UTAKUA tatizo kwa kukosa uelewa. Penda kuuliza badala ya kuassume. . .